Yericko Nyerere.
Kazi yenu kubwa chadema ni kusifia nchi jirani bila Tafakuri.
Mkiamini katika nyinyi pekee kuyaona maono hayo.
Na kudharau wasio upamde wenu ki itikadi.
Umeisifia sana Msumbiji ya Philipo Nyusi iliyojaza majasusi Dunia nzima ila imeshindwa kupigana na kundi la Islamic state walioivamia na kulikalia jimbo la Cabo Delgado.
Nchi yenye majasusi Duniani kote ila imeshindwa kulinda uwekezaji mkubwa wa uchimbaji gesi uliowekezwa nchini kwake.
Nchi yenye majasusi kote duniani lakini imepigwa na magaidi hadi ikaomba msaada wa nchi ndogo ya Rwanda ili kujiokoa.
Umeisifia Rwanda kwa kujenga kiwanda cha uchenjuaji madini wakati haina madini yoyote ardhini kwake.
Ila hukutaka kuutumia ujasusi wako kueleza kwamba kiini cha machafuko nchini Congo DRC.
Ni kwa sababu Rwanda inatumika na mataifa makubwa ya nje ili kupora madini ya Congo DRC!.
Umeshindwa kutumia ujasusi wako kutueleza kiini cha majeshi ya kulinda amani nchini Congo DRC (Monusco).
Yamekuwa yakijiingiza kwenye utoroshaji wa madini ya nchi hiyo kwa miongo kadhaa,badala ya kutimiza wajibu wao uliowapeleka huko.
Pia umesifia majasusi wa Kagame walivyojaa Dunia nzima.
Lakini hukutwambia jinsi anavyowatumia kuwaua political opponents wake pamoja na kuwateka popote pale Duniani.
Huku hao mabingwa wa Demokrasia wa Dunia wakikaa kimya.
Sababu ya kutotaka kumuudhi mtoto wao Kagame anayewasaidia kuiba raslimali za Congo DRC!
Umeisifia Uganda kwa uwekezaji mkubwa ilioufanya kwa kuanza kutengeneza magari yenye teknolojia ya Solar nk.
Lakini umesahau kutuambia ni kwa nini waganda hao hao wanavyomkataa
museveni kwa ukiukaji mkubwa wa Demokrasia nchini mwake huku mataifa hayo makubwa yakifumbia macho.
Tofauti na wanavyotupigia kelele sisi Tanzania kwa mambo ambayo kimsingi ni madogo kabisa kulinganisha na kinachotokea Rwanda na Uganda.
Umesifia Kenya kwa kuikaribisha Microsoft kuwekeza nchini humo,lakini hujatuwekea mfano hata mmoja wa faida ilizozipata Kenya kwa kuwa mnufaika mkuu wa uwekezaji huo.
Umesifia uwekezaji uliokuwa umepangwa wa Bandari ya Bagamoyo na ukasitishwa na Magufuli kwa sababu ambazo umeziita za kipuuzi.
Sasa ebu tumia Ujasusi wako mkubwa kwa sasa na umshawishi mama Samia aulete Bungeni huo mkataba ujadiliwe kipengele kwa kipengele na ikibidi wananchi tuupigie kura kabla ya kuingizwa mkenge kama tulivyofanywa kwenye Gesi na Mafuta.
Niishie kukupa taarifa kwamba,hata Magufuli aliona mbali kuhusu madini yetu na ndio maana aliamua kujenga masoko ya madini nchi nzima nahivyo kuondoa urasimu katika sekta ya wachimbaji wadogo wadogo wamadini..
Ili wananchi wauze madini kwa kulipa kodi halali na kwa bei halali ya Soko huku akiondoa utoroshaji wa madini kwenda nchi kama Rwanda na Kenya uliokuwa umekithiri.
Kwa kupitia walanguzi haramu wa Madini nchini kwa ushirika na mtandao wa nje.
Pia Magufuli aliona mbali kwa kuanza kujenga hizo refineries sehemu mbalimbali nchini na baadhi tayari zinafanya kazi.
Ikiwemo mojawapo kubwa iliyoko
mwanza na inachenjuwa dhahabu kwa kwenda mbele.
Pia umesahau kutumia ujasusi wako kutufahamisha kwamba Angola inafanyauwekezaji mkubwa.
Katika jimbo la Cabinda kwa kutumia bandari ya Lobito,wanajenga reli ya kisasa ambayo itakuja mpaka kusini mwa Congo DRC.
commonmwananchi
10101.