Naendelea:
Ikafika kipindi akanionya zaidi ya mara nne ila nilijirudi na kulia na kuahidi nitaacha mambo yangu, japo hakuwa na uhakika ila alikuwa ananihisi tu.
Mwaka 2017 alinipa 500M kwa ajili ya kujenga nyumba nzuri ya kifahari na kufungua biashara pale Kariakoo ya hardware.
Alifanya hivi ili watoto wakija huku wasipate shida kuishi maisha angalau yenye unafuu. Hela hii aliyonipa ilikuwa ni mgao aliopata baada ya baba yake kuuza nyumba moja ya nyumba zake.
So hela yote akanipa mimi. Siku moja wakati nimeenda kariakoo nilitokea kumpenda dada mmoja ambaye alikuwa mweupe mwenye shape kubwa.
Aliitwa Manka(sio jina halisi na alikuwa Mchagga). Tulianza mahusiano rasmi kwani hakuonesha ugumu sana.
Ile pick up ya mama nilimdanganya nikampa huyu Manka ili abebee mizigo yake pale K/Koo kwani alikuwa na frame zake tatu zimepangana. Hakuwa haba alikuwa na hela.
So mama akawa anachukua usafiri kwenda shamba. Ikumbukwe nilikuwa nimejenga jumba ndogo ya kawaida tu huku Tz kwa wakati huo.
Manka alijitahidi kunizoea haraka haraka na ndani ya muda mfupi tukawa tumeshazoeana sana.
Wakati huo wote mawasiliano na Linda yaliendelea kama kawaida na nikamdanganya nakamilisha ile mipango.
To cut long story short, nilimuambia kuhusu ile milioni miatano kwenye acc na akashauri nimpe aingize kwenye biashara.
Sasa sijui kilitokea nini akampigia Linda simu na kumuambia amuachie mume wake. Linda alichukia mno na akakata mawasiliano na mimi mazima, hakutaka kusikia kitu tena kuhusu mimi.
Niliumia mno ila nilijishangaa nikapotezea(nafikiri huenda aliniroga huyu Mchagga).
Baada ya kumpa zile hela mawasiliano yakaanza kupungua. Akawa anachelewa kupokea simu zangu na wakati mwingine hapokei kabisa. Hiyo ilikuwa 2017 mwishoni mwezi wa 12 hivi.
Mwisho mwaka 2018 mwanzoni kabisa akaniandikia msg ndefu akisema nisimfuatilie tena,,nikithubutu atanitengenezea kesi ya madawa ya kulevya.
Pia akasema hata hicho kijumba ningeamua ningekichukua ila nimekuachia.
Sikuamini, kwa mara ya kwanza nililia nikigumia kama mbwa, nililia kilio cha mbwa. Sitoisahau siku ile***
Maisha niishiyo sasa nafikiri huenda ni laana imechangia,,hakunidai chochote yule Mzungu. Sijawaona tena wanangu mpaka leo hii na sijui wanaendeleaje.[emoji24]
Manka bado yupo kariakoo na anaendelea na biashara yake. Hata dukani kwake nimepigwa marufuku kwenda.
Mpaka leo hii siamini kama 500m imekwenda kizembe hivyo najiona mjinga na najipa moyo huenda ni ndoto.[emoji24][emoji24]
Daaah[emoji24][emoji24][emoji24] ndani ya muda mfupi maisha yamenigeukia namna hii.
[emoji24][emoji24][emoji24]nimeamua ku share humu kupunguza uchungu, sijamuambia yeyote. Ila huyo Mchagga kama yupo humu, akisoma atanijua.
Mchana mwema[emoji24][emoji24]