Ngongo
JF-Expert Member
- Sep 20, 2008
- 18,933
- 31,178
HATUA ya Rais Jakaya Kikwete kukiri kuwa kulikuwapo na udhaifu katika kufanya uchunguzi wa kutosha (due diligence) kuhusu kampuni tata ya kufua umeme ya Richmond, aliyoitoa wakati wa kujibu maswali ya wananchi, imeanza kutafsiriwa na wabunge kama mwongozo wa ripoti ya Serikali itakayowasilishwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda bungeni kuhusu utekelezaji wa maazimio 23 ya Bunge kuhusu kampuni hiyo.
Katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete alikiri kutofanyika kwa kile alichokitaja kuwa ni due deligence udhaifu ambao uliibuliwa pia na Kamati Teule ya Bunge, iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harisson Mwakyembe. Hali hiyo inaunganisha mtazamo unaofanana kati ya Bunge na Rais Kikwete.
Katika azimio namba saba kati ya hayo 23, kamati teule ya Bunge ilipendekeza kuwa: Wajumbe wote wa kamati ya Serikali ya majadiliano (Government Negotiation Team-GNT) ambao ni maafisa waandamizi wa Serikali wawajibishwe kwa manufaa ya umma kwa kulitia hasara taifa kutokana na kushindwa kutumia elimu na ujuzi wao kulinda maslahi ya taifa.
Baada ya mapendekezo hayo, Agosti 28, mwaka 2008, Waziri Mkuu pia alitoa taarifa bungeni kuelezea hatua zilizochukuliwa katika utekelezaji wa maazimio hayo na hususan azimio hilo namba saba, ambalo linawahusu vigogo wa Serikali ambao ni pamoja na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika.
Wengine ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Arthur Mwakapugi na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja. Kamati hiyo ilikuwa na jukumu la kutoa ushauri mzuri kwa Serikali kwa ujumla.
Katika taarifa yake, Waziri Mkuu alieleza hatua zilizochukuliwa kuwa ni pamoja na kuwataka wahusika hao pamoja na kuandikiwa ili kutoa maelezo ya utetezi au ufananuzi katika kile kilichotajwa kuwa ni kuwapa haki ya asili ya kusikilizwa.
Mbali na timu hiyo ya GNT ambayo katika sakata hilo ilipewa jukumu la kushauri serikali, pia ipo timu nyingine ya wataalamu iliyokuwa imepewa jukumu la kutathmini wazabuni wote katika orodha ya wazabuni waliokuwa wakiwania zabuni ya kuzalisha umeme kwa wakati huo.
Waziri Mkuu alieleza kuwa miongoni mwa maeneo ambayo watumishi hawa wametakiwa kutoa maelezo ni jinsi walivyohusika katika mchakato mzima na kuingiza Serikali katika mkataba unaonekana kutokuwa na maslahi kwa Taifa ni pamoja na kutotumia utaalamu na uzoefu wao kikamilifu ili kutambua mapema kuwa Richmond Development Company LLC haikuwa na uwezo kitaalamu, kifedha na kuzoefu na hivyo kutokidhi matakwa ya zabuni.
Maeneo mengine kwa mujibu wa Waziri Mkuu kwa wakati huo ambayo wahusika katika kamati hizo mbili walitakiwa kujieleza ni kutozingatia kikamilifu Sheria ya Manunuzi ya Umma, ya mwaka 2004 katika mchakato mzima wa kutoa zabuni, wajumbe kushindwa kuishauri Serikali kuhusu kuifanyia Kampuni ya Richmond Development LLC uchunguzi wa awali (Due Diligence) pamoja na ukaguzi baada ya tathmini ya zabuni (post qualification).
Katika kipengele hicho cha due deligence ndipo panapotajwa kuwamo katika ripoti itakayowasilishwa na Waziri Mkuu na kwamba kwa kuwa tayari Rais alikiri kuwa jambo hilo halikufanyika ipasavyo, matarajio ya wabunge wengi ni kuwa ripoti hiyo itakayowasilishwa kwenye mkutano huu wa 17 wa Bunge itabainisha hatua zilizochukuliwa dhidi ya wahusika.
Tayari Rais Kikwete aliungana na maoni ya Kamati Teule ya Bunge hasa kuhusu kutofanyika kwa uchunguzi wa kina kuhusu Richmond , alikiri kuwapo kwa tatizo hilo hadharani alipozungumza na wananchi kwa hityo utaona wahusika wakuu kwenye suala hili wanamakosa ya wazi ambayo yametambuliwa tayari na Rais,
Kwa hiyo tunatarajia kusikia tu hatua zinatazochukuliwa kwa kuzingatia kukiri huko kwa Rais. Na ukweli ni kwamba unapokuwa na timu za watumishi wanaoaminika ni watalaamu na kisha kazi haifanyiki vizuri na Rais anakiri ni wazi hatua kali zinapaswa kuchukuliwa kama ambayo kamati teule ya Bunge ilivyopendekeza, alidokeza mbunge mmoja.
