Namna pesa inabadilisha vijana kwenye mahusiano.

Namna pesa inabadilisha vijana kwenye mahusiano.

Diwani

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2014
Posts
2,824
Reaction score
3,021
Hapa nazungumzia sana vijana ambao wanajitafuta kwa wakati huu; mara nyingi jamii inawapa msukumo wa kutafuta hela na inawathibitishia kwamba bila kuwa na pesa wao si kitu na hawana nafasi ya kimaamuzi au ushawishi wowote kwenye jamii na hata kwenye mahusiano.

Vijana (ME) kwa sababu ya fikra hii hujikuta wakitafsiri maisha kwenye mitazamo ya kifedha tu, bila kujali utu, mapenzi, haiba, mwenendo na hata heshima. Ikitokea ameingia kwenye mahusiano na amepata fedha, atakuwa akitafsiri kila anachofanyiwa hata kama ni kwa upendo kutoka kwa mwenza wake, ataona ni kwa sababu ya fedha alizo nazo.

Hata akihudumiwa kama mume au mwenza; tafsiri juu ya afanyavyo ni kwa sababu ya pesa alizonazo, jambo ambalo linamuondolea utu na kumtazama mwenza wake kama bidhaa, na wakati mwingine kumuondolea heshima kama binadamu; hii inatokana na mtazamo aliopandikizwa kuhusu fedha.

Kuna kundi kubwa la Wanawake wanavumilia mahusiano machungu, kwa sababu tu ya kuwa na Wanaume wenye fedha, na Wanaume hao wanahisi wana haki ya kuwafanya lolote kwa sababu ya fedha zao.

Endapo mitazamo hii inabadilika, haitaweza kumuathiri Mwanamume anapopata mpenzi; atazingatia upendo na heshima kwa Mwanamke kwa sababu ni msingi wa mahusiano yake naye, na si kwa sababu ya fedha zake lakini jambo hili linaanzia na kupewa heshima hata pale ambapo hana kitu.
 
Kwani uwongo? Uwongo lakini?

Ishu wanapokosea ni kuliweka wazi. Wanatakiwa waishi katika imani hiyo bila ya kutamka wazi kwamba wanajua kinachoendelea.

They should play the game silently, since women hate it when you play it openly.
 
Kwani uwongo? Uwongo lakini?

Ishu wanapokosea ni kuliweka wazi. Wanatakiwa waishi katika imani hiyo bila ya kutamka wazi kwamba wanajua kinachoendelea.

They should play the game silently, since women hate it when you play it openly.
True
 
If i could give my children three things,it would be the strength to follow their passion,
the confidence to always know their self worth,and the ability to know how deeply and truly loved they are.
 
Kazi ya Mwanaume ni kusambaza his genes, kadiri ya uwezo wake, awe maskini au Tajiri.
Asili ya mwanamke ni manipulation ya potential (Me) kurutubisha mayai yake.Hasa vidume vyenye strong genes na uwezo wa kuhudumia watoto.
Hii ndio law of nature. Mengine ni ziada tu.
 
mahusiano ya sasa hivi kama huna kitu hupati mapenzi

mpz anataka abaya jipya wewe unaleta stori za vumilia mpz ipo siku nawe utapendeza
 
Kazi ya Mwanaume ni kusambaza his genes, kadiri ya uwezo wake, awe maskini au Tajiri.
Asili ya mwanamke ni manipulation ya potential (Me) kurutubisha mayai yake.Hasa vidume vyenye strong genes na uwezo wa kuhudumia watoto.
Hii ndio law of nature. Mengine ni ziada tu.
Law of Nature? Mengine ni ziada! Unadhani hatma ya maisha ni law of nature? Tungebaki kwenye law of Nature unadhani kungekuwa na civilization>?
 
mahusiano ya sasa hivi kama huna kitu hupati mapenzi

mpz anataka abaya jipya wewe unaleta stori za vumilia mpz ipo siku nawe utapendeza
Ni kama wanaishi kwenye scripts
 
Law of Nature? Mengine ni ziada! Unadhani hatma ya maisha ni law of nature? Tungebaki kwenye law of Nature unadhani kungekuwa na civilization>?
Natural selection ya stronger genes ndio matokeo ya freji, magari, vibarua, computers. Civilization.
 
Hapa nazungumzia sana vijana ambao wanajitafuta kwa wakati huu; mara nyingi jamii inawapa msukumo wa kutafuta hela na inawathibitishia kwamba bila kuwa na pesa wao si kitu na hawana nafasi ya kimaamuzi au ushawishi wowote kwenye jamii na hata kwenye mahusiano.

Vijana (ME) kwa sababu ya fikra hii hujikuta wakitafsiri maisha kwenye mitazamo ya kifedha tu, bila kujali utu, mapenzi, haiba, mwenendo na hata heshima. Ikitokea ameingia kwenye mahusiano na amepata fedha, atakuwa akitafsiri kila anachofanyiwa hata kama ni kwa upendo kutoka kwa mwenza wake, ataona ni kwa sababu ya fedha alizo nazo.

Hata akihudumiwa kama mume au mwenza; tafsiri juu ya afanyavyo ni kwa sababu ya pesa alizonazo, jambo ambalo linamuondolea utu na kumtazama mwenza wake kama bidhaa, na wakati mwingine kumuondolea heshima kama binadamu; hii inatokana na mtazamo aliopandikizwa kuhusu fedha.

