sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
Hapo majuzi, timu kubwa ufaransa ya PSG ilienda kucheza mechi huku wachezaji maarufu wa dini kuu mbili wakiwa wamevaa jezi za kuhamasisha na kuutetea ushoga na usagaji lakini kuna mchezaji moja Idrissa Gueye alikataa kuvaa hizo jezi akilalamika ni kinyume na anachoamini
Hili suala si la kidini tu, ni suala la utu.
Mabeberu haya yanajinadi ni nchi zenye uhuru ila kiukweli sijaona chochote kinachoruhusu mtu awe huru kwa anachoona kwake ni sahihi kukisimamia, mabeberu wanajipa uhuru kwenye mambo wanayoyaona ni sahihi kwao lakini wanawazuia wengine kuwa huru kwa wanachoona ni sawa na hakimdhuru yeyote wanapo kisimamia.
Mtu analipwa kucheza mpira ila wanaanza kumlazimisha awe balozi na mhamasishaji wa vitu ambayo vipo kinyume mno na dini yake na hata tamaduni zake.
Kama kuna mashoga na wasagaji, sawa tu waendelee na itikadi zao wao kimpango wao, lakini haya mambo ya kuanza kumlazimisha mtu kutetea mashoga si uungwana hata kidogo.