MKWEPA KODI
JF-Expert Member
- Nov 28, 2015
- 28,707
- 71,003
Huyu jamaa yetu Jokolilo alikuwa rafiki yetu sana mimi bonge na makame, Jokolilo ni mrefu kwa umbile kutuzidi mimi na makame, huwa anapenda sana kujiita kuwa yeye ni mlingoti mrefu kutuzidi sisi,
Kwa ujumla Jokolilo ana madharau sana kwa sababu mara nyingi huwa anatupa sapoti kifedha kwa mambo mbalimbali basi anajiona kama malaika, hata tukiwa tunajitwanga na pombe anataka kuongea yeye tu kama vile yeye ndiye mwenye akili peke yake,
Halafu kinachoudhi ana kicheko huwa anajilazimisha kucheka ukimuona anavyocheka utadhani baboon anakula mahindi, tulivyoona anatuzuia kuongea na anataka kuongea yeye tu peke yake tukaamua kwenda studio kurekodi maigizo na nyimbo mbalimbali ili tujiburudishe kimyakimya bila kuongea ili tumfurahishe,
Sasa cha kushangaza amewatuma sungusungu na kumweka ndani mmiliki wa studio leo ni siku ya tatu, kwa sasa tunasali kumuombea huyo mmiliki wa studio ili aachiwe, sasa hatujui tufanye nini ili tujiliwaze, ila tuna hasira sana na huyu Jokolilo
Kwa ujumla Jokolilo ana madharau sana kwa sababu mara nyingi huwa anatupa sapoti kifedha kwa mambo mbalimbali basi anajiona kama malaika, hata tukiwa tunajitwanga na pombe anataka kuongea yeye tu kama vile yeye ndiye mwenye akili peke yake,
Halafu kinachoudhi ana kicheko huwa anajilazimisha kucheka ukimuona anavyocheka utadhani baboon anakula mahindi, tulivyoona anatuzuia kuongea na anataka kuongea yeye tu peke yake tukaamua kwenda studio kurekodi maigizo na nyimbo mbalimbali ili tujiburudishe kimyakimya bila kuongea ili tumfurahishe,
Sasa cha kushangaza amewatuma sungusungu na kumweka ndani mmiliki wa studio leo ni siku ya tatu, kwa sasa tunasali kumuombea huyo mmiliki wa studio ili aachiwe, sasa hatujui tufanye nini ili tujiliwaze, ila tuna hasira sana na huyu Jokolilo