Namshauri Rais afute vitambulisho vya wamachinga

Namshauri Rais afute vitambulisho vya wamachinga

Tulimumu

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2013
Posts
14,395
Reaction score
13,266
Huenda aliwaza vizuri lakini utekelezaji wake imekuwa ni karaha kwa wafanya biashara wadogo. Watendaji wa serikali wanatumia nguvu kubwa sana kukazimisha watu kununua vitambulisho hivyo. Sehemu nyingine watumishi wametishiwa hadi kufukuzwa kazi wasipofanikiwa kuuza vitambulisho hivyo.

Hapa ilipaswa kujuliuliza kwanini vitambulisho hivyo havinunuliwi? Jibu ni fupi tu wafanyabiashara wengi wana mitaji midogo sana hivyo kwa lugha nyingine wao ni masikini kabisa. Sasa kwenda kuchukua 20,000/= kwa masikini kwa kisingizio cha kitambulisho hiyo ni sawa uuaji. Ukiangalia baadhi ya wafanyabiashara wanaolazimishwa kununua vitambulisho hivyo mitaji yao ni chini ya 20,000/= halafu analazimishwa kununua kitambulisho cha 20,000/= ambayo hana. Hivi shoe shiner na muuza karanga kwa mfano mitaji yao ni shilingi ngapi hadi walazimishwe kununua kitambulisho?

Kwakuwa hili lilikuwa ni wazo binafsi la rais kama alivyoeleza yeye mwenyewe na kwakuwa ni yeye ndiye aliyevitengeneza na kwakuwa ni yeye ndiye aliyepanga bei namshauri avifute kabisa vitambulisho hivyo kwani vina mshushia hadhi sana miongoni mwa wafanyabiashara wadogo masikini na wananchi kwa ujumla. Vinginevyo ili kuwasaidia ni bora avitoe bure. Ikumbukwe madhara yoyoyte watakayopata wamachinga, watumishi na wananchi kwa ujumla lawama zote zitaelekezwa kwake rais kwakuwa yeye ndiye mwenye vitambulisho hivyo.

Ni vizuri rais ajue kuwa watendaji wake wanafanya kazi kwa nidhamu ya woga sana na kujipendekeza ili kumfurahisha yeye hivyo wanaoumia ni wananchi kutokana na hatua wanazochukua dhidi ya wananchi. Ni watendaji wasioweza kutoa ushauri pale wanapoona mambo magumu zaidi ya kutumia nguvu ili kila mmoja aonekane anaweza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Sasa hivi Hali kwake imekuwa Ni tete.
Misaada ndiyo haieleweki.
Biashara na makampuni binafsi yanafungwa ukitaka kuthibitisha nenda kariakoo ukitaka fremu au stoo unapata Tena bila dalali kwani namba zimebandikwa kwenye fremu.
Sasa inabidi mbinu za ziada zitumike Kama kupitia polisi barabarani na hivyo vitambulisho.

Huo ushauri Ni mgumu kupokelewa kutokana na Hali ilivyo
 
Ameshafeli tayari. Issue ya kodi ni ya kisheria ambako TRA ndio wahusika. Sasa hili zoezi la kodi lakini wahusika ni ikulu na wakuu wa mikoa na wilaya. Kiujumla jiwe kafeli tena kama kwny korosho
 
Bado tu hujagundua lengo la hivyo vitambulisho? Lengo ni kukusanya kodi kutoka kwa watu ambao hawana pato la kutosha kuwadai kodi. In other words, day light institutional robbery.
 
rais anawapenda mno wamachinga na wafanyabiashara wadogo ndio maana amewaletea hivyo vitambulisho bure ili wasisumbuliwe na mgambo
 
Kuna mkoa mmoja nasikia wameazimia mpaka wale waokota makopo nao wanunue hivyo vitambukisho.

Hivi mtaji wa muokota makopo ni shilingi ngapi?

Wrong plan ...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huenda aliwaza vizuri lakini utekelezaji wake imekuwa ni karaha kwa wafanya biashara wadogo. Watendaji wa serikali wanatumia nguvu kubwa sana kukazimisha watu kununua vitambulisho hivyo. Sehemu nyingine watumishi wametishiwa hadi kufukuzwa kazi wasipofanikiwa kuuza vitambulisho hivyo.

Hapa ilipaswa kujuliuliza kwanini vitambulisho hivyo havinunuliwi? Jibu ni fupi tu wafanyabiashara wengi wana mitaji midogo sana hivyo kwa lugha nyingine wao ni masikini kabisa. Sasa kwenda kuchukua 20,000/= kwa masikini kwa kisingizio cha kitambulisho hiyo ni sawa uuaji. Ukiangalia baadhi ya wafanyabiashara wanaolazimishwa kununua vitambulisho hivyo mitaji yao ni chini ya 20,000/= halafu analazimishwa kununua kitambulisho cha 20,000/= ambayo hana. Hivi shoe shiner na muuza karanga kwa mfano mitaji yao ni shilingi ngapi hadi walazimishwe kununua kitambulisho?

