Nani Anajua Namna ya Kumsaidia Huyu Mdada?

mnahukumu upande mmoja .....amshauri huyo mshenzi wakapime DNA ka mwanamke hajala kona:yuck:

huyu mtu mpaka ameandika hapa ni kweli huwezi kuamka toka usingizini ukamsingizia mtu kuwa huyu mtoto ni wako.
Lakini mbona wapo wanaokata watoto kama mheshimuwa mahita:confused:
 
Sheria sijui inasema ni shilingi mia moja kwa mwezi kumlisha kumsomesha na hata kumzika akifa? I think so lakini niko karibu na ukweli
 
lea mwanao wewe acha kutegemea huyo ambae umeshamuita mshenzi....
Unamuita mshenzi lakini hela yake unaitaka!!!!:angry:
 
Sheria sijui inasema ni shilingi mia moja kwa mwezi kumlisha kumsomesha na hata kumzika akifa? I think so lakini niko karibu na ukweli

is better than nothing,ht km shing' mia sio kitu kutokana na mshahara wake huyo baba lakini kwa mtu asiyetaka rensposibility ni adhabu tosha,aende tu mahakamani huyo dada....mibaba mingine sijui ikoje!
 
haya ndio maelezo yake:-

Habari zenu marafiki ?

Mimi ni mwanamke mwenye miaka 27 kwasasa nina mtoto mmoja wa kike ambae nilizaa na mshenzi mmoja miaka mitano iliyopita.
Huyo jamaa jina lake linaanziwa na K, alinikimbia toka kipindi cha mimba na alikuwa akiwaambia watu kuwa mimba sio yake,kwa kudra za mwenyezi Mungu nilijifungua salama na mtoto amefafana na baba yake kupita kiasi.
Toka kipindi cha mimba mpake leo hii mtoto ana miaka 5 sijawahi kuona hata senti ya huyo kaka kwa ajili ya malezi ya mtoto, huyo kaka ana kazi nzuri sana na analipwa mshahara mzuri tu kwa kweli.
Swali langu ni kwamba nikimpeleka mahakamani je ataamuriwa kunipa pesa za mtoto? Je pesa za nyuma na hizo ataambiwa anilipe? Je ni kiasi gani kwa mwaka anaweza kuamuriwa anipe. Mshahara wake kwa mwezi sio chini ya milioni 3
By 2007 kama sikosei, ukienda ustawi wa jamii fidia ilikuwa ni sh 200/= (mia mbili) kwa mwezi kwa mtoto mmoja. Nisingekushauri uende huko hata siku moja, nenda haki za binadamu na kuna wana sheria wenye moyo wanaoweza kukusaidia vizuri sana
 
Nampa pole sana huyo dada - baadhi ya binadamu walioumbwa na Mungu wamejawa na roho ya kishetani - hivi huyo baba anamkana vipi mwanae??? Lazima atakuwa selfish sana na mwenye roho ngumu sana ndio maana huyu dada anadiriki kumwita "mshenzi" - mtu mstaarabu hawezi kufanya kitu cha aina hiyo.

Dada huyo Baba ana haki ya kumtunza mtoto wake - asikimbie majukumu yake - mtoto akishakuwa mtu mzima - umemsomesha - ana kazi nzuri - utamwona anajitokeza anadai mtoto ni wake - some men can really be stupid

Mpeleke kwenye sheria na sheria imlazimishe kuwajibika - alipokuwa anafanya tendo la ndoa hakujua kuna matokeo???
Ushauri: Kabla hujapendana na mwingine - uwe makini - asije akakuzalisha mtoto mwingine akakukimbia tena - TAFAKARI - SIO VYOTE VING'AAVYO NI DHAHABU
Milioni 3 anazopata zimtunze mwanae - sio amalizie kwenye pombe na wanawake wengine
 
haya ndio maelezo yake:-

Habari zenu marafiki ?

mtoto mmoja wa kike ambae nilizaa na mshenzi mmoja miaka mitano iliyopita.
Huyo jamaa jina lake linaanziwa na K, ..... mtoto amefafana na baba yake kupita kiasi.
.... huyo kaka ana kazi nzuri sana

mshenzi = jamaa = kaka

Napatwa na shaka kama unamfahamu hata huyu aliyekutia mimba!
 
wanaume wamekuwa wakali kweli kny hii mada,naona hilo neno mshenzi limawatia kiwewe,yeyote anayemtia mtu mimba na kumkana=MSHENZI!!
 
