Namshukuru Mungu nimepona

Namshukuru Mungu nimepona

Nitapenda kuona ukithibitisha.

Muujiza ni nini na utajuaje huu ni muujiza na si kitu nisichokijua tu?

Wazungu walivyokuja na gramophone kucheza muziki, waafrika ambao hatukujua sayansi ya kunasa sauti tulivyoona kibox kinaimba muziki ni kama muujiza.

Tukawaona wazungu kamamiungu fulanihivi, ndiyomaana mzungu na mungu zinapishana z tu.

Hawa waafrika waliona muujiza kwa sababu hawakuelewa ile gramophone inavyofanya kazi.

Leo vitukuu vyao tumeelewa hatuoni tena muujiza.

Utakapoona kitu unachofikiri muujiza, utajuaje huu muujiza kweli na si ujinga wako tu kutokujua mambo kama wale waafrika walioona gramophone kutoa sauti ya mtu ni muujiza?

supernatural power ndio inaaminika kuwa ina control kila kilichopo ambacho kipo beyond ya uwezo wa kibinadamu.

Sasa hapo kwenye hiyo supernatural power kuna mtu yeyote umewahi kuskia akikwambia chanzo chake ni hiki!? Na kama hayupo unahisi chanzo ni nini!?

Kusema kwamba kitu usichokijua sio miujiza bali ni ujinga tu wa kutokujua na kuhisi kwamba kuna siku kitu hicho kitafahamika tu chimbuko lake ni nini huo sasa ni ubishi tu na kujaribu kupingana na nature.

Huwezi ukasema ni kwanini hatuwezi kuzuia vifo hata iweje ni lazima tufe basi ni kwa sababu tu sisi binadamu wa kizazi cha Leo bado ni wajinga ila naamini kuna siku itapatikana soln ya kuzuia kifo.

Miujiza ipo sana tu mkuu. Umewahi kuona mtu ameoteshwa mpera kichwani?
 
Ukiwa tayari na negative thought juu ya chochote kinacho muhusu Mungu basi ni rahisi kuleta argument kama hii, kwamba eti kwa sababu mgonjwa X pamoja na kumuomba Mungu hajapona lakini mgonjwa Y amepona basi huyo Mungu unamuona kama ana upendeleo na hatimae kuhitimisha kuwa hayupo.

Hapo inaonesha unahitaji kupata darasa linalohusu Maombi ndio utafahamu kwani kuna maombi hayajibiwi na mengine yanajibiwa. Sio kila huwa inasiklizwa ndugu.

Hata kitendo cha binadamu kufariki bado ni uthibitisho tosha wa uwepo wa Mungu.. "ni kwanini lazima ufariki"?
Kwhyo kumbe kuomba mungu bado ni probability either akujibu au asikujibu
Ni sawa sawa na mtu muovu akipata mabalaa mnasema amelaaniwa
Na mtu mwema akipata mabalaa hayo hayo mnaita ni majaribu

Hayo maombi ambayo hayakubaliwi yanakuwa yamekosa nini?
Kifo hakikithibitishi kwamba mungu yupo
 
Thibitisha kwamba Mungu yupo.

Binadamu kufariki si uthibitishokwamba Mungu yupo.

Ni uthibitisho kwamba Mungu hayupo.

Mungu mwenye uwezo wote,ujuzi wote na upendo wote angekuwepo, kifo kisingekuwepo.

Kifo kinam contradict huyo Mungu.

Ukiambiwa hata wewe mwenyewe hapo ndani ya nafsi yako kuna uungu ambao ndio unakusukuma kuwaza na kuandika haya yote hapa utakataa!?

Lakini nafsi hiyo hiyo ukiiruhusu ikaingiliwa na ibilisi kwa kumkataa Mungu ndio inakufanya uwe hivi ilivyo sasa. Baada ya kumkataa Mungu umempa nafasi ibilisi akutumie kufanya evil manipulation.

Umewahi kushuudia ajari mbaya abiria wote wakafa halafu akapona mtoto peke yake!?

Kifo ni adhabu tuliyopewa Mungu, hakuna binadamu anaependa kufa sasa mpaka Leo hii hakuna mwenye uwezo wa kuzuia kifo hiyo tu clarity tosha kuwa kifo ni uthibitisho.
 
Kwhyo kumbe kuomba mungu bado ni probability either akujibu au asikujibu
Ni sawa sawa na mtu muovu akipata mabalaa mnasema amelaaniwa
Na mtu mwema akipata mabalaa hayo hayo mnaita ni majaribu

Hayo maombi ambayo hayakubaliwi yanakuwa yamekosa nini?
Kifo hakikithibitishi kwamba mungu yupo

Sio probability, suala la maombi ni pana sana.

Kuna sala ambazo hazikubaliwi na ambazo zinakubaliwa, na hii inatokana na ukaribu wa kiimani wa muombaji na anae muomba.

Hata utakaso wa muombaji una play part kubwa kwenye kukubaliwa.
 
Ukiambiwa hata wewe mwenyewe hapo ndani ya nafsi yako kuna uungu ambao ndio unakusukuma kuwaza na kuandika haya yote hapa utakataa!?

Lakini nafsi hiyo hiyo ukiiruhusu ikaingiliwa na ibilisi kwa kumkataa Mungu ndio inakufanya uwe hivi ilivyo sasa. Baada ya kumkataa Mungu umempa nafasi ibilisi akutumie kufanya evil manipulation.

Umewahi kushuudia ajari mbaya abiria wote wakafa halafu akapona mtoto peke yake!?

Kifo ni adhabu tuliyopewa Mungu, hakuna binadamu anaependa kufa sasa mpaka Leo hii hakuna mwenye uwezo wa kuzuia kifo hiyo tu clarity tosha kuwa kifo ni uthibitisho.
Kwa nini Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aumbe ulimwengu ambao Ibilisi anaweza kuwepo wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao Ibilisi hawezi kuwepo?
 
Kuna aliyethibitisha Mungu yupo? Au hadithi tu bado?
 
Back
Top Bottom