kwisha
JF-Expert Member
- Sep 9, 2021
- 1,793
- 5,042
Katika watu ambao walikuwa wabishi kuhusu uwepo wa Mungu mimi wa kwanza na nilikuwa na sababu zangu
Sababu hasa ilikuwa matatizo ambayo nilikuwa nayo:
Nilikuwa na matatizo ya ugonjwa wa ini. Niliteseka saana. Nilikwenda hospitali mbalimbali bila mafanikio yoyote yale. Nilikwenda kwenye Makanisa mbalimbali kutafuta msaada bila mafaniko nilikwenda kwa waganga wa asili bila mafanikio.
Familia na ndugu zangu walikuwa wanasubiri tu siku nitoweke duniani. Na mimi nilikuwa nimeshakata tamaa ya kuishi kabisa maana. Tumbo ilikuwa imeanza kujaa maji na miguu kuvimba.
Kuna siku ilikuwa mchana nilikuwa nimepumzika ndani. Sijui nini kilitokea mpaka sasa hivi sijuagi kama nilikuwa nipo kwenye ndoto au nilikuwa vipi. Nilijikuta nimechukuliwa mpaka makaburini na mzee mmoja ambaye huyo mzee alikuwa tayari ameshakufa alikuwa naishi mtaani kwetu pale. Ndo nilijikuta nipo naye akawa ananiambia unajua dawa ya ugonjwa wako ni nini.
Nikajibu sijui mzee wangu nateseka saana na ugonjwa huu mimi ni wakufa tu akajibu apana wewe sio wakufa
Dawa ya ugonjwa wako ni jiwe ili akanipa jiwe fulani hivi jeusi akaniambia nimeze jiwe ilo nitapona. Nilimeza jiwe hilo halafu baada ya hapo nikajikuta nimeamka.
Kufika jioni nilianza kutapika damu kuharisha damu walinikimbizi hospitalini watu walikuwa wameanza kulia nyumbani kwetu maana walijua mwisho wangu umefika. Nilipelekwa huko hospitalini. Nilifanya siku 4 sijui mchana ni upi au usiku ni upi nilikuwa nimezimia.
Madokta nao walikuwa wanasubiri moyo usimame tu maana wazee wangu walikuwa hawana pesa za matibabu ambayo walikuwa wanaomba. Baada ya wiki hali yangu ilianza kurudi polepole mpaka nikapona kabisa. Sasa hivi mimi ni mzima wa afya kabisa.
Ila mpaka sasa hivi najiulizaga maswali mengi kuhusu ndoto hile yule alikuwa Mungu alikuja kwa sura ya yule mzee au ni mambo tu wazee wetu.
Sababu hasa ilikuwa matatizo ambayo nilikuwa nayo:
Nilikuwa na matatizo ya ugonjwa wa ini. Niliteseka saana. Nilikwenda hospitali mbalimbali bila mafanikio yoyote yale. Nilikwenda kwenye Makanisa mbalimbali kutafuta msaada bila mafaniko nilikwenda kwa waganga wa asili bila mafanikio.
Familia na ndugu zangu walikuwa wanasubiri tu siku nitoweke duniani. Na mimi nilikuwa nimeshakata tamaa ya kuishi kabisa maana. Tumbo ilikuwa imeanza kujaa maji na miguu kuvimba.
Kuna siku ilikuwa mchana nilikuwa nimepumzika ndani. Sijui nini kilitokea mpaka sasa hivi sijuagi kama nilikuwa nipo kwenye ndoto au nilikuwa vipi. Nilijikuta nimechukuliwa mpaka makaburini na mzee mmoja ambaye huyo mzee alikuwa tayari ameshakufa alikuwa naishi mtaani kwetu pale. Ndo nilijikuta nipo naye akawa ananiambia unajua dawa ya ugonjwa wako ni nini.
Nikajibu sijui mzee wangu nateseka saana na ugonjwa huu mimi ni wakufa tu akajibu apana wewe sio wakufa
Dawa ya ugonjwa wako ni jiwe ili akanipa jiwe fulani hivi jeusi akaniambia nimeze jiwe ilo nitapona. Nilimeza jiwe hilo halafu baada ya hapo nikajikuta nimeamka.
Kufika jioni nilianza kutapika damu kuharisha damu walinikimbizi hospitalini watu walikuwa wameanza kulia nyumbani kwetu maana walijua mwisho wangu umefika. Nilipelekwa huko hospitalini. Nilifanya siku 4 sijui mchana ni upi au usiku ni upi nilikuwa nimezimia.
Madokta nao walikuwa wanasubiri moyo usimame tu maana wazee wangu walikuwa hawana pesa za matibabu ambayo walikuwa wanaomba. Baada ya wiki hali yangu ilianza kurudi polepole mpaka nikapona kabisa. Sasa hivi mimi ni mzima wa afya kabisa.
Ila mpaka sasa hivi najiulizaga maswali mengi kuhusu ndoto hile yule alikuwa Mungu alikuja kwa sura ya yule mzee au ni mambo tu wazee wetu.