Kwakuwa hili lilikuwa ni wazo binafsi la rais kama alivyoeleza yeye mwenyewe na kwakuwa ni yeye ndiye aliyevitengeneza na kwakuwa ni yeye ndiye aliyepanga bei namshauri avifute kabisa vitambulisho hivyo kwani vina mshushia hadhi sana miongoni mwa wafanyabiashara wadogo masikini na wananchi kwa ujumla. Vinginevyo ili kuwasaidia ni bora avitoe bure. Ikumbukwe madhara yoyoyte watakayopata wamachinga, watumishi na wananchi kwa ujumla lawama zote zitaelekezwa kwake rais kwakuwa yeye ndiye mwenye vitambulisho hivyo.

Ni vizuri rais ajue kuwa watendaji wake wanafanya kazi kwa nidhamu ya woga sana na kujipendekeza ili kumfurahisha yeye hivyo wanaoumia ni wananchi kutokana na hatua wanazochukua dhidi ya wananchi. Ni watendaji wasioweza kutoa ushauri pale wanapoona mambo magumu zaidi ya kutumia nguvu ili kila mmoja aonekane anaweza.

Sent using Jamii Forums mobile app

Nakubaliana nawe kwa 100% kwani kuna sehemu nilikuwa nimekaa jana napiga zangu ' Soga ' kama kawaida akaja Mtendaji mmoja ( namuhifadhi ) na katika mazungumzo yetu mengine baadae akaniambie tena mbele ya Watu wengine waliokuwepo pale kwamba ananiomba Mimi ' niwashawishi ' Wafanyabiashara wa eneo husika ambao wengi Wao ni Marafiki zangu wakubwa tu na tunaheshimiana mno ili wakachukue Vitambulisho hivyo kwakuwa hadi hivi sasa ' vinawadodea ' kama siyo ' kuwaozea ' kabisa Maofisini Kwao na nilishtuka sana na kuanza Kujiuliza Maswali lukuki / mengi mno juu ya hili jambo la Vitambulisho. Nadhani linatakiwa liangaliwe Kiumakini na si vibaya wala dhambi likawa ' revised ' kwa Manufaa mazuri, mema na makubwa ya baadae. Sitaki Kuamini kwakuwa bado sijathibitisha ila kuna taarifa nimesikia kwamba sehemu zingine Watu ( Wamachinga ) hawapewi hivi Vitambulisho mpaka Kwanza wawe ' Wanachama ' au ' Waungaji Mkono ' wa Kutukuka wa Mitaa ya Mnazi Mmoja na Lumumba jijini Dar es Salaam.
 
Ameshafeli tayari. Issue ya kodi ni ya kisheria ambako TRA ndio wahusika. Sasa hili zoezi la kodi lakini wahusika ni ikulu na wakuu wa mikoa na wilaya. Kiujumla jiwe kafeli tena kama kwny korosho
Kwa hiyo ni mapato nje ya mfumo wa TRA, CAG anakazi kubwa
 
Huenda aliwaza vizuri lakini utekelezaji wake imekuwa ni karaha kwa wafanya biashara wadogo. Watendaji wa serikali wanatumia nguvu kubwa sana kukazimisha watu kununua vitambulisho hivyo. Sehemu nyingine watumishi wametishiwa hadi kufukuzwa kazi wasipofanikiwa kuuza vitambulisho hivyo.

Hapa ilipaswa kujuliuliza kwanini vitambulisho hivyo havinunuliwi? Jibu ni fupi tu wafanyabiashara wengi wana mitaji midogo sana hivyo kwa lugha nyingine wao ni masikini kabisa. Sasa kwenda kuchukua 20,000/= kwa masikini kwa kisingizio cha kitambulisho hiyo ni sawa uuaji. Ukiangalia baadhi ya wafanyabiashara wanaolazimishwa kununua vitambulisho hivyo mitaji yao ni chini ya 20,000/= halafu analazimishwa kununua kitambulisho cha 20,000/= ambayo hana. Hivi shoe shiner na muuza karanga kwa mfano mitaji yao ni shilingi ngapi hadi walazimishwe kununua kitambulisho?

