Namuunga mkono Kigwangalla dhidi ya MO Dewji

Namuunga mkono Kigwangalla dhidi ya MO Dewji

118827217_397407764578762_8736407526797776520_n.jpg
 
MO akitaka kubaki salama, aunde club yake na aendelee kuwa shabiki wa Simba.
Timu ya Simba ina mashabiki wengi wenye madaraka Serikalini.
Haingii akilini MO akiingia uwanjani akashangiliwa kuliko Rais ambaye naye ni shabiki wa Simba.
Mtawala huwa hapendi mwanainchi wa kawaida kuwa maarufu kuliko yeye.
MO akianza kupingana na Kigwangala mwisho wa Siku ataanza kupingana na Majaliwa na kumalizia na MH. Magufuli.
Rais Mstaafu Kikwete alisema, hatutaki club inayomilikiwa na mtu moja.
Michezo ni burudani na tunataka kushangilia kilicho chetu na si cha mtu.
Msahafu unasema .
"Ole wake mtu yule amuaminiane mwanadamu kama kinga yake, mbinguni amelaaniwa"
Club ya Simba sasa inamuamini MO kama kinga yao, mbinguni wamelaaniwa.
Je kesho Mo kama hayupo Duniani club ya Simba itakuwa na hali gani?
Let us think beyond one year.
 
Umeandika bila skrini shoti utadhani kila mwana Jf yupo twita.
 
Ile issue ya.mo na Kigwangala haijaanza leo ilianza toka kipindi kile mo anatishia kujitoa simba aliposema anatumia pesa nyingi kuhudumia simba akamwuliza hizo pesa ni sehemu ya bilioni 20 au zake za mfukoni .
Kigwangala amehoji mambo ya msingi ila kwa ujinga walionao watu wengi wamemjadili zaidi yeye binafsi ikiwa pamoja na mo kukwepa mjadala na kuingiza personal issue.
Mo anapaswa kutoa majibu kwa wanasimba na sio kwenda kutoa majibu kwa wasafi fm ambao tunajua watangazaji wake wengi ni yanga wa kutupwa.
Kuna madudu mengi kuhusiana na uwekezaji wanmo ila madudu hayo hayaonekani kwa sababu ya mafanikio tunayoyapata uwanjani.
Ajatoa bilioni 20 kwa sababu mchakato haujakamilika lakini ameshakuwa na madaraka makubwa kabla mchakato haujakamilika.
Kuna bidhaa zake ambazo hazipo kwenye mkataba na simba lakini amekuwa akizitangaza kupitia simba mfano mo protector sasa ukiacha zile pikipiki zake sasa kama anamleta CEO ambaye ni msaidizi wake binafsi ataweza vp kutenganisha maslahi ya simba na ya kampuni anazoongoza mo.
Kuna kanga zilikuwa zinauzwa simba day hazijulikani nani ametengeneza na pesa zinaenda kwa nani ukichukulia na yeye anamiliki viwanda vya nguo.
Mpaka sasa simba haijaweza kujitegemea leo mo akitoka simba itasimama vipi pamoja na mishahara mikubwa ya wachezaji.
MO hatufai mfukuzeni mlete muwekezaji mwingine.
 
Yanga ikifungwa leo utasema ni sababu ya kampeni za siasa! Mkuu achana na siasa maana inaonekana imekuathiri sana. Kila kitu unahusisha na siasa...yaani hata chai hujanywa maana naamini uko Tz, ila umeamkia na ishu ya mo na kigwa na kuileta moja kwa moja kwenye siasa.
umekua mtumwa!
 
Habari za asubuhi wakuu....ujue hawa waheshimiwa wanataka kutuona sisi kama watoto ila kwa kile nilichokiona nje ya mchezo ni sio hisa za mo kwa simba wala uwekezaji wake pale msimbazi bali tukae na kutambua kwamba hawa wote ni wana ccm na wanachokijalibu kukifanya hapa ni kututoa kwenye mawazo ya kampen maana wameshaona mgombea wao kila anakoenda anapigwa k.o kwahiyo wameona watuamishie upande wa pili ili kila mtu akili yake ikae upande huu na sio kwenye kampen tena ili waweke mambo yao sawa.

Hivyo tutumie akili kuwaza hii inaweza ikawa ni technical plan ya mataga baada ya kuona mkubwa havutii
Hisa za MO na CCM wapi na wapi bwashee!!!
 
Yanga ikifungwa leo utasema ni sababu ya kampeni za siasa! Mkuu achana na siasa maana inaonekana imekuathiri sana. Kila kitu unahusisha na siasa...yaani hata chai hujanywa maana naamini uko Tz, ila umeamkia na ishu ya mo na kigwa na kuileta moja kwa moja kwenye siasa.
umekua mtumwa!
Watanzania tufanye kazi kwa bidii.. huu ni Kama ugonjwa unatunyemelea.. mtu akijikwaa CCM hiyoo.. Mtu akipita na baiskeli anatoka shamba kajichokea.. CCM hiyo.. Mtu akifanikiwa akanunua kagari kake akipita utasiki tu MaCCM hayo..

Ni Kama ukiwa Tanzania Hakuna kitu utafanya ukawa salama..

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Habari za asubuhi wakuu....ujue hawa waheshimiwa wanataka kutuona sisi kama watoto ila kwa kile nilichokiona nje ya mchezo ni sio hisa za mo kwa simba wala uwekezaji wake pale msimbazi bali tukae na kutambua kwamba hawa wote ni wana ccm na wanachokijalibu kukifanya hapa ni kututoa kwenye mawazo ya kampen maana wameshaona mgombea wao kila anakoenda anapigwa k.o kwahiyo wameona watuamishie upande wa pili ili kila mtu akili yake ikae upande huu na sio kwenye kampen tena ili waweke mambo yao sawa.

Hivyo tutumie akili kuwaza hii inaweza ikawa ni technical plan ya mataga baada ya kuona mkubwa havutii
Sio kila kitu ukichukulie kisiasa mkuu, kuna maisha nje ya siasa lazima utambue ukweli huo.

Lissu kumshinda Magufuli mwenye kuimiliki dola yote ni ndoto za mchana wa jua kali.
 
Mbona mizozo ya hizi Club za Simba na Yanga huwa zipo tu hata kabla ya kampeni.
Kigwa anafikra za kumpaka matope Mo kwa sababu ya chuki zake binafsi kwa Mo kwenye mambo yao binafsi(personal issues)
Unachotakiwa kujua ni kwamba CCM itashinda mapema sana uchaguzi huu kushinda chaguzi zilizopita.
 
Huyu Mwamedi bado hajaweka B20 mezani lakini kashaanza kuitumia club yetu anavyotaka yeye. Mimi binafsi ile siku alivyogeuza shughuli ya simba kuwa jukwaa la siasa aliniudhi sana.
Ujue siasa ni stress, watu tumekimbia stress tumekuja kwenye mpira kufurahi, then wewe unatuletea stress za siasa tena.

Hili la CEO ndio limeniacha hoi maana member mwenzetu Shark alishatuletea nyepesi kuhusu huyo CEO tangu mwezi uliopita.
 
Back
Top Bottom