Nani amemdanganya Mkuu wa Kaya?

Nani amemdanganya Mkuu wa Kaya?

Hao abiria 400+ wanaokwenda Songea ni kina nani? Tumia akili hii nyepesi: Why send a nearly empty Boeing to Songea when a Bombardier could fit the purpose? Tatizo lenu sio ndege, ingekuwa kubwa mngeponda, sasa ni ndogo mnaponda. Mbona hamzungumzii mabehewa mapya ya kuifufua Reli ya Kati? Acheni siasa za chuki
Kwa nyingeza kuna gharama ambazo ni lazima (fixed costs) ndege imepaa au la! Ndege imejaza abiria na mizigo au la!

Ati unanua roli na mtoto wake (tani 40) kubeba tani 5 ambazo zingebebwa na canter! Uchumi gani huo! Mtoa mada akajifunze uchumi kwanza "economies of scale"!
 
.......
.......
.......
.......
Kwahiyo kama kuna abiria 450 wa kwenda Songea, ndege ya Boeing 777 itawabeba wote na itakwenda mara moja tu kwa mafuta ya milioni 6. Lakini Bombadier itabidi iende trip 6 ndipo iweze kuwamaliza. Yani iende kwa mafuta ya milioni 1, irudi kwa mafuta ya milioni 1 (round ya kwanza), iende tena kwa mafuta ya milioni 1 na kurudi kwa mafuta ya milioni moja (round ya pili). Hadi round zote 6 ziishe Bombadier yetu itakua imetumia mafuta ya milioni 12.
Maana yake ni kwamba Bombadier itaenda round 6 na itatumia mafuta ya milioni 12, kubeba abiria walewale ambao wangebebwa na Boeing 777 mara moja tu na kwa gharama ya mafuta ya milioni 6 tu.

Inaonekana hata waliompa taarifa Mkuu wa kaya hawakufanya utafiti wa kutosha kuhusu gharama, aliposikia mafuta ya milioni 1 Dar to Songea akaona ni gharama ndogo kumbe ndege pia inabeba abiria wachache.
Calculation ya gharama za mafuta lazima ziende sambamba na idadi ya abiria. .

ALIYEMDANGANYA MKUU WA KAYA AADHIBIWE....

NAIPENDA TANZANIA NAWACHUKIA WAPIGA DILI.
Mkuu,

1) Ikitokea tuseme kuna demand ya abiria labda 200 tu wa kwenda songea kwa Muda huo uliozungumzia huoni kama hesabu zako zitakinzana??
Manake Bombardier itahitajika kwenda trip mbili labda kwa mafuta ya hiyo 4mil total wakati Boeing mwendo ni uleule wa afuta ya 6mil (kwenda tu)??

2) Kama umeweza kufanya upembuzi ukagundua Si kweli kua Boeing inagharimu Over 26Mil bali only 6mil, mbona hukufanya upebuzi huohuo kwenye mafuta ya Bombardier? Huoni kama inawezekana aliedanganya kwenye mafuta ya Boeing atakua amedanganya pia kwenye mafuta ya Bombardier?? Huoni kama inawezekana hata hiyo 1mil per trip inaweza kua kubwa nayo kama ilivyokuzwa ile ya Boeing??
 
Mkuu,

1) Ikitokea tuseme kuna demand ya abiria labda 200 tu wa kwenda songea kwa Muda huo uliozungumzia huoni kama hesabu zako zitakinzana??
Manake Bombardier itahitajika kwenda trip mbili labda kwa mafuta ya hiyo 4mil total wakati Boeing mwendo ni uleule wa afuta ya 6mil (kwenda tu)??

2) Kama umeweza kufanya upembuzi ukagundua Si kweli kua Boeing inagharimu Over 26Mil bali only 6mil, mbona hukufanya upebuzi huohuo kwenye mafuta ya Bombardier? Huoni kama inawezekana aliedanganya kwenye mafuta ya Boeing atakua amedanganya pia kwenye mafuta ya Bombardier?? Huoni kama inawezekana hata hiyo 1mil per trip inaweza kua kubwa nayo kama ilivyokuzwa ile ya Boeing??
Yes Mkuu, na kwa kuwa hii aliyofanya ni comparative analysis, under ceteris peribus, basi hakutakuwa kutoa conclusion kwa derivative ya comsuption kwa boing against number of trips kwa bombardier, alitakiwa aweke analysis ya consumption ya hayo mapanga boi kwanza ndipo ajenge base ya hitimisho. Kifupi kafanya kazi nusu, kahukumu bila kumpa mshtakiwa wasaa wa kujitetea. Pangu Pakavu.
 
Hao abiria 400+ wanaokwenda Songea ni kina nani? Tumia akili hii nyepesi: Why send a nearly empty Boeing to Songea when a Bombardier could fit the purpose? Tatizo lenu sio ndege, ingekuwa kubwa mngeponda, sasa ni ndogo mnaponda. Mbona hamzungumzii mabehewa mapya ya kuifufua Reli ya Kati? Acheni siasa za chuki
Mimi nadhani uamuzi wa kununua ndege ndogo kwa matumizi ya ndani, ni uamuzi sahihi kwa wakati huu kwa sababu kwa sasa watumiaji wa usafiri wa ndege ni wachache.