Kwakuwa hili lilikuwa ni wazo binafsi la rais kama alivyoeleza yeye mwenyewe na kwakuwa ni yeye ndiye aliyevitengeneza na kwakuwa ni yeye ndiye aliyepanga bei namshauri avifute kabisa vitambulisho hivyo kwani vina mshushia hadhi sana miongoni mwa wafanyabiashara wadogo masikini na wananchi kwa ujumla. Vinginevyo ili kuwasaidia ni bora avitoe bure. Ikumbukwe madhara yoyoyte watakayopata wamachinga, watumishi na wananchi kwa ujumla lawama zote zitaelekezwa kwake rais kwakuwa yeye ndiye mwenye vitambulisho hivyo.

Ni vizuri rais ajue kuwa watendaji wake wanafanya kazi kwa nidhamu ya woga sana na kujipendekeza ili kumfurahisha yeye hivyo wanaoumia ni wananchi kutokana na hatua wanazochukua dhidi ya wananchi. Ni watendaji wasioweza kutoa ushauri pale wanapoona mambo magumu zaidi ya kutumia nguvu ili kila mmoja aonekane anaweza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ushauri wako ni mzuri sana mkuu.Wananchi wa kawaida niliopata nafasi ya kuongea nao hawapendi kabisa wazo hili.Wengi wanaona ni njia tu ya serikali kujitafutia mapato bila,kujali hali yao ya maisha.Wengi wao wanasema kula yao tu ni shida,sembuse kupata Sh.20,000?Mmoja akaniambia,
"nampenda sana Rais Magufuli,lakini katika hili, amebugi step.Akaongeza,
"niandikishwe ili iweje hasa,mimi mlala hoi kitambulisho hicho hakinisaidii?"
 
Ifike wakati watanzania tuache ujinga kama watu hawataki kutoa elfu ishirini kwa ajili ya kitambulisho kitakacho wa exempt kulipa kodi ambayo ingekuwa kubwa zaidi basi hao watu wasidai maji, umeme, barabara wala hudumu yoyote toka serikalini , haiwezekani watu wachache watozwe kodi kwa ajili ya 60% ya watanzania wengine. Hivi ikitokea tunyimwe msaada tutaishiji kama nchi? Mbona watu mnaendekeza uvivu, ujinga na ukosefu wa ubunifu wa kutafuta pesa. Watu wanatoa sababu kibao lakini wanasahau uvivu na ujinga wa watu wasiolipa kodi. Hii nchi ingekuwa chini ya wakoloni au hao wazungu wanaotupa misaada wote tungelipa kodi hata kwa fimbo.
 
Huenda aliwaza vizuri lakini utekelezaji wake imekuwa ni karaha kwa wafanya biashara wadogo. Watendaji wa serikali wanatumia nguvu kubwa sana kukazimisha watu kununua vitambulisho hivyo. Sehemu nyingine watumishi wametishiwa hadi kufukuzwa kazi wasipofanikiwa kuuza vitambulisho hivyo.

Hapa ilipaswa kujuliuliza kwanini vitambulisho hivyo havinunuliwi? Jibu ni fupi tu wafanyabiashara wengi wana mitaji midogo sana hivyo kwa lugha nyingine wao ni masikini kabisa. Sasa kwenda kuchukua 20,000/= kwa masikini kwa kisingizio cha kitambulisho hiyo ni sawa uuaji. Ukiangalia baadhi ya wafanyabiashara wanaolazimishwa kununua vitambulisho hivyo mitaji yao ni chini ya 20,000/= halafu analazimishwa kununua kitambulisho cha 20,000/= ambayo hana. Hivi shoe shiner na muuza karanga kwa mfano mitaji yao ni shilingi ngapi hadi walazimishwe kununua kitambulisho?

Kwakuwa hili lilikuwa ni wazo binafsi la rais kama alivyoeleza yeye mwenyewe na kwakuwa ni yeye ndiye aliyevitengeneza na kwakuwa ni yeye ndiye aliyepanga bei namshauri avifute kabisa vitambulisho hivyo kwani vina mshushia hadhi sana miongoni mwa wafanyabiashara wadogo masikini na wananchi kwa ujumla. Vinginevyo ili kuwasaidia ni bora avitoe bure. Ikumbukwe madhara yoyoyte watakayopata wamachinga, watumishi na wananchi kwa ujumla lawama zote zitaelekezwa kwake rais kwakuwa yeye ndiye mwenye vitambulisho hivyo.

Ni vizuri rais ajue kuwa watendaji wake wanafanya kazi kwa nidhamu ya woga sana na kujipendekeza ili kumfurahisha yeye hivyo wanaoumia ni wananchi kutokana na hatua wanazochukua dhidi ya wananchi. Ni watendaji wasioweza kutoa ushauri pale wanapoona mambo magumu zaidi ya kutumia nguvu ili kila mmoja aonekane anaweza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa mujibu wa RC wa Ruvuma hata hawa wanapaswa kununua kitambulisho hicho

FB_IMG_1549369100113.jpeg
 
Back
Top Bottom