Nani anafaa kuwa Mrithi wa IGP Simon Sirro?

Nani anafaa kuwa Mrithi wa IGP Simon Sirro?

Said mwema ndie igp bora kwa kipindi nilichokishuhudia lakini ndio hivyo umri wa kustaafu.

Omari mahita nae alikua na ubora wake japo kipindi kile kulikua na changamoto sana za uhalifu. Ubora wake unatokana jinsi alivyopambana na huo uhalifu kwa nyakati zile.

Kwa Sasa arudishwe tu Ernest mangu amalizie muda wake kwa kweli.
Amestaafu tayari
 
Hili ni la
Sirro is among of the fewer professional police we have.

Sirro ni viwango vya Donald Rumsfeld aliyekuwa waziri wa ulinzi wa Marekani 2001 hadi 2006.

Sirro hajawahi kushindwa kwenye kazi, waulize majambazi waliovamia watalii mbugani watakuambia Sirro ni nani.

Jiulize kwa miaka hii ya Sirro wale majambazi waliokuwa wakitamba wako wapi?
Sirro chapa kazi baba.

Msiimuonee sirro kwa kuwa tumeshindwa chaguzi. Ccm haikutumia jeshi la polisi ioicheza na watendaji


Sent from my LG-F800S using JamiiForums mobile app
 
Kwasasa nawaona wawili tu wenye hekima za kutosha kuongoza jeshi la polisi
1. Salum Rashid Hamdini (RPC Arusha)
2. Ladson Mwabulambo Mponjoli (RPC Geita)

Lakini kwakua mheshimiwa mwenyekiti anapenda wateule makondoo, basi sitoshangaa kumwona Mambosasa akiukwaa u IGP.
Jamaa wa Geita namkubali saaaana
 
Bongo movie iliyofeli kiwango cha kununuliwa hata na muhindi.

Mzigo wa mwenzako kwako ni ganda la usufi . Tulioathirika tumewaona na namna walivyowatesa ndugu zetu , hakuna asiyejuwa hapa mjini Zanzibar kuwa askari wengine kwenye magari ya Polisi, wakiongea kiswahili cha kiburundi na kifaransa
 
uhusu elimu yake, Simon Sirro alisoma Shule ya Sekondari ya Ilboru jijini Arusha na Tosamaganga kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu kusoma Shahada ya awali katika Sheria.
hapa kuna utata! elimu ya Sirro kwa O'level ni Uru Seminary na Kilimanjaro Boys
 
Hivi unajua kwamba jeshini kuna ngazi za uongozi (ranks)?

Huwezi kumpa Mambosasa u-IGP halafu uwaache makamishna na manaibu makamishna pale Makao Makuu.

Hilo likifanyika basi itabidi Mhe. Rais pia awaondoe viongozo wote ngazi za juu za Polisi ili tu kumpa uhalali Mambosasa awe IGP kitu ambacho sioni kama kinaweza kufanyika.

Hivyo mtu ambae naona ni candidate wa u-IGP baada ya Sirro ni Sabas ambae kwa sasa ni Kamishna wa Operesheni.
Unakumbuka uteuzi wa Mahita Uliwaacha Makamishina wangapi?
 
Sirro is among of the fewer professional police we have.

Sirro ni viwango vya Donald Rumsfeld aliyekuwa waziri wa ulinzi wa Marekani 2001 hadi 2006.

Sirro hajawahi kushindwa kwenye kazi, waulize majambazi waliovamia watalii mbugani watakuambia Sirro ni nani.

Jiulize kwa miaka hii ya Sirro wale majambazi waliokuwa wakitamba wako wapi?
Sirro chapa kazi baba.


Sent from my LG-F800S using JamiiForums mobile app
Hapo kwa majambazi waliokuwa wanavamia watalii mbugani usimpe sirro sifa za uongo. Polisi walishindwa kuwadhibiti hadi wakasaidiwa na askari wa TANAPA na JWTZ na pia walidhibitiwa kipindi cha IGP Said Mwema
 
Ma IGP walionivutia,
Harun mahundi.
Samweli pundugu,huyu nilifika hadi kuhiji kaburini kwake,
Said mwema.
Ezekiel Mangu.
Umemkwepa mzee Mgaya muanzilishi wa makampuni binafsi ya ulinzi

Na yeye akajianzishia kampuni yake Kuubwa sasa SGA
Mwaka huu imeandamwa na kuibiwa hela kwa walinzi wake mwenyewe kupaki gari za kusafirishia hela mpaka ikaanzishwa database ya walinzi wote na mzee wa watu hadi akafariki
 
Afande Simon Sirro is the best at present moment, utake usitake kajitahidi sana, majambazi yamemalizwa, vibaka kwisha, nchi atleast imetulia na hii ndio kazi kubwa alipewa na Mh. Rais JPM, lingine Afande Sirro is an intelligent guy ukatae ukubali, Sirro knows well his job, he is a really professional police, mchapa kazi sana, pia ni msikivu sana, well mannered, hajivuni, mtenda haki, in general, he is the best IGP niseme ukweli, sioni dalili zozote zile za wanaomuombea mabaya ili Mh. Rais ambadilishe, naona Mh. Rais atamaliza na Afande Sirro hadi 2025. Niseme tu, Dua ya kuku ( kuku = Chadema) haimpati mwewe.