Lakini pia siyo kweli kwamba Dash 8 Q400 ndiyo ndege bora kuliko nyingine zote kwa mazingira ya aina zote. Kusema kuwa Q400 inatumia mafuta kidogo kuliko ndege nyingine zote nao ni uwongo pia. Matumizi ya mafuta kwa ndege hupimwa kwa kuangalia wastani wa matumizi ya mafuta kwa abiria mmoja kwa kilometa 100. Na kwenye kipimo hicho mpaka sasa Q400 is not the best.

Hapo unaongelea matumizi ya mafuta. Na matumizi ya mafuta siyo yanayoweza kulihakikishia shirika kupata faida. Faida hutegemea zaidi efficiency ya shirika.

Ni efficiency pekee ndiyo itakayolifanya ATCL isonge mbele au ianguke, wala siyo kiasi cha mafuta ndege zinachotumia au upya wa ndege tulizo nazo.
 
Hivi alichokisema raisi kuwa, bomberdia inatumia mafuta ya ml.1 mpaka songea ni kweli?
 
hii picha ina inazungumza mengi mambo si mambo umejifunza nini hapa.
View attachment 410241
swissme
Mkuu....
Hivi unayo hiyo milioni 7?
Yaani ukisoma hoja ya swali la mleta uzi ni kwamba.. NANI ANAMDANGANYA MKUU WA KAYA?
Alafu wewe ulipo weka picha ya Waziri mkuu na Mkuu wa kaya, maana yake ni kwamba huyo ndie anae mdanganya...
Ebu ngoja niishie hapa kwanza
 
Wewe mdau mleta mada kias flan hauko sawa.kama trip moja ya Bomberdier ni abiria 75, kwenda na kurudi si abiria 150? Na ili upate hao 450 itahitaj trip 3. Au mwenzetu ulichukulia inarud na ruban tu bila abiria wala chochote? Au hiyo 1 million sio return trip?
Hapa nazungumzia abiria 450 waliopo Dar na wanaenda Songea
 
Kwa hiyo wewe unashauri boeing triple 7 itumike kwenye usafiri wa Dar Songea? Makubwa tena makubwa kabisa. Will you please refrain from giving advanced technical advise for something you dont know? Ningeshauri sana wewe na watanzania wengi wanaofungua thread za kijinga kila siku hapa kusemea technical issues za air aviation ambazo hawajui hata abc zake wakae kumya.
Am much better, ndiyo maana nimeweka na link hapo ili udukue zaidi.
 
Awali ya yote nichukue fursa hii kumpongeza Mkuu wa Kaya yetu kwa moyo wake wa kizalendo wa kutuletea ndege mbili mpya ili kufufua shirika letu ambalo wenzie walilitafuna na kulifilisi. Japo haohao ndio wanaomshangilia kama vile waliofilisi shirika hilo siyo wao.

Mkuu wa Kaya umedanganywa kuhusu gharama za usafiri wa ndege Dar to Songea. Amesema kuwa ndege za kawaida zinaweza kutumia mafuta ya milioni 28 kutoka Dar to Songea lakini ndege mpya za Bombadier Q400 zitatumia mafuta ya milioni 1 tu. Mimi sio mtaalamu wa ndege lakini taarifa imenifanya kufanya utafiti kidogo

Katika kajiutafiti kangu nimegundua kiwango cha mafuta ya ndege kwa safari hakipo constant. Kinatofautiana kutokana na sababu anuai, kama vile aina ya ndege, umbali wa safari, uzito wa mzigo wa kwenye cabin, kimo kutoka usawa wa bahari, namna ya kupaa. Vyote hivi huchangia utofauti wa utumiaji wa mafuta ktk ndege.

Katika hayo tuchukue moja la aina ya ndege na hayo mengi yawe constant (under ceteris peribus). Mkuu wa Kaya amesema "ndege nyingine" zitatumia mafuta ya mil.28 kutoka Dar kwenda Songea, lakini Bombadier zetu zitatumia mafuta ya milioni 1 tu. Tuchukulie mfano wa ndege aina ya Boeing 777 yenye uwezo wa kubeba abiria hadi 450 (mara 6 zaidi ya Bombadier zetu).
Umbali wa Dar to Songea kwa barabara ni maili 655 sawa na kilomita 1,054. Lakini kwa anga ni maili 364 sawa na kilomita 585. Boeing 777 inauwezo wa kukimbia kwa speed ya maili 590 kwa saa, sawa na kilomita 949 kwa saa. Kwahiyo ikisafiri kutoka Dar to Songea (kilomita 585) itatumia mwendo wa dakika 36 tu.
www.distancecalculator.net

