Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,147
- 14,711
- Thread starter
- #21
Nyoka ni watambaachi au reptilia wasio na miguu. Kuna takriban spishi 3,000 duniani wako kwenye mabara yote nje ya Antaktiki na Aktiki.
Kama reptilia wote wana damu baridi na ngozi ya magamba. Wote ni wala nyama na spishi mbalimbali hutumia sumu kwa kuvionda lakini nyoka walio wengi hawana sumu wanashika windo kwa miili yao au kwa mdomo tu.
Wote wanazaa kwa njia ya mayai lakini spishi kadhaa hubeba mayai ndani ya mwili hadi wadogo wamekua tayari.
Mijusi wasio na miguu wanafanana sana na nyoka lakini nyoka hawana makope machoni wala masikio ya nje.
Kuna nyoka ndogo wenye sentimita kumi tu wakiwa wazima na nyoka kubwa hadi urefu wa mita 7.6. Nyoka anaweza kuanzia mika 5 mpaka miaka 7tu Mkuu.@Marire
Heshima kwako Mkuu. Pokea hiyo...
View attachment 202055