Tatizo la watanzania tunafanya mambo kwa hisia na mihemko.
Hakuna mahali ambapo Lowasa alisema kuwa atazungumzia ishu ya Richmond Arusha.
Richmond Lowasa alishaizungumzia mara nyingi tangu sikua ile alipojiuzulu.
Na aliizungumzia ndani ya kikao cha chama pale alipoona anakashfiwa na kina Nape na kundi lake kwa gharama za chama.
Lowasa tangu siku ile alipojiuzulu aliweka sawa na watanzania wote wasio na maslahi ya kisiasa na kimadaraka wakamuelewa kuwa alionewa na ndio maana watu wanamuunga mkono na makundi mbalimbali.
Alichosema Lowasa ni kuwa mambo mengine yanayohusu vipao mbele vyake asingependa kumaliza uhondo wa kuyazungumzia pale Dodoma badala yake atayazungumzia Arusha.
Sasa watu bado wanaendelea na hilo suala ili tu kuanzisha malumbano ya kimakundi badala ya mijadala ya kuondoa umaskini.
Hata ukiangalia kwa sasa watanzania hawazungumzii masuala ya kumtaja sijui Mwakyembe ,sijui Sita kama agenda wao wanataka waondokane na umaskini.
Umaskini umewatesa sana watu na wengi wanakoeshwa haki zao kwa sababu ya umaskini na kukosa elimu.
Sasa makundi mengine ya kisiasa yanashindwa kujipanga baala yake wanakuja na hadithi za nani ni hasimu wa nani!
Lowasa angekua ni fisadi na Mwakyembe na Samweli Sita wana vielelezo vyote vya kumtia hatiani wasingeendelea na hadithi za kusema kuwa ni fisadi tu huku wakimwomba mwenyezi Mungu ili Lowasa afe ,badala yake wangempeleka mahakamani ili ahukumiwe.
Ni mwanasheria gani asiyejua kuwa chombo cha kutoa hukumu ni mahakama. Iweje wao kama wanasheria na tena mawaziri waendelee kupita kuwema tutatoa vielelezo vyote.
Je,inakuaje wapenda haki wanaficha vielelezo vya wahalifu?
Je,kama ni kweli kama Mwakyembe na Sita watakuwa na vielelezo vya wizi unaofanywa na baadhi ya watumishi wa umma halafu wakaamua kuvificha kwa ajili ya kuvitumia kwa manuafaa yao ya kisiasa kwa nini tuendelee kuwaamini hawa watu wanafiki na wabinafsi?
Kuungwa mkono kwa namna yoyote sio jambo jepesi kama watu wanavyotuambia .
Miaka kumi Sita na Mwakyembe wanatumia gharama za serikali na nafasi za uwaziri kujisifia na kuona kila mtu hafai na wao ndio bora lakini bado imekuwa ni vigumu kuingia kwenye mchuano na Lowasa.Pamoja na kuwa Lowasa amewekwa benchi kwa miaka 8 huku kila njama zikitumika kumchafua na kumchonganisha na rais na chama chake lakini bado anaushawishi kwa watanzania kuliko hata hao mawaziri walioko madarakani huku wakishindwa kuwatumikia watanzania kwa vitendo.