Mafuta ya ndege hupimwa kwa galoni (US Liquid gallon) ambapo galoni moja ni sawa na lita 3.7 za ujazo. Boeing 777 inatumia galoni 14.4 za mafuta kwa injini moja kwa dakika (1 lg/engine/minute). Boeing 777 ina injini mbili za "Rolls Royce trent 892" zinazotumia galoni 28.8 za mafuta kwa dakika moja (ingia hapa ). Hivyo basi kwa dakika 36 itakazotumia kutoka Dar to Songea itatumia galoni 1,036.
www.askcaptainlim.com

Galoni moja ya mafuta (US liquid gallon) ina lita 3.7 za ujazo. Kwahiyo galoni 1,036 ni sawa na lita 3,836. Bei ya mafuta ya ndege (jet fuel) katika soko la Marekani ni dola 1.38 kwa galoni moja kwa bei ya September 1 mwaka huu. Kwa Tanzania sijui bei ni kiasi gani, lakini tukadirie ni mara mbili ya bei ya Marekani, yani dola 2.76 kwa galoni moja ya lita 3.7.
www.flightdeckfriend.com

Kwahiyo tukitaka kujua gharama za mafuta ya Boeing 777 kutoka Dar kwenda Songea tunachukua galoni 1,036 mara dola 2.76, mara bei ya dola kwa leo ambayo ni TZS 2,182/=. Utapata Shilingi 6,239,123/=. Hii ndio gharama halisi ya mafuta ambayo Boeing 777 itatumia kutoka Dar to Songea.

Maana yake ni kwamba Boeing 777 itatumia mafuta ya milioni 6.2 kupeleka abiria 450 Songea kutokea Dar.

Sasa twende kwenye Bombadier zetu ambazo Mkuu wa Kaya amesema zinatumia mafuta ya milioni 1 tu kwa safari ya Dar - Songea. Bombadier Q400 inatumia mafuta ya milioni 1 kusafirisha abiria 75 tu kutoka Dar to Songea.
Kwahiyo kama kuna abiria 450 wa kwenda Songea, ndege ya Boeing 777 itawabeba wote na itakwenda mara moja tu kwa mafuta ya milioni 6. Lakini Bombadier itabidi iende trip 6 ndipo iweze kuwamaliza. Yani iende kwa mafuta ya milioni 1, irudi kwa mafuta ya milioni 1 (round ya kwanza), iende tena kwa mafuta ya milioni 1 na kurudi kwa mafuta ya milioni moja (round ya pili). Hadi round zote 6 ziishe Bombadier yetu itakua imetumia mafuta ya milioni 12.
Maana yake ni kwamba Bombadier itaenda round 6 na itatumia mafuta ya milioni 12, kubeba abiria walewale ambao wangebebwa na Boeing 777 mara moja tu na kwa gharama ya mafuta ya milioni 6 tu.

Inaonekana hata waliompa taarifa Mkuu wa kaya hawakufanya utafiti wa kutosha kuhusu gharama, aliposikia mafuta ya milioni 1 Dar to Songea akaona ni gharama ndogo kumbe ndege pia inabeba abiria wachache.
Calculation ya gharama za mafuta lazima ziende sambamba na idadi ya abiria. .

ALIYEMDANGANYA MKUU WA KAYA AADHIBIWE....

NAIPENDA TANZANIA NAWACHUKIA WAPIGA DILI.
Kwani jamaa huwa anasikia la kuambiwa au kajidanganya yeye mwenyewe ?
 
we subiri atumbuliwe jicho maaana watamstukia tyuu TRA wa miaka hiii sio wa zama zileeeeeeeeee
 
Sasa mkuu abiria 450 wa kwenda songea siku moja unawatoa wapi?
Huko nyie mabasi tu yanawatosha.
 
Hoja yako inaweza kuwa na substance. Lakini jee tunao abiria 450 wa kupanda Boeing 777 kwenda Songea Kwa wakati mmoja? Nadhani walimshauri Mkuu wa Kaya waliangalia vigezo kadhaa ikiwemo ulichokijengea hoja.
Abiria 75 wa DAR - SONGEA pia itakuwa ni shida kuwapata.
 
Hao abiria 400+ wanaokwenda Songea ni kina nani? Tumia akili hii nyepesi: Why send a nearly empty Boeing to Songea when a Bombardier could fit the purpose? Tatizo lenu sio ndege, ingekuwa kubwa mngeponda, sasa ni ndogo mnaponda. Mbona hamzungumzii mabehewa mapya ya kuifufua Reli ya Kati? Acheni siasa za chuki
Hoja hujibiwa kwa hoja, sio vioja. Njoo na mathrmatical formula ku prove kwamba fastjet inatumia mafuta ya milioni 28 kwenda Mwanza.
 
Mkuu umefanya analysis nzuri lakini hukumalizia ndio maana utapata critism nyingi. ungefanya kitu kimoja ungekata mzizi wa fitna

moja ungeafanya cost analysis kwa abiria mmoja ndege ikiwa imejaa (fully capacity), ikiwa na abiria (50% capacity) na ikiwa na abiria 25% inakuaje. hii itamaliza kabisa fitna yeyote
 
Back
Top Bottom