giningi asilia
Member
- Sep 17, 2013
- 12
- 4
Kaka kwanza pole sana!
Unapitia kipindi kigumu. Katika maisha unapokuwa umempenda mtu na kujitoa kwa kila kitu juu yake na kisha mtu huyo akafanya mambo ambayo unaona ni tofauti ni lazima nafsi yako itaumia. Jambo ninaloliona kwako ni hili; inawezekana mwanamke huyo hakuwa amekupenda tangu mwanzo. Mtu huyo alikubali kuwa na wewe na kukuonyesha kuwa anakupenda kutokana na hali yake ya kimaisha na wewe ulimpenda kutokana na unyonge wake na kujitolea kila kitu. Hili si jambo baya-kumpenda mtu na kumsaidia. Lakini, kwa upande mwingine upo uwezekano kuwa mwanamke huyo alikupenda kweli ila kama unavyojua hulka za binadamu za kubadilika; mazingira ya kufanikiwa na uwezo wa kifedha na matamanio yamemfanya abadilike; upo uwezekano anakuona humvutii tena kuwa kuna watu kwa mtazamo wake anawaona wanamfaa kuliko yeye na amekuchoka. Mapenzi yameonesha tabia hiyo kihistoria, unaweza ukapendana na mtu leo, mkapendana kwa kiasi kikubwa kiasi cha kwamba mkaona hamuwezi kuachana daima, lakini inatokea bila kujua wala kupenda mnachokana au mmoja anamchoka mwenzake. Aidha, inaweza ikawa ni ulimbukeni, kuna watu huwa hawakui anabadilika miaka tu lakini akili za kishamba; na anajikuta anachezewa na kila mtu kirahisi.
Uamuzi wa kuachana nae si mbaya ila usiufanye kwa hasira, wala usiumize kichwa kufikiria gharama ulizotumia; haya ndiyo maisha, na hizo ndio changamoto.Tulia, mshukuru MUNGU kuwa uhai. Ongea naye kwa utulivu mwambie kwa namna mnavyoenda unaona ni vyema mkatengana kwa amani hiii ni kwaajili ya afya yako. Fanya mambo yako na bado naamini utampata mtu mwingine wa kuishi naye kwa amani. Kuhusu watoto pangeni utaratibu.
Kaka katika maisha tumezaliwa watupu tutaondoka watupu; nakuhakikishia kuwa hata siku yakufa huwezi kuzikwa na mtoto wala hela wala mali ulizozichuma so the game is kupata na kupoteza ulimpata, ukampenda mapenzi yameisha, iruhusu nafsi yako kukubaliana na hali halisi.
GININGI
Unapitia kipindi kigumu. Katika maisha unapokuwa umempenda mtu na kujitoa kwa kila kitu juu yake na kisha mtu huyo akafanya mambo ambayo unaona ni tofauti ni lazima nafsi yako itaumia. Jambo ninaloliona kwako ni hili; inawezekana mwanamke huyo hakuwa amekupenda tangu mwanzo. Mtu huyo alikubali kuwa na wewe na kukuonyesha kuwa anakupenda kutokana na hali yake ya kimaisha na wewe ulimpenda kutokana na unyonge wake na kujitolea kila kitu. Hili si jambo baya-kumpenda mtu na kumsaidia. Lakini, kwa upande mwingine upo uwezekano kuwa mwanamke huyo alikupenda kweli ila kama unavyojua hulka za binadamu za kubadilika; mazingira ya kufanikiwa na uwezo wa kifedha na matamanio yamemfanya abadilike; upo uwezekano anakuona humvutii tena kuwa kuna watu kwa mtazamo wake anawaona wanamfaa kuliko yeye na amekuchoka. Mapenzi yameonesha tabia hiyo kihistoria, unaweza ukapendana na mtu leo, mkapendana kwa kiasi kikubwa kiasi cha kwamba mkaona hamuwezi kuachana daima, lakini inatokea bila kujua wala kupenda mnachokana au mmoja anamchoka mwenzake. Aidha, inaweza ikawa ni ulimbukeni, kuna watu huwa hawakui anabadilika miaka tu lakini akili za kishamba; na anajikuta anachezewa na kila mtu kirahisi.
Uamuzi wa kuachana nae si mbaya ila usiufanye kwa hasira, wala usiumize kichwa kufikiria gharama ulizotumia; haya ndiyo maisha, na hizo ndio changamoto.Tulia, mshukuru MUNGU kuwa uhai. Ongea naye kwa utulivu mwambie kwa namna mnavyoenda unaona ni vyema mkatengana kwa amani hiii ni kwaajili ya afya yako. Fanya mambo yako na bado naamini utampata mtu mwingine wa kuishi naye kwa amani. Kuhusu watoto pangeni utaratibu.
Kaka katika maisha tumezaliwa watupu tutaondoka watupu; nakuhakikishia kuwa hata siku yakufa huwezi kuzikwa na mtoto wala hela wala mali ulizozichuma so the game is kupata na kupoteza ulimpata, ukampenda mapenzi yameisha, iruhusu nafsi yako kukubaliana na hali halisi.
GININGI