Kaka, kwa kweli pole kwa hayo yanayotokea kwenye ndoa yako. Tafadhali jua na amini kuwa si rahisi ukajijua wewe mwenyewe kwa 100% na hasa udhaifu wako. Ni dhahiri mdogo wangu unayo mapungufu ambayo mke wako hakuyajua mwanzoni wakati wa uchumba. Kwa jinsi walivyo wengi wao, amekustadi, akaona udhaifu wako ulipo na akakulinganisha na "rafiki yake wa kiume". Anadhani kuwa, kwa vile mlishaoana na watu wote wanajua basi ni aibu kukwambia baadhi ya mambo ambayo yatakuumiza, anaona ni bora iwe kimya kimya tu potelea mbali ukija gundua utaamua kumuuliza na atakataa... anaamini hutakuwa na ushahidi dhahiri kuwa anagawa p... nje. Na pengine kama anajua kuwa alishawahi kukuambia/kukulalamikia juu ya wewe kutomfikisha kunako theluji za Evarest,basi kwake yeye anachukulia hicho kama msingi wa uhalali wa yeye kuyakuza mahusiano yake na huyo mme mwenza wako. USHAURI WANGU: Hakikisha kila mmoja wenu anakuwa na Uhuru usiozidi 50% (Wewe 50% na yeye pia 50%) hii itawasaidia kwa kila mmoja wenu kujiona kuwa hakandamizwi, hanyonywi, hapuuzwi na wala hana haki ya kufanya jambo lolote zuri au baya pasipo kumshirikisha mwenzake.(Ndoa ni ya wawili, si mmoja bhana!) Pia kuwa na kiasi katika kumpenda. Usimpende hadi ukashindwa kumkaripia na kumshauri kwa tabia zake zinazokukera na ambazo kabisa unaziona ni hatarishi kwa ndoa yenu. Ukishindwa kabisa, basi hebu washirikishe watu wengine unaoamini wana hekima na heshima ili wawashauri nyote kwa pamoja ama peke yake kwa kadiri ya uwezekano. vinginevyo ningependa kujua hali ya ndoa yenu baada ya mwezi mmoja.