Nampenda sana ila simuelewi

Nampenda sana ila simuelewi

Yeye hakupendi halafu nawewe unampenda na pia Unamwogopa,Mwanaume hupaswi kuwa hivyo na hapo ukweli ni kwamba kaonesha ishara zote za kutokukujali wewe na atakuwa na mtu mwingine huyo. Achana naye kwani atakutesa sana halafu pia utapoteza muda mwingi ambao ungeweza kuutumia kuanzisha mahusiano kwa mwingine.

Kiukweli nikiachana nae huyu, sitapoteza muda tena kwenye mahusiano kwa muda fulani maana kuna muda nikikaa nikiwaza anayofanya huwa nacheka kwa huzuni
 
Mambo yakungangania sehem usiyotakiwa ndo ayo. Bora usepe utakuja kubwagwa usipotarajia
 
Mpaka akupige puu ndo utaelewa

Keshaniumiza sana hadi shakuwa sugu, akinitosa sitashangaa, tasonga mbele tu kiume, huwa natatua kila kitu kwa upendo wa dhati na upole ila mbidada kama hanisomi vile ndo maana simuelewi kabisa
 
Sitisha mawasiliano ghafla bila taarifa, usipige simu wala kutext. Akikuuliza tatizo, we mwambie umechoka na unahitaji kujitoa katika uhusiano huo. Ukishamueleza hilo, endelea na yako na usirudi nyuma kwa sababu huyo mwanamke hakupendi na anakuchezea na kukufanya bweg.e kwa vile inaonekana wewe ni mpole sana au amethibitisha kuwa unampenda sana na huna uwezo wa kumuacha.
 
Mkuu mimi ni ke!
Ila naomba nikwambie hapo umeiingia miguu yote miwili na amekugundua! Hayuko na feeling na wewe ila kama binti kuonesha ana mtu na coz unaonekana una mpenda ndo maana yuko hapo!

1. punguza mawasiliano kama kweli anakupenda atakutafuta (kama sms zilikuwa 10 peleka 5 kisha 1) hapa utaumia ila baadae utazoea

2. Punguza matunzo fanya pale anapoomba na siyo lazima kila akiomba utimize (kama yeye kakosa hata wewe unaweza kukosa pia )
Utapata shida mwanzoni lakn ni namna nzur ya kujua position yako kwake! Unaweza ukute kakufanya wa back up tu!!!

Exactly
 
Mkuu mimi ni ke!
Ila naomba nikwambie hapo umeiingia miguu yote miwili na amekugundua! Hayuko na feeling na wewe ila kama binti kuonesha ana mtu na coz unaonekana una mpenda ndo maana yuko hapo!

1. punguza mawasiliano kama kweli anakupenda atakutafuta (kama sms zilikuwa 10 peleka 5 kisha 1) hapa utaumia ila baadae utazoea

2. Punguza matunzo fanya pale anapoomba na siyo lazima kila akiomba utimize (kama yeye kakosa hata wewe unaweza kukosa pia )
Utapata shida mwanzoni lakn ni namna nzur ya kujua position yako kwake! Unaweza ukute kakufanya wa back up tu!!!

Mkuu, ww mwanake nimekupenda, una akili sana. Pongezi zako.
 
Mwananchi B

ilo tatizo ata mm ninalo yani natengenezewa makosa kila siku yani tunaweza kuwa na furaha ghafla tu ana ni badilikia tupo mikoa miwili tofauti nami msaada plz maana stress sana
 
Last edited by a moderator:
Mpe Atm card yako na password tuone.
 
Wewe ndio tatizo. Kuna mahali huwa naona humu watu wanasema imeandikwa hawa viumbe inatakiwa uishi nao kwa akili, hawakukosea kabisa. Ni hivi hapo kuna mawili.
  1. Huyo mdada anakufanya we mchepuko, hakupendi hata nukta.
  2. Ni aina ya wale wasichana ambao wanaamini mwanaume anatakiwa kuwa mbabe na mkali hivyo wakipata watu wanaojali sana wanajikuta tu wanakuwa wakorofi maana hawapati kile wanachotaka. Ninaamini kwa kiasi kikubwa hiki ndicho kinachotokea kwa upande wako. Dawa ya hili tatizo huwa ni ndogo sana, unachotakiwa ni kufanya kama vile hayupo. Mpotezee hivi kidogo, saa nyingine mwambie nakuja kukutembelea halafu usitokee bila taarifa akikuuliza mwambie ulibanwa na majukumu. Halafu akiwa mkali we kuwa mkali mara 100 halafu cheki situation. Kumbuka Sio kila mwanamke anaelewa lugha ya upole.
Ni hayo tu kwa sasa.