Afande Sirro you are the best IGP, period, keep going..!!
Well said mkuu

Sent from my Infinix X653 using JamiiForums mobile app
 
Acha wivu.
Kama majambazi waliingia mbugani walipo TANAPA na kufanya uhalifu kwa watalii na kisha polisi kuwasaka na kuwakamata, unaachaje kumpongeza Kamada wa Operation hiyo?
Askari wa JWTZ ulisikia wapi wakisaka majambazi wewe?
Ulisikia wapi? Wee uliona wapi?

Sent from my LG-F800S using JamiiForums mobile app
 
Hivi unajua kwamba jeshini kuna ngazi za uongozi (ranks)?

Huwezi kumpa Mambosasa u-IGP halafu uwaache makamishna na manaibu makamishna pale Makao Makuu.

Hilo likifanyika basi itabidi Mhe. Rais pia awaondoe viongozo wote ngazi za juu za Polisi ili tu kumpa uhalali Mambosasa awe IGP kitu ambacho sioni kama kinaweza kufanyika.

Hivyo mtu ambae naona ni candidate wa u-IGP baada ya Sirro ni Sabas ambae kwa sasa ni Kamishna wa Operesheni.
Uko wrong kabisa

Sio lazima awe kamishina, anaweza kuongezwa mtu vyeo kutoka chini mpaka kamishina ili achaguliwe u-IGP tu au akarushwa kutoka chini mpaka IGP

Records zipo
 
Salaam Wakuu salaam

Tumsaidie Rais Magufuli kutafuta Watendaji wenye Uchungu na Nchi Watetezi wa Wanyonge.

Kumbuka sisi Wanachama wa JamiiForums ndio tulimpendekeza Sirro kwa Rais na akateuliwa na katuangusha.


Ni Wakati wetu wa kumsaidia kupa mrithi wake.

Weka Wasifu na kwanini unadhani huyo ulomtaja anaweza kuvaa Viatu vya Sirro?

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania Simon Sirro, ana mambo mazuri kafanya katika Nchi yetu. Lakini kila mtu ana madhaifu yake kama ilivyo kwa Sirro.

Ila kutokana na Hotuba rais aloitoa Wakati anamuapisha Waziri Mkuu Majaliwa, ni ukweli usio na Shaka kwamba lolote laweza kutokea kwa IGP Sirro.

Afande Sirro kwa hii miaka Mitano, alitakiwa awe amejiuzulu. Hata rais alimpa nafasi ya kujitafakari akashindwa.

Kuna Makosa ambayo Sirro kafeli kutimiza ambayo yamefaya nimuondolee alama.

1. Lissu kupigwa risasi na Watu Kutekwa na kupotea. Hii imechafua sana Nchi yetu. Hii hali ilimchafua hadi rais kwani Uzembe wa Sirro kufanyakazi, kumefanya watu wadhani kwamba Watekaji wanalindwa. Hii kosa alitakiwa ajiuzulu. Ila amshukuru rais alimvumilia.

2. Kuna Sakata la sare za Polisi. Rais Magufuli aliibua Sakata la sare za Polisi ambazo ulifanyika ufisadi wa karibia Bil 60, akamuagiza afanyie kazi, lakini hafanyi chochote. Alitakiwa ajiuzulu.

3. Sakata la Lugumi. Kuna ufisadi wakaribia Bilioni 34 za kifunga mitambo ya alama za Vidole ambalo liliibuliwa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

4. Majeshi yote ya Tanzania yana miradi ya maendeleo ili kupunguza utegemezi kwa Serikali. Lakini kwa Miaka mitano ameshindwa kubuni miradi hata ya kuwasaidia Askari.

NB: Sitaki kuzungumzia Rushwa, Uchakavu wa Ofisi za Polisi na Uchakavu wa sare za Polisi,kubambikia kesi nk.

Hata akiendelea kuliongoza jeshi la Polisi kwa upande wangu naona kakosa uhalali wa kuendelea kuwepo hapa alipo. Namuombea kila la heri katika maisha yake ya baadaye. Na tunashukuru kwa Mchango wange hasa wa kudhibiti Ujambazi Nchi.

