Mwita Matteo
JF-Expert Member
- May 16, 2010
- 216
- 55
Kwani inakatazwa?Si ni bora yeye kuliko wale ambao hawaisaidii jamii na badala yake wanaishia kuibuka na kuhadaa wananchi?
duh. Umejuaje kuwa nI yeye?okey tumekupata bwana Aweda kwa kuja na Id yako nyingine kuja kujifagilia mwenyewe humu JF juu ya kuattend kwako ITV katika mdahalo
pamoja na aliyoyasema lakini aliupotosha umma kuhusu maraisi wa Mexico, rais wa sasa wa Mexico anaitwa Enrique Peña Nieto, na si Felipe Calderón kama alivyosema yeye wakati anachangia kuhusu tatizo la madawa ya kulevya nchini
okey tumekupata bwana Aweda kwa kuja na Id yako nyingine kuja kujifagilia mwenyewe humu JF juu ya kuattend kwako ITV katika mdahalo
Kamanda Aweda ameonyesha ujasiri na umahiri wa hali ya juu,hata kama kwao Mbulu level yake ni huko Dar kwenye jimbo la akina "Zungu" wanao tuhumiwa kwa uuzaji "unga"
Jana Aweda alinifurahisha sana kwenye ile kipindi yao ya malumbano ya hoja ya kwenye ITV kuliko mtu mwingine yeyote.
Mada ilikuwa inasema, MADAWA YA KULEVYA KUANGAMIZA VIJANA WETU NA WATANZANIA, NINI KIFANYIKE?
Kamanda wangu Aweda aliibua bifu la Reginald Mengi na Godrefy Nzowa. Nzowa alikuwa amekaa kwenye kiti cha mchokozo mada. Aweda alimwaliza Godfrey Nzowa swali gumu ambalo halikujibiwa. Godfrey Nzowa ni bosi wa kuzuia madawa ya kulevya tena akajisifia kuwa yeye ni bosi wa Tume ya kuzuia madawa ya kulevya kwa miaka saba.
Swali la AweDA,
kuna mtu moja anayeheshimika sana kwenye jamii ya watanzania anaitwa Reginald Mengi na alimtaja wazi. Miaka 2 iliyopita alikutuhumu wewe Nzowa kuwa ulikuwa umetega mtego wa kumbambikia mtoto wa Bwana Reginald Mengi kwa madawa ya kulevya. Je, ni kweli? Halafu akawekaga na chumvi kweye kidonda kwa kuongezesha kuwa ninavyo jua mimi, wewe bado hujakanusha taarifa hiyo. akamalizia kwa kusema tunaomba utupe majibu leo.
Binafsi sijui habari ya Mengi kumtuhumu Nzowa kutaka kumbambikia mtoto wa Mengi kwa madawa ya kulevya ilishia wapi?.
Bahati mbaya Godfrey Nzowa hakujibu na alikaa kimya kama hajasikia na wasimamizi wa kipindi hawakumbana hata kidogo.
Hongera Aweda, lakini taratibu kamanda wangu si unajua kuna tindi kali siku hizi??? Hivi kama wanapanga kumbambikia mtoto wa Mengi madawa ya kulevya, si watamdhuru na yeye Aweda? Namshauri tu kamanda wetu. Nampa Big up.
Mimi nawashangaa sana watanzania wenzangu yani tunafikia kuamini kuwa yeyote anaye pigania haki za jamii yake basi anataka uoongozi. Inauma sana kuona uwezo wetu wa kufikiria umegota kkuamini hivyo maana yake mtu akipigwa ntu asiamulie kwani atambiwa anataka cheo tuachane na mawazo hayo Aweda he was right to ask such question.
okey tumekupata bwana Aweda kwa kuja na Id yako nyingine kuja kujifagilia mwenyewe humu JF juu ya kuattend kwako ITV katika mdahalo
Matema Beach,
Nashukuru kwa comment yako. Watu hawanitendei haki kwa kunibambikia majimbo ya kugombea ubunge wakati mimi sijatangaza nia ya kugombea udiwani, uenyekiti wa mtaa/kijiji wala wala ubunge ktk maeneo hayo yanayotajwa tajwa. muda uliopo ni kuwajenga mtandao wa chama.
Madawa ya kulevya yanaangamiza watoto wetu.
Hata mimi niliangalia, je, mada ya jana madawa ya kulevya kuendelea kuangamiza vijana wetu, nini kifanyike? AWEDA alimwuliza Nzowa kuwa wewe unatuhumiwa kubambika kesi ya mtoto wa Mengi je, jibu hoja. Yule dada alitaka kumsaidia tu Nzowa. Ukweli swali lilikuwa ndani ya mada kabisa, tena sana.
labda ni magreth cosmas kama sijakoseaYule mzuri mweusi kidogo jina la pili anaitwa Cosmas, wadada wako 2 tu. Siyo fatma Almasi Nyangasa. Mara nyingi yuko Redio one.
TATIZO LA VIJANA WA CHADEMA..... sio kutokuwa weledi,bali ni kila kitu kuzungumzwa kisiasa na kujitafutia umaarufu binafsi na wa chama. wanafika mahali wanatanguliza siasa zaidi kuliko kuli-approach tatizo na kuli address.
huu ukamanda wa kuishia kuvaa gwanda na kujilipua kwa kutumia vumbi wala hautaifikisha nchi yetu popote.
ule mjadala haukuwa na malengo ambayo AWEDA alijaribu kuyaongelea... he was just out of the point and shamefull
hukuangalia kipindi nadhani.Kwa hili la Madawa ya kulevya yanayoangamiza watoto wetu, tuache uccm na uchadema kwanza - vijana wetu kwanza. ktk hili Aweda alikuwa sahihi kuhoji usafi wa NZOWA. Tuache ushabiki.
TATIZO LA VIJANA WA CHADEMA..... sio kutokuwa weledi,bali ni kila kitu kuzungumzwa kisiasa na kujitafutia umaarufu binafsi na wa chama. wanafika mahali wanatanguliza siasa zaidi kuliko kuli-approach tatizo na kuli address.
huu ukamanda wa kuishia kuvaa gwanda na kujilipua kwa kutumia vumbi wala hautaifikisha nchi yetu popote.
ule mjadala haukuwa na malengo ambayo AWEDA alijaribu kuyaongelea... he was just out of the point and shamefull