Samahani mdadaa, kwanza pole, ni kweli sisi wanaume kuna nyakati tunakua washenzi :frown: Lakini dawa ya mshenzi si kumfanyia unyambilisi, sababu kwa case yako atakayeumia saana ni mtoto. Je wewe ni wa dini gani? kama ni mkristo naomba umpeleke mwanao ili aombewe na kufunguliwa na laana ya kukataliwa, maana alikataliwa toka mimba ni mbaya sana kwa makuzi ya mtoto, sababu za huyo mshenzi kukataa mimba mpaka mtoto sizijui na siwezi kukisia lakini kikubwa wanaume tunaogopa commitment hicho ni kikubwa, wadada usifikiri kuwa na kamkia kwetu wanaume ndio ujasiri wa kuwa the head of the family au mashujaa fulani, we are weak in another way. Fuatilia usemi "In every successfull man there is a woman but also In every unsuccessfull there is two" Msamehe bure huyo mshenzi na wewe lea mwana, huwezi shindwa umepiga 5 years already what else do you want from mshenzi?
 
mnahukumu upande mmoja .....amshauri huyo mshenzi wakapime DNA ka mwanamke hajala kona:yuck:

HAHAAAA MKUU UKO FASTA SANA!!!

Ushauri kuhusu TAMWA na ustawi wa jamii... wako slow na tena afadhali ya TAMWa hao ustawi usiwategemee sana...

kuhusu huyo "mshenzi", nadhani ni very simple akishapata msaada wa sheria, waombe consent ya kupima DNA then atakua na right zote za kudai matumizi, nje ya hapo huyo mshenzi ataendelea kuwa mshenzi which is not good

PELEKA SAMPLE YA DNA KWANZA NDIO UCONFIRM KUWA JAMAA NI MSHENZI
 
by 2007 kama sikosei, ukienda ustawi wa jamii fidia ilikuwa ni sh 200/= (mia mbili) kwa mwezi kwa mtoto mmoja. nisingekushauri uende huko hata siku moja, nenda haki za binadamu na kuna wana sheria wenye moyo wanaoweza kukusaidia vizuri sana

jamani mbavu zangu.... Hahahaaaaaaa, kweli tanzania ni zaidi ya uijuavyo

duh
 
Awasiliane na WLAC (Women for Legal Action) kwa namba zifuatazo 0785-066555 au 0757-726660. Hapa utapata msaada wa kisheria kupitia hizo namba.

Pia waweza kwenda Tanganyika Law Society (Chama cha Wanasheria Tanzania Bara) ambao nao wanaweza kukusaidia kupata haki yako ya matunzo ya mtoto. Haki hiyo unaweza ipata hata kwa miaka yote aliyogoma kumtunza mtoto.

Ofisi za TLS zipo maeneo ya Namanga Mtaa wa Ruhinde No. 299.
 
ni haki yake kuhakikisha baba mtoto anatoa pesa ya malezi ya mtoto. haijalishi kama aliikataa mimba awali au la.

mtoto anaweza kuwa anakosa hudua muhimu kwa kuwa mama labda hana pesa ya kutosha kumhudumia.

akifungua kesi mahakama itamwita jamaa, atapimwa dna na kama mwana ni wake kweli, atalazimika kumpatia pesa za matumizi na wala haitamamuru ampe mtoto huyu mwanamme.

haki ya mtu inapiganiwa haiji tu ....................pigania haki ya mtoto wako lakini epuka kumuita baba yake mwanao mshenzi hasa kama una nia ya kumshirikisha kwenye malezi ya mtoto wenu

Ni kweli ni haki yake lakini nashindwa kuelewa kama baba alishakataa mimba mwanzoni what makes it easier for him to accept mtoto sasa hivi? Mimi nafikiri kabla ya kuulizia kama atafidiwa au la angeuliza kama anawezampeleka for check up yaani wakathibitishe kuwa mtoto ni wa mr. Hapa tunasikiliza upande mmoja wa shilingi pengine huyo jamaa anayeitwa mshenzi hadi sasa anaamini kuwa mtoto sio wake na pengine anayo sababu nzuri tu ya kumfanya yeye aamini kuwa anachoamini ni sahihi (labda mdada alikuwa anawachanganya kwa wakati mmoja) So la kuanza ni kumthibitishia kuwa mtoto ni wake and then hayo ya fidia yanakuja baadae!!

Kwa sababu katika post yake sijaona sehemu alosema ameshathibitisha kuwa mtoto ni wake!! Eti anafanana naye je hiyo inatosha kumfanya awe baba wa mtoto? Ukizingatia
- wanawake wengi wanaocheat wana tendency ya kucheat na watu wanaoresemble na waume zao meaning kama ni mweusi mwenye big eyes bus atacheat na wa kufanana naye!!.
- Je kama bibiye alifumaniwa akicheat na shemejiye yaani ndugu wa huyo mshenzi? Si mtoto atafanana na ukoo wa kina mr. Mshenzi?

Akahakikishe kwanza kama mtoto ni wa Mr. Mshenzi, ndo aje aulize sheria inasemaje juu ya utunzaji wa mtoto.
 
haya ndio maelezo yake:-

Habari zenu marafiki ?