Katika taarifa yake hiyo ya Agosti 28, mwaka jana, Waziri Mkuu pia aliweka bayana kuwa wahusika walipewa nafasi ya kujieleza na wakafanya hivyo na katika mkutano wa 16 wa Bunge, Waziri Ngeleja alitoa taarifa iliyokataliwa akisema wahusika walipewa barua za onyo.
Lakini kutokana na mazungumzo ya Rais wakati akijibu maswali ya wananchi, alihidi kuwa taarifa ya sasa bungeni kuhusu Richmond itakuwa nzuri hali ambayo itafsiriwa kuwa wahusika ambao hawakufanya utafiti wa kutosha kuhusu Richmond watachukuliwa hatua za ziada.
Pamoja na kusubiriwa kwa hamu kwa taarifa ya serikali kuhusiana na Richmond, ndani ya Bunge kumekuwapo na mgawanyiko wa dhahiri kuhusiana na sakata hilo ikielezwa kuwapo mkakati mahususi wa kusafisha wanasiasa na watendaji wa serikali waliochafuka kutoka na kashfa ya kampuni hiyo.
Mgawanyiko huo umeelezwa kuwa chanzo cha msuguano uliopo sasa kati ya Bunge na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambako Mkurugenzi wake, Dk. Edward Hosea, ameonekana kuwa na jeuri ya kulumbana waziwazi na wabunge baada ya kutaka kuwahoji kuhusiana na suala la posho.
Dk. Hosea pekee ndiye aliyebaki katika watendaji wa serikali waliotajwa katika kashfa ya Richmond na kwamba kupona kwake kulitokana nay eye kutokuwamo katika timu ya majadiliano ya serikali iliyoundwa na Waziri Mkuu aliyejiuzulu kutokana na kashfa hiyo, Edward Lowassa. Hosea yeye alituhumiwa kupindisha taarifa ya wataalamu wake, tuhuma ambazo alisafishwa nazo Agosti mwaka huu na Bunge kuridhia.
Makundi ndani ya Bunge yanaashiria hata kukiyumbisha Chama cha Mapinduzi (CCM) chenye wabunge wengi na kukilazimu chama hicho tawala kuunda Kamati ya Maalumu inayoongozwa na Rais Mstaafu, Ally Hassan Mwinyi akisaidiwa na wana CCM mashuhuri, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Pius Msekwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho Abdulrahman Kinana.
Source: Raia mwema
Makongoro Mahanga na Bi Sofia Simba tayari wameshaonyesha misimamo yao.Nilidhani huo ni msimamo wa serekali,
Katika mazungumzo hayo, Rais Kikwete alikiri kutofanyika kwa kile alichokitaja kuwa ni due deligence udhaifu ambao uliibuliwa pia na Kamati Teule ya Bunge, iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harisson Mwakyembe. Hali hiyo inaunganisha mtazamo unaofanana kati ya Bunge na Rais Kikwete.
Katika azimio namba saba kati ya hayo 23, kamati teule ya Bunge ilipendekeza kuwa: Wajumbe wote wa kamati ya Serikali ya majadiliano (Government Negotiation Team-GNT) ambao ni maafisa waandamizi wa Serikali wawajibishwe kwa manufaa ya umma kwa kulitia hasara taifa kutokana na kushindwa kutumia elimu na ujuzi wao kulinda maslahi ya taifa.
Baada ya mapendekezo hayo, Agosti 28, mwaka 2008, Waziri Mkuu pia alitoa taarifa bungeni kuelezea hatua zilizochukuliwa katika utekelezaji wa maazimio hayo na hususan azimio hilo namba saba, ambalo linawahusu vigogo wa Serikali ambao ni pamoja na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika.
Wengine ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Arthur Mwakapugi na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja. Kamati hiyo ilikuwa na jukumu la kutoa ushauri mzuri kwa Serikali kwa ujumla.
Katika taarifa yake, Waziri Mkuu alieleza hatua zilizochukuliwa kuwa ni pamoja na kuwataka wahusika hao pamoja na kuandikiwa ili kutoa maelezo ya utetezi au ufananuzi katika kile kilichotajwa kuwa ni kuwapa haki ya asili ya kusikilizwa.
Mbali na timu hiyo ya GNT ambayo katika sakata hilo ilipewa jukumu la kushauri serikali, pia ipo timu nyingine ya wataalamu iliyokuwa imepewa jukumu la kutathmini wazabuni wote katika orodha ya wazabuni waliokuwa wakiwania zabuni ya kuzalisha umeme kwa wakati huo.
Waziri Mkuu alieleza kuwa miongoni mwa maeneo ambayo watumishi hawa wametakiwa kutoa maelezo ni jinsi walivyohusika katika mchakato mzima na kuingiza Serikali katika mkataba unaonekana kutokuwa na maslahi kwa Taifa ni pamoja na kutotumia utaalamu na uzoefu wao kikamilifu ili kutambua mapema kuwa Richmond Development Company LLC haikuwa na uwezo kitaalamu, kifedha na kuzoefu na hivyo kutokidhi matakwa ya zabuni.
Maeneo mengine kwa mujibu wa Waziri Mkuu kwa wakati huo ambayo wahusika katika kamati hizo mbili walitakiwa kujieleza ni kutozingatia kikamilifu Sheria ya Manunuzi ya Umma, ya mwaka 2004 katika mchakato mzima wa kutoa zabuni, wajumbe kushindwa kuishauri Serikali kuhusu kuifanyia Kampuni ya Richmond Development LLC uchunguzi wa awali (Due Diligence) pamoja na ukaguzi baada ya tathmini ya zabuni (post qualification).
Katika kipengele hicho cha due deligence ndipo panapotajwa kuwamo katika ripoti itakayowasilishwa na Waziri Mkuu na kwamba kwa kuwa tayari Rais alikiri kuwa jambo hilo halikufanyika ipasavyo, matarajio ya wabunge wengi ni kuwa ripoti hiyo itakayowasilishwa kwenye mkutano huu wa 17 wa Bunge itabainisha hatua zilizochukuliwa dhidi ya wahusika.
Tayari Rais Kikwete aliungana na maoni ya Kamati Teule ya Bunge hasa kuhusu kutofanyika kwa uchunguzi wa kina kuhusu Richmond , alikiri kuwapo kwa tatizo hilo hadharani alipozungumza na wananchi kwa hityo utaona wahusika wakuu kwenye suala hili wanamakosa ya wazi ambayo yametambuliwa tayari na Rais,
Kwa hiyo tunatarajia kusikia tu hatua zinatazochukuliwa kwa kuzingatia kukiri huko kwa Rais. Na ukweli ni kwamba unapokuwa na timu za watumishi wanaoaminika ni watalaamu na kisha kazi haifanyiki vizuri na Rais anakiri ni wazi hatua kali zinapaswa kuchukuliwa kama ambayo kamati teule ya Bunge ilivyopendekeza, alidokeza mbunge mmoja.
Katika taarifa yake hiyo ya Agosti 28, mwaka jana, Waziri Mkuu pia aliweka bayana kuwa wahusika walipewa nafasi ya kujieleza na wakafanya hivyo na katika mkutano wa 16 wa Bunge, Waziri Ngeleja alitoa taarifa iliyokataliwa akisema wahusika walipewa barua za onyo.
Lakini kutokana na mazungumzo ya Rais wakati akijibu maswali ya wananchi, alihidi kuwa taarifa ya sasa bungeni kuhusu Richmond itakuwa nzuri hali ambayo itafsiriwa kuwa wahusika ambao hawakufanya utafiti wa kutosha kuhusu Richmond watachukuliwa hatua za ziada.
Pamoja na kusubiriwa kwa hamu kwa taarifa ya serikali kuhusiana na Richmond, ndani ya Bunge kumekuwapo na mgawanyiko wa dhahiri kuhusiana na sakata hilo ikielezwa kuwapo mkakati mahususi wa kusafisha wanasiasa na watendaji wa serikali waliochafuka kutoka na kashfa ya kampuni hiyo.
Mgawanyiko huo umeelezwa kuwa chanzo cha msuguano uliopo sasa kati ya Bunge na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ambako Mkurugenzi wake, Dk. Edward Hosea, ameonekana kuwa na jeuri ya kulumbana waziwazi na wabunge baada ya kutaka kuwahoji kuhusiana na suala la posho.
Dk. Hosea pekee ndiye aliyebaki katika watendaji wa serikali waliotajwa katika kashfa ya Richmond na kwamba kupona kwake kulitokana nay eye kutokuwamo katika timu ya majadiliano ya serikali iliyoundwa na Waziri Mkuu aliyejiuzulu kutokana na kashfa hiyo, Edward Lowassa. Hosea yeye alituhumiwa kupindisha taarifa ya wataalamu wake, tuhuma ambazo alisafishwa nazo Agosti mwaka huu na Bunge kuridhia.
Makundi ndani ya Bunge yanaashiria hata kukiyumbisha Chama cha Mapinduzi (CCM) chenye wabunge wengi na kukilazimu chama hicho tawala kuunda Kamati ya Maalumu inayoongozwa na Rais Mstaafu, Ally Hassan Mwinyi akisaidiwa na wana CCM mashuhuri, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Pius Msekwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya chama hicho Abdulrahman Kinana.
Source: Raia mwema
Makongoro Mahanga na Bi Sofia Simba tayari wameshaonyesha misimamo yao.Nilidhani huo ni msimamo wa serekali,