Habari za jioni wapendwa wana jamii foramu
Naamini mu wazima
Mimi si mgeni jamii forum ni mfuatiliaji wa mada mbali mbali japo naingiaga Kama guest user, baada ya kusoma visa na mikasa mingi leo rasmi nimeamua kutengeneza akaunti kwa lengo moja tu la kutafuta mwenzi wa maisha kama second chance.
Kwa wale mlioowa na kuolewa na bado mkadumu katika ndoa Mungu awabariki na awazidishie upendo milele.
Niliolewa kabisaa lakini kuna mambo mazito hasa yalinikumba ndoa ikavunjika baada ya uwezekano wa kurekebishika ulipogonga mwamba.
Kwa muda wote niliokaa peke yangu nimetafakari kwa kina sana na kuamua kutafuta mwanaume ambaye anaweza kunipenda iili baadaye awe mume.
Sifa zangu
-Ni mdada naejituma, mcha Mungu na naejiheshimu
-Ni msomi na najiweza kiuchumi
-Umri wangu upo chini ya miaka 30
-Umri wa utoto na kurukaruka ulishapita, najielewa na najua nachokitaka.
-Nina mtoto mmoja
Sifa za mwanaume
-Awe Mkristo asiyetumia pombe
-Awe asiyependa anasa (sipo tayari kusex naye hadi hapo tutakapo weka kiapo)
-Mwenye uthubutu katika mambo ya maendeleo ( asiye amini sana masuala ya kuajiriwa zaidi sana awe na malengo ya kujiajiri mana matajiri wengi ni wale waliojiajiri)
-Mchapakazi mchapakazi mchapakazi
-Awe amekomaa kiakili, asiwe toz mvaa milegezo na ambaye bado anataka kurukaruka na vibinti
-mwenye upendo sana, kuheshimu na kujali utu.
Huyu namkaribisha tuwe marafiki wenye malengo
Sent using
Jamii Forums mobile app