Kuna kundi kubwa la Wanawake wanavumilia mahusiano machungu, kwa sababu tu ya kuwa na Wanaume wenye fedha, na Wanaume hao wanahisi wana haki ya kuwafanya lolote kwa sababu ya fedha zao.

Endapo mitazamo hii inabadilika, haitaweza kumuathiri Mwanamume anapopata mpenzi; atazingatia upendo na heshima kwa Mwanamke kwa sababu ni msingi wa mahusiano yake naye, na si kwa sababu ya fedha zake lakini jambo hili linaanzia na kupewa heshima hata pale ambapo hana kitu.
hivi hao viumbe(ke) unawajua ukiwa huna hiyo fedha???
acha tuwagegede tukipata pesa
 
Natural selection ya stronger genes ndio matokeo ya freji, magari, vibarua, computers. Civilization.
The existing genes are stronger genes, suala la weak genes ni mpaka pale nature itakapofanya selection. Na si kila selection inayofanyika inatokana na nature, nyingine ni miundo ya kijamii ambayo ni Man-made, do you think nature created homelessness? NO, but they are likely to perish, kwa sababu adaptation ya mazingira wanayoishi ni risky na wapo karibu na kifo. Nature haiku create NUCLEAR WEAPONS, guns neither; Lakini zinatumika na watu wana perish, are they weak genes? So, civilizition decides our fates too; hili suala la mahusiano lipo NATURALLY hata bata wana familia, how can a civilized monster like HUMANS aishi kama bitch fox? Yaani uwezo wake na ukuu wake ni kurutubisha tu mayai, na kuhudumia? Unahudumia vipi kama hisia zako za kuchukuliwa kama binadamu zinadharaulika in the name of HUNA HELA?
 
Heshima ya mwanaume Iko directly proportional na mchango wake (kifedha,au kimamlaka) katika mahusiano.Vinginevyo heshima yake inapungua
 
Man made, Nuclear, guns = Stronger genes secure his territory na his offsprings.
; hili suala la mahusiano lipo NATURALLY hata bata wana familia,
Kazi ya Mwanaume ni kusambaza his genes, kadiri ya uwezo wake, awe maskini au Tajiri.
Asili ya mwanamke ni manipulation ya potential (Me) kurutubisha mayai yake.Hasa vidume vyenye strong genes na uwezo wa kuhudumia watoto.
Hii ndio law of nature. Mengine ni ziada tu.
 
Unahudumia vipi kama hisia zako za kuchukuliwa kama binadamu zinadharaulika in the name of HUNA HELA?
Binadamu Ana evolve kutoka Hunter Gatherers. Pesa ni morden mikuki, pinde, mishale. Zama hizo mwindaji bora ndie aliyekuwa na heshima, wake wengi, na familia bora.
Huruma unazoleta ni ufeminia.
 
Binadamu Ana evolve kutoka Hunter Gatherers. Pesa ni morden mikuki, pinde, mishale. Zama hizo mwindaji bora ndie aliyekuwa na heshima, wake wengi, na familia bora.
Huruma unazoleta ni ufeminia.
😀😀😀😀 Mzee, wewe unazungumza animality hapa; unashindwa kutofautisha na Survival for the fittest notion. Kama unadhani civilization inaundwa na watu kama hao, maana yake tusingekuwapo, hata hicho unachoita Ufeminia kimeletwa na NATURE. So you got to learn and understand what does the nature offer to human sense.

Kuhus ku secure offspring of course they do, but they do not run off their rationality. Wewe hiko unachoita Ufeminia ndicho kimekulea, au unadhani nimekuja kutia huruma hapa? Kama una associate Ufeminia na huruma ni kwa sababu una confuse Feminism na Femininity. Usiogope kufikiri.
 
The existing genes are stronger genes, suala la weak genes ni mpaka pale nature itakapofanya selection. Na si kila selection inayofanyika inatokana na nature, nyingine ni miundo ya kijamii ambayo ni Man-made, do you think nature created homelessness? NO, but they are likely to perish, kwa sababu adaptation ya mazingira wanayoishi ni risky na wapo karibu na kifo. Nature haiku create NUCLEAR WEAPONS, guns neither; Lakini zinatumika na watu wana perish, are they weak genes? So, civilizition decides our fates too; hili suala la mahusiano lipo NATURALLY hata bata wana familia, how can a civilized monster like HUMANS aishi kama bitch fox? Yaani uwezo wake na ukuu wake ni kurutubisha tu mayai, na kuhudumia? Unahudumia vipi kama hisia zako za kuchukuliwa kama binadamu zinadharaulika in the name of HUNA HELA?
Mkuu,nafikiri wachangiaji wengi wamemiss point yako,

Mimi nilivyokuelewa ni kwamba,
Japo hela ni muhimu but the power of money should not exceed the power of love,
an excessive focus on wealth and materialism can lead to unhappiness and may even detract from meaningful relationship.
 
Mkuu,nafikiri wachangiaji wengi wamemiss point yako,

Mimi nilivyokuelewa ni kwamba,
Japo hela ni muhimu but the power of money should not exceed the power of love,
an excessive focus on wealth and materialism can lead to unhappiness and may even detract from meaningful relationship.
Of course.
 
Back
Top Bottom