SHIEKA
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,240
- 4,270
Ni mwalimu wa Hisabati Shule ya Msingi Kimara B wilayani Kinondoni.
Mwanafunzi aliyepata alama 50 juu ya 50 katika somo la Hisabati alifundishwa na mwalimu huyu
aitwaye Aron Athanas
Kwa mujib wa mahojiano mwalimu huyu aliyoyafanya na televishen ya East Africa, mwalimu huyu
alieleza kwamba kwenye mitihani ya taifa anaandaa wanafunzi wake kuanzia darasa la tatu.Msichana Rachel Kiunsi ni mmoja wa
wanafunzi walioandaliwa na mwalimu huyu kwenye somo la hisabati tangu wakiwa darasa la tatu.
Mwalimu huyu anaeleza kwamba anatumia mbinu alizobuni za kuwavuta wanafunzi kulipenda somo la hisabati
na mbiu hii inatokana na motisha binafsi alio nao na si motisha kutoka serikalini.
Bila shaka wapo waalimu wengi wa aina hii ya mwalimu aron ambao wamejaa ubunifu katika ufundishaji wa masomo lakini serikali haiwaongezei motisha kwenye ufundishaji kwa kuboresha maslahi na vifaa vya ufundishaji.
Yanayotokea wizara ya afya ndio polepole yananyemelea wizara ya elimu na itafika siku akina aron watagoma, na hapatakuwepo tena wanafunzi kama Rachel na wengineo kupata alama A au B kwenye masomo yao.
Mwanafunzi Rachel Kiunsi
Mwanafunzi aliyepata alama 50 juu ya 50 katika somo la Hisabati alifundishwa na mwalimu huyu
aitwaye Aron Athanas
Kwa mujib wa mahojiano mwalimu huyu aliyoyafanya na televishen ya East Africa, mwalimu huyu
alieleza kwamba kwenye mitihani ya taifa anaandaa wanafunzi wake kuanzia darasa la tatu.Msichana Rachel Kiunsi ni mmoja wa
wanafunzi walioandaliwa na mwalimu huyu kwenye somo la hisabati tangu wakiwa darasa la tatu.
Mwalimu huyu anaeleza kwamba anatumia mbinu alizobuni za kuwavuta wanafunzi kulipenda somo la hisabati
na mbiu hii inatokana na motisha binafsi alio nao na si motisha kutoka serikalini.
Bila shaka wapo waalimu wengi wa aina hii ya mwalimu aron ambao wamejaa ubunifu katika ufundishaji wa masomo lakini serikali haiwaongezei motisha kwenye ufundishaji kwa kuboresha maslahi na vifaa vya ufundishaji.
Yanayotokea wizara ya afya ndio polepole yananyemelea wizara ya elimu na itafika siku akina aron watagoma, na hapatakuwepo tena wanafunzi kama Rachel na wengineo kupata alama A au B kwenye masomo yao.
Mwanafunzi Rachel Kiunsi