Nakupenda sana mke wangu (miaka 3 katika ndoa)

Nakupenda sana mke wangu (miaka 3 katika ndoa)

Ambiele Kiviele

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2014
Posts
15,271
Reaction score
29,937
Najua nina WEWE na hiyo INATOSHA! Wewe ndio siri ya NGUVU YANGU, wewe ndio kila kitu kwenye maisha yangu.. najua nimewahi kukukosea lakini ninachofahamu hata wakati nakukosea bado ulikuwa mwanamke pekee ninaekupenda, hakuna aliewahi kuzidi thamani yako, na nakuaminisha leo

HATATOKEA!!

Vingine ni ubinaadamu tu lakini haina maana kuna mbora zaidi yako, Huenda ubinaadamu huohuo kwa mwingine angeshindwa na kunikatia tamaa, lakini HUKUNIACHA, ulikuwa upande wangu, hata pale nilipokupa huzuni bado

FURAHA YANGU ndio kitu cha kwanza ulichokiangalia, kama MAMA anavyomtizama mtoto ndivyo ulivyokuwa ukinitazama, na bado hukuacha kuniombea kwenye kila ninalolifanya, wewe ni wa thamani kubwa sana kwangu, nashindwa jinsi ya kumshukuru

MUNGU kwa uwepo wako ndani ya maisha yangu, nilipofeli ulikuwepo, ninapofaulu upo na hata Dunia yote inizomee najua nina mtu ambae thamani yangu bado ni KUBWA mbele ya macho yake ambayo haitaka ishuke hata mbingu na ardhi vigeuke,

Katika anniversary yetu hii leo tukiwa tunatimiza miaka 3 ya ndoa yetu, bado

Sura ya kwanza inayonijia machoni kila ninapoamka ni YAKO!!

Mapenzi yangu kwako ni ya pekee kiasi hata nakosa cha kufananisha nayo....!!!!

Nakupenda Sana Mke Wangu
 
Acha kujidanganya na kutangazia watu eti unampenda mkeo. Miaka mitatu usiite ndoa. Subiri ifike miaka ishirini ya ndoa ndio uandike tutakupongeza. Wakati huo matiti yatakuwa yamekongoroka, meno nayo ya kuhesabu, atakuwa na kitambi, hapo ndio utwambie hiyo shine yako.
 
Juz nimepewa kibuti, Jana nimepewa kibuti, leo naona dalili zile zile akibaki mmoja nitajua hii ni chain nampa mimi kibuti sio kila mtu anioshee na mwaka mpya wote huu.
 
Miaka mitatu michache sana mkuu kuweza kupima ubora wa mapenzi yenu kila mmoja kwa mwenzake
 
Back
Top Bottom