Bulaya001
JF-Expert Member
- Dec 21, 2018
- 5,868
- 6,480
Binti wahenga walipata kunena kuwa "matendo hukidhi maridhawa kuliko maneno"
Iko hivi, hiyo formula anayotumia mimi nilishaitumia sana enzi za ujana wangu, kwamba kwakua mahusiano yetu yanahusisha mpaka watu wa family basi sitokwambia sikutaki ili nisijekubeba lawama za familia, nataka tuachane automatic tu bila matamko officially.
Iko hivi, huyu Kijana wako anampenzi mwengine ambaye anampenda sana ila tatizo tayari na wewe ushakua nae..
Ngoja nikwambie, mimi sijawahi kumwambia mwanamke yeyote ambaye sitaki kuendelea kuwa nae kwenye mahusiano "TUACHANE". .Yaani sinaga confidance kabisa, ila ilikua nikitaka tuachane nakaa tu kimya, ikitokea umenibananisha tukawasiliana nakwambia nakupenda sana, hakuna kama wewe ila ukweli sikupendi na nitakaa hivyo mpaka wewe unakasirika na kujikuta unaamua kuniacha so nakua nimeepuka lawama, sasa huyu jamaa yako naona amefanana sana na kaliba yangu enzi hizo kabla sijaoa.
So jiongeze tu, hapo hamna UPENDO tena binti yangu, hata kukwambia ukatafute experience kwa mwengine ni namna ya kutaka tu kukufanya uende kule unogewe au apate sababu halali, HAKUNA mwanaume anayempenda mwanamke wake atayaruhusu eti "Akapate exprience" kwa mwanaume mwengine..
Pole sana bibie.
Sent using Jamii Forums mobile app