Wakuu jana kunagazeti moja la kila siku liliripoti kuwa chadema yamsusa obama lakini baadaye humu jf nikasoma maelezo ya dk slaa akieleza kuwa wao kama chadema hawakushirikishwa kuhusika kwenye huu ugeni kwa maana hiyo hawawezi kujipeleka kwenye ugeni ambao hawakushirikishwa.
Lakini baadaye nikasoma post tena humu jf inabainisha kuwepo kwa mh.mbowe kwenye dhifa ya ikulu ambayo iliandaliwa na rais jk akimwandalia mgeni wake rais obama.
Hali hii ilifanya nijiulize ukweli wa hili gazeti uko wapi na ukweli wa slaa ni upi,awali nikajua ni ule mtindo wa magazeti yetu kuandika taarifa bila kutafiti yawezana slaa yuko sahihi kwa sababu ndiye katibu mkuu wa chama na barua zote hupita kwake kama katibu mkuu,lakini kilichonichanganya tena kusikia mbowe alikuwepo nikashindwa kujua nani aliudanganya uma ni gazeti au slaa au mbowe alialikwa kutokana na mahusiano yao mazuri na jk au mwaliko ulikuwepo lakini slaa akaamua kuongea alivyoongea na gazeti lile taarifa ile lilitoa wapi.
NANI MUONGO AU NINI UDHATI WA HALI HII