Mimi ni mwanamke mwenye miaka 27 kwasasa nina mtoto mmoja wa kike ambae nilizaa na mshenzi mmoja miaka mitano iliyopita.
Huyo jamaa jina lake linaanziwa na K, alinikimbia toka kipindi cha mimba na alikuwa akiwaambia watu kuwa mimba sio yake,kwa kudra za mwenyezi Mungu nilijifungua salama na mtoto amefafana na baba yake kupita kiasi.
Toka kipindi cha mimba mpake leo hii mtoto ana miaka 5 sijawahi kuona hata senti ya huyo kaka kwa ajili ya malezi ya mtoto, huyo kaka ana kazi nzuri sana na analipwa mshahara mzuri tu kwa kweli.
Swali langu ni kwamba nikimpeleka mahakamani je ataamuriwa kunipa pesa za mtoto? Je pesa za nyuma na hizo ataambiwa anilipe? Je ni kiasi gani kwa mwaka anaweza kuamuriwa anipe. Mshahara wake kwa mwezi sio chini ya milioni 3

...kisa cha kusikitisha ila naona mwanadada yupo kwenye kutaka kujua gharama zaidi kuliko hatma ya mtoto. Je, baada ya mahakama na vipimo kuthibitisha uhalali wa huyo Baba wa mtoto, atakuwa tayari huyo mtoto alelewe (shared parenting) na huyo kaka (Iwapo atataka iwe hivyo)?






 
Jamani inakuwaje hapa. Dada kazaa na mshenzi. Mtoto anafanana na MSHENZI. Jamani jamani, mtoto wa kike mzuri katulia nyumbani mnamwita mshenzi? Hivi mmefikia hatua hii?
Dada zangu jitahidini sana kufanya yanahitajika kwenye jamii. Fikiria wewe ni mtu na akili zako! Hukulazimishwa ulijua shairi dhahiri kuwa mwisho wa siku utanasa. Umenasa ukaamua kulea mimba hadi sasa mtoto ana miaka 5. Leo unaibuka unataka MSHENZI alipe gharama za matunzo! utamwambia mwanao naenda kwa MSHENZI baba yako kuchukua hela za matumizi? Believe me ulikuwa unamendea hizo m3 za mshenzi.
OK Mama Kapimeni DNA muone kama kweli mmezaa mshenzi nanyi mtakuwa washenzi kweli! lol
Hayo ni matokeo ya UASHERATI. Huna mpango wa kuzaa TUMIA KONDOM ama! We unaacha malango wazi usiibiwe.
Lea Mwanao mama tena mwombe msamaha kwa kumwita mshenzi
 
...Kwa sababu katika post yake sijaona sehemu alosema ameshathibitisha kuwa mtoto ni wake!! Eti anafanana naye je hiyo inatosha kumfanya awe baba wa mtoto? Ukizingatia
- wanawake wengi wanaocheat wana tendency ya kucheat na watu wanaoresemble na waume zao meaning kama ni mweusi mwenye big eyes bus atacheat na wa kufanana naye!!.
- Je kama bibiye alifumaniwa akicheat na shemejiye yaani ndugu wa huyo mshenzi? Si mtoto atafanana na ukoo wa kina mr. Mshenzi?
...

....eeeehhhhhhh????!! MwJ'1 naomba tu niku Quote hii for my future use/referrence.
 
Mpe mtoto mapenzi yako yote kama mwanao na katu usihangaike na mtu ambaye hakutaka kujihusisha nawe! Iko siku atakuja na wala usimhesabie! Ikiwa kweli unao uwezo wa kumlea mwanao. La nenda kamdai ikiwa kweli umeshindwa kumlea! Na usimuhubirie chuki kwa babaye mwanao mwache akue akijua wazazi hamkuweza kuwa pamoja; Ukubwani yeye ataamua nini cha kufanya; wewe timiza wajibu wako wa kuwa mzazi mwema !
 
Kweli neno mshenzi limetuchoma sana wengine kwa kuwa hatujapokea maelezo ya upande wa pili! nwayz huo ushenzi ulijugundua lini? ni kabla hujampa tundi?!
 
Brigita good observation, how can you call baba wa mtoto wako Mshenzi!!?

By the way sijamuelewa wifi anachotaka, kaka si alishamkataa mtoto tangu akiwa mimba? Sasa wewe unataka kumpeleka mahakamani ili amkubali au ili akupe pesa za fidia? Na je ukishalipwa unamkabidhi kwa babake au ndo inakuwaje sasa? Mimi nafikiri ungefurahi kuwa umeachiwa zawadi ya mtoto. na wala usisikie uchungu kumlea mwanao, she is yours for God's Sake

Kuna wakati tunaacha mambo mengine kuwa untold truths...the lady sounds bitter... mbona basi uhangaike tena na kumpeleka mahakamani? Achana nae, when you have hate in your heart it does not make you a better person than what he is or what he did.

One thing I know, you could have unreconcilable differences, lkn name calling hasa ikiwa ni mother or father to your children is the lowest we can get as human beings. Forgive and forget.

What he did was not right, but do not sink to his level.
 
Komaa umlee mtoto wako. Adhabu nyingine huwa ziko hapa hapa wala usihofu. SAtakuja kukuangukia wakati ukifika
 
Back
Top Bottom