Kwa Upande wangu bado nafuatilia CV ya Afande wa Taifa Fortunatus Muslimu ambaye amefanikiwa kudhibiti ajali barabarani. Tangu 2017 yeye yupo Field. Ni Askari Mcha Mungu, Mwenye Upendo, hekima na Msikivu. Nafuatilia CV yake. Sisi watu wa barabarani tunaona mchango wake. Madereva Walevi wameisha. Huwa hakai Ofisini..

Simon Nyakoro Sirro kabla ya kuwa IGP, alikuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam amekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi wa 10 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mwisho wa makala hii tutawaorodhesha wengine waliomtangulia kushika wadhifa huo.

Sirro alizaliwa eneo la Kiabakari wilaya ya Butiama mkoani Mara mwaka 1963.

Kuhusu elimu yake, Simon Sirro alisoma Shule ya Sekondari ya Ilboru jijini Arusha na Tosamaganga kabla ya kujiunga na Chuo Kikuu kusoma Shahada ya awali katika Sheria.

Sirro amesoma pia seminari (masomo ya upadri) na kufikia ngazi ya juu kabla ya kuacha na kujiunga na Jeshi la Polisi.
Kamanda Sirro alisema kuwa kama isingekuwa baba yake basi leo yeye angekuwa ni Padri wa Kanisa Katoliki kwani ndiyo ndoto yake kubwa, lakini baada ya wazazi wake kumkatisha ndipo alipojiunga na jeshi hilo.

Unajua wazazi kule kwetu Musoma walikuwa hawakuelewi usipooa. Mzazi aliona mimi ni kijana mkubwa akasema haiwezekani,” alisema Sirro alipofanya mahojiano na Mwananchi kipindi cha nyuma.

Sirro amewahi kuwa Mkuu wa Upelelezi Kituo cha Polisi Buguruni mwaka 1998, Mkuu wa Upelelezi Tarafa ya Magomeni kwa miaka 5 na Mkuu wa Upelelezi Msaidizi Mkoa wa Tabora.

Mwaka 2002 alikuwa Mkuu wa Upelelezi Msaidizi Mkoa wa Dar es Salaam akiwa ni msaidizi wa Abdallah Zombe.

Sirro ni Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam wa tatu ambapo aliteuliwa na Rais Dkt Magufuli Februari 15 mwaka 2006 akichukua nafasi ya Suleiman Kova aliyeshika wadhifa huo tangu mwaka 2008. Kabla ya Kova aliyekuwa akiongoza Kanda Maalum ya Dar es Salaam ni Alfred Tibaigana.

Wakati Suleiman Kova akiongoza Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Sirro alikuwa msadizi wake ambapo baadae alirithi mikoba yake.

Kabla ya kuongoza Kanda Maalum Dar es Salaam, Sirro amewahi kuwa Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Tanzania. Moja ya opersheni kubwa alizowahi kuongozi ni Operesheni Kimbunga dhidi ya wahamiaji haramu mwaka 2012.

Lakini pia, Simon Nyakoro Sirro amewahi kuwa Kamanda wa Polisi wa Mikoa mbalimbali ambayo ni Tanga, Mwanza na Shinyanga.

Wakuu wengine wa Jeshi la Polisi ni;
1. Elangwa Shahidi (1964-1970), alistaafu.

2. Hamza Azizi (1972-1973), aling’olewa na Mwl. Nyerere kwa matumizi mabaya ya madaraka.

3. Samwel Pundugu (1973-1975).

4. Philemon Mgaya (1975-1980),
aliachishwa kazi kwa manufaa ya umma.

5. Solomoni Liani (1980-1984), alihitimisha kipindi cha mwisho cha Mwl. Nyerere.

6. Harun Mahundi (1984-1996), alistaafu.

7. Omari Mahita (1996-2006), alistaafu.

8. Said Mwema (2006-2013), alistaafu.

9. Ernest mangu (2013-2017), atapangiwa kazi nyingine, na

10. Simon Sirro (2017-2020) yupo madarakani.

Mkuu wa Jeshi la Polisi, Simon Nyakoro Sirro ameoa mke mmoja na ana watoto wanne.
Afande Ashraf yule trafiki njia panda ya kawe anatosha kabisa.
 
Hivi unajua kwamba jeshini kuna ngazi za uongozi (ranks)?

Huwezi kumpa Mambosasa u-IGP halafu uwaache makamishna na manaibu makamishna pale Makao Makuu.

Hilo likifanyika basi itabidi Mhe. Rais pia awaondoe viongozo wote ngazi za juu za Polisi ili tu kumpa uhalali Mambosasa awe IGP kitu ambacho sioni kama kinaweza kufanyika.

Hivyo mtu ambae naona ni candidate wa u-IGP baada ya Sirro ni Sabas ambae kwa sasa ni Kamishna wa Operesheni.
Hata mimi namkubali sana Kamishna Liberatus M. (Mathias or what nimesahau) Sabas. Amemudu vema sana kila ngazi aliyopitia, na yuko very professional
 
Back
Top Bottom