Namuonya Mwigulu Nchemba - Kitila Mkumbo

Namuonya Mwigulu Nchemba - Kitila Mkumbo

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema aliyetimuliwa hivi karibuni Dr Kitila Mkumbo amemuonya vikali Naibu Katibu Mkuu CCM Mwigulu Nchemba kwamba akae mbali na yeye.

Dr Kitila amedai kushangazwa na machozi ya mamba ya Mwigulu ambaye kwa unafiki mkubwa eti amemsikitikia kwa yaliyomfika.

Dr Kitila amesema siku zote Mwigulu Nchemba amekuwa akimchafua lakini tangu atimuliwe uongozi Chadema Mwigulu amejifanya kumsifu sana na kumhurumia.

Dr Kitila amemuonya Mwigulu kwamba inyeshe mvua au liwake jua ni lazima atamvaa katika uchaguzi wa Ubunge jimbo la Iramba Magharibi ama kupitia Chadema au kwa njia nyingine yoyote.

Dr Kitila amemtaka Mwigulu kutambua kwamba yeye bado ni mwanachama wa Chadema.
 
mwigulu hadi aibu. nzeshi type. maneno hayo yalipaswa yazungumzwe na zitto kwani ndio anatetewa sana na maccm lakini kaogopa kutoa kauli hiyo.
 
Dr fwata Mkumbo yeye na Mwiguru wote weu tu hapa anajifanya anamkana ila wakikutana wanapanga mambo yao pamoja
 
Post gan hii sasa, yan katika speech yake ulichoona ni hiki tu?
 
Hadi raha.....tofauti na mawazo ya Lumumba kwamba sasa CDM kwisnei, CHADEMA ipo mioyoni mwa wengi kama sio Watanzania wote basi shetani (CCM) naye ana nguvu zake.........ila mwisho wake unakaribia maana naona kama akiba ya damu zetu kwenye mishipa yake imeanza kuisha na sisi wanyonywaji tumeshtuka kuwa damu aliyokuwa atunyonya alikuwa haipeleki kunakostahili bali alikuwa anajiopngezea mwenyewe.
 
Wote ni ndugu zangu kitila na mchemba lkn kwa sasa ni mwigulu tuu kuhusu iramba, kitila pamoja na Elimu yako hujawaonyesha wana iramba utawafanyia nn na chadema yako.
 
Post gan hii sasa, yan katika speech yake ulichoona ni hiki tu?

Bado nakufuatilia kwa karibu kiongozi wangu, vipi? nini kimekusibu? mbona posti zako zimebadilika sana tokea ule mkutano wa asubuhi, post zako zimekuwa za kinyonge kama mtu aliyekosa matumaini! Bado una nafasi kiongozi, fuata njia aliyoichukua Kiongozi wako kitila mkumbo, na wewe una chansi ya kuomba msamaha, nina uhakika utasamehewa tu, jirudi kiongozi, bado tunakupenda, rudisha moyo.
 
Kama ni kweli, Dr. Kitila kanikuna ubongo. Sasa nimeamini kuwa hayo Maccm yameshaanzi kuchanganyikiwa. Laiti yangeacha siasa zao za maji taka. Yanafikiri ni rahisi kukisambaratisha CDM kwa kuwarubuni watu. CDM ni litaasisi sio kikundi, CDM ni mbuyu mukubuwa, hautishwi na vuli.
Kitila, kujikwaa si kuanguka, inuka Kamanda. Omba msamaha na 2015 tutakutuma kumnyoa huyo "Bata mzinga" yale manyoya.
Singida ni CDM yoote
 
JAPO DHAMBI ZENU NI NYEKUNDU KAMA DAMU ZITASAMEHEWA NA KUWA NYEUPE KAMA THELUJI ENDAPO MTAJIRUDI NA KUONA JE NI WAPI TULIKOSEA,japo kuna dhambi ambazo ni ngumu kuzisamee hasa dhambi ya usaliti kama ya "YUDA"alimsaliti yesu kwa vipande thelathini vya fedha kwa mujibu wa andiko.je endapo "YESU" angefanikiwa kuwatoroka watesi wake,akaja kuonekana tena israel,je "YUDA" angesheshindwa kumsaliti tena kwa mara ya pili?
 
Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema aliyetimuliwa hivi karibuni Dr Kitila Mkumbo amemuonya vikali Naibu Katibu Mkuu CCM Mwigulu Nchemba kwamba akae mbali na yeye.

Dr Kitila amedai kushangazwa na machozi ya mamba ya Mwigulu ambaye kwa unafiki mkubwa eti amemsikitikia kwa yaliyomfika.

Dr Kitila amesema siku zote Mwigulu Nchemba amekuwa akimchafua lakini tangu atimuliwe uongozi Chadema Mwigulu amejifanya kumsifu sana na kumhurumia.

Dr Kitila amemuonya Mwigulu kwamba inyeshe mvua au liwake jua ni lazima atamvaa katika uchaguzi wa Ubunge jimbo la Iramba Magharibi ama kupitia Chadema au kwa njia nyingine yoyote.

Dr Kitila amemtaka Mwigulu kutambua kwamba yeye bado ni mwanachama wa Chadema.

Safi sana!
Hiyo ndiyo misimamo mapambano kwa kwenda mbele na nimatarajio yangu kuwa ni kwa kupitia CDM!
Dr.Kitila naomba usisahau kuwa Kazi ya miaka yote ya kuimarisha CDM mpaka ilikofika utakuwa uamuzi usiowabusara kama Jabza itaongoza katika kutafuta suluhu ya Mgogororo uliopo.
 
Back
Top Bottom