Good,..
Wish wanaume wote tungekua na mtazamo kama huu,..hawa viumbe wasingetuzea kamwe.Hua nakereheka sana kumuona mwanaume tena kijana mwenzangu analalamika tena mitandao eti anapelekeshwa na mwanamke wake_huu ni ubwege ulioletwa na hizi shule za academy.
Mwanaume ni kichwa cha nyumba ni lazima ujitambue na uiheshimu nafasi yako kama mwanaume-ingawa sio kunyanyasa wanawake ila ni lazima mwanamke wako awe anakuheshimu na kukuogopa wakati mwingine....mtachapiwa sana wake zenu huku mkijifanya wa kishua.

Ukiona anakuzingua wewe mteme for good and never come back,...sio kuja kulalama kwenye mitandao.
 
ilo tatizo ata mm ninalo yani natengenezewa makosa kila siku yani tunaweza kuwa na furaha ghafla tu ana ni badilikia tupo mikoa miwili tofauti nami msaada plz maana stress sana

Mwanamke anakupa stress-unashindwa kumzibiti unakuja kulalamika kwenye mitandao,...hebu jiongezeni kidogo basi.
 
Sitisha mawasiliano ghafla bila taarifa, usipige simu wala kutext. Akikuuliza tatizo, we mwambie umechoka na unahitaji kujitoa katika uhusiano huo. Ukishamueleza hilo, endelea na yako na usirudi nyuma kwa sababu huyo mwanamke hakupendi na anakuchezea na kukufanya bweg.e kwa vile inaonekana wewe ni mpole sana au amethibitisha kuwa unampenda sana na huna uwezo wa kumuacha.

Safi-na huu ndio tunaita uanaume,...ajifunze kuchukua hatua kwa kufanya maamuzi ya kulinda hadhi yake.
 
Huyo mwanamke hana feelings na wewe kabisa,ni kwamba anajilazimisha tu kukuridhisha wewe na ndiomana viashiria vinajonyesha wazi kabisa.
wewe ndio unaetumia effort kubwa sana kufanya uhusiano wenu kuendelea kuwepo.
Jaribu ku invest muda na pesa yako kwenye mambo mengine ya msingi .
kama anakupenda kweli atatambua kuwa yeye pia ana jukumu la kuimalisha uhusiano wenu na c wewe peke yako.
 
Mwanamke anakupa stress-unashindwa kumzibiti unakuja kulalamika kwenye mitandao,...hebu jiongezeni kidogo basi.

aksante mkuu kwani mitandaoni c kuna ushauri na maoni jiongeze plus plus
 
aksante mkuu kwani mitandaoni c kuna ushauri na maoni jiongeze plus plus

Ni sawa lakn tulitaka kusikia umewajibika wewe binafsi kulinda usipatwe na stress then ndio uje huku,...umekaa tuu na mistress yako ndio unakuja kutuomba ushauri....tatizo ni chips mayai kila siku akili ni lazima ziwe laini kama za mwanamke,..try ugali -maharage.
 
Ni sawa lakn tulitaka kusikia umewajibika wewe binafsi kulinda usipatwe na stress then ndio uje huku,...umekaa tuu na mistress yako ndio unakuja kutuomba ushauri....tatizo ni chips mayai kila siku akili ni lazima ziwe laini kama za mwanamke,..try ugali -maharage.

poa ndugu nimekubari basi nipe ushauri nifanyaje ndugu maana imezidi
 
poa ndugu nimekubari basi nipe ushauri nifanyaje ndugu maana imezidi

Hivi mtu akikupa stress bado anakua rafiki yako ama..?...kwani kujitoa kwenye stress unashindwa nini,..au ndio umario wenu ndio unawasumbua i.e kulala kwa mwanamke,gari la mwanamke,chakula kwake,matibabu yeye,....ndio maana anakustress lakn bado unang'ang'ania.......
 
yaani huyo angekutana na mm angejuta, huwa sinaga ngoma zakukaanga, ukimjali anazingua, ukimpotezea eti sio romantic, naomba niwe na moyo huu huu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom