Kwani wakati wa NCCR ulikuwepo peke yako ina maana wengine hatukuwepo, enzi za Mrema upinzani ulikuwa mchanga haukuwa na mbinu madhubuti wala resources za kupambana figisu za CCM, mihemuko ilizidi uhalisia.
Matatizo ya NCCR yalikuwa tofauti na ya Chadema intelijensia ya NCCR ilikuwa tofauti na intelijensia ya Chadema leo, vile vile kitaasisi huwezi kuilinganisha Chadema na NCCR ya kina Mrema na Marando.
Hili ni andiko la George Kahangwa nafikiri unamfahamu vizuri ....soma katikati ya mstari ...
Muuliza swali nashawishika kuamini kwamba ulitaka kujua kweli. Kama ni utafiti naomba uzingatie taarifa hizi
1. Vuguvugu la wanamageuzi lilianza miaka ya 80 wakati wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam walipoanza kuhoji uwepo wa mfumo wa chama kimoja. Ni katika kipindi hicho Ndg. Mabere Nyaucho Marando (Katibu Mkuu wa kwanza wa NCCR) alifanya presentetion hapo chuoni kuhusu suala hilo. (Kama nakala ya presentation yake inaweza kupatikana basi siku moja tutaiweka hapa, kwa ajili ya kuweka kumbukumbu vizuri)
2. Mnamo mwaka 1984, Ndg.James Mapalala (makamu mwenyekiti wa kwanza wa NCCR) alimwandikia Mwalimu Nyerere barua ya wazi akitaka mfumo wa vyama vingi urejeshwe nchini (kumbuka ulikuwepo awali Mwalimu akaufuta)
3.Miaka saba baadaye (1990) Mwalimu akaanza kuelewa (wakati huo alishaacha urais) akaanza kusema si vibaya mfumo wa vyama vingi ukirejeshwa nchini
4. Mnamo mwaka 1991 wasomi wa UDSM, pamoja na wanaharakati wakaianzisha NCCR. Ikawa chini ya Uenyekiti wa Marehemu Chifu Abdallah Fundikira (waziri wa zamani wa Mwalimu), Makamu; Mapalala, Katibu Mkuu; Marando.
5. Mwaka huo huo 91 Rais Ali Hassan Mwinyi akaunda tume ya kukusanya maoni ya wananchi kama vyama vingi viruhusiwe au visiruhusiwe. Watanzania wengi hawakuvitaka, lakini wapo waliosema virudi.
6. Mzee Mwinyi akaheshimu mawazo ya wachache, mwaka 1992 akaruhusu virudishwe.
7. Mwaka huo 1992 (hapa ndipo sura ya sasa ilipotoka) waliokuwemo ndani ya NCCR wakagawanyika. Fundikira Mwenyekiti akaunda chama; UMD (japo kabla hajafa alirejea CCM), Mapalala huyo naye akaunda CCW ambayo kwa kushirikiana na Shaban Mloo wa KAMAHURU ya Zanzibar wakaunda CUF (sasa Mapalala yuko CHAUSTA). Marando akaendelea kuiongoza NCCR kwa kuiboresha na neno Mageuzi (sasa naye yuko CHADEMA), baadhi ya wajumbe wengine wa NCCR wakashiriki kuiunda CHADEMA wakitumia kaulimbiu ya NCCR 'demokrasia na maendeleo'. Na wengine wakaendelea kuunda vingine, matharani hata Mziray wa APPT-Maendeleo anatokea NCCR.
Kwa ufupi NCCR ilisambaa kabla ya ujio wa Mrema. 'ikawa kama maandiko; nitampiga mchungaji wa kondoo, na kondoo wa kundi lake watatawanyika)
8. Ndio sinema ya 1995 ikaanza (Hii sasa usome Kitabu cha Ndimara Tegambwage)