abbas-hassan
Member
- Nov 21, 2013
- 11
- 15
- Thread starter
- #61
Kipindi kigumu sana hiki
Kipindi kigumu sana hiki
lara 1 unaufahamu wimbo mmoja sikumbuki jina la kwaya ila wanasema
........watoto wa nyumba zote njooni tuungane
tuwalilie wazazi chozi la damu...........
haki ya malezi bora tumepoteza
urithi wa maadili tumepotezaa
ooh duniaaa dunia ooh tumekusea nini
beti ya 3 anasema
..............familia moja baba na mama watano...........
its a sad thing.
Mmmmmmmmh! *Covers face from shame!*
Huyo dawa yake wala si kukibia na kumuachia jiji ajitanue! Dawa yake ndogo sanaaa! We tafuta nyumba ndogo hapo hapo jirani utiize ule usemi ULIKIONA CHA NINI, WENZIO WASEMA WATAKIPATA LINI? Atanyooka kama nguo mbichi iliyopigwa pasi!
I realy do feel mercy for the kids! Wataisoma namba, chezea baba wa kambo na mama wa kambo!
abbas-hassan yaani ulivyoongea tu hapo, ninakufahamu, ulimsomesha chuo kikuu, unakaa jetrumo dsm, yeye anafanya kazi afisa mambo ya elimu, anasafiri sana mikoani, wewe ulikuwa unafanya kazi zamani katika ubalozi fulani hivi hapa dsm, uliachishwa kazi, na una kisukari, dada ana hela za kutosha tu na mmejenga nyumba yenu nzuri sana huko jet. yeye mtu wa iringa, wewe ni mngoni. hadi nakuonea huruma.
kumfumania mwanamke mara 7 yahitaji ujasiri. mwombe Mungu usiingie majaribuni ukaja kujutia maisha yako yaliyobaki, usichukue uamuzi mbaya kwani utakugarimu.
Wadau nawaelewa sana. Ujue mpaka sasa akili imestack....sijui pa kwenda....sijui cha kufanya. Na roho ya mauti inaniwinda sana....bora nife...nyingine nenda hata Lindi ukaanze upya. Mara. ..we vumilia tu kidogo umuone ujinga wake.....kila jaribu lina mlango wake....kwamba soon nitapata ahuheni nitaondoka kuendelea na mambo yangu upya. Kama ni watoto ipo siku wakitaka kumjua baba yao watanitafuta.
Maskini watoto wanguuuuuu........Mungu waupushe na mabaya yote. Sikua na nia mbaya na huyu mwanamke. Kwa wema wote niliotenda mpaka kumtafutia kazi leo naonekana mburula.....ananidharau na kunijibu kunya??..NSSF nilimpa zaidi ya 80% ili afungulie biashara zake. Leo sina kazi ananiona mjinga kweli.........nipeni bastola wadau....nipeni tafadhali. Pls
kwanin ndoa nying (sio zote) ndugu walizotia mdomo huwa znakuja kuwa mbaya.......? Usiachane na mkeo, tengana nae. Mpe muda na jipe muda wa kujitathmini.
kwa hiyo akimbie nyumba kisa mwanamke?
hayajakukuta wewe!!
Kisa mwanamke....! Yes kisa mwanamke...unataka afanye nini analea nini hapa kama si kuendelea kunyanyasika tu. Kaka tafuta room 2 sehemu tulia huko weka vizuri mipango yako tengeneza bond nzuri na wanao kama ni wakubwa waeleze kila kitu....achana na huyo limbukeni atakuambukiza ukimwi bure
Wana jf....mi nimeoa na nina watoto wa3. Huyu binti nilimtoa kwao nikawaahidi wazazi wake kua nitamsomesha mpaka elimu yeyote. Nikafanya hivyo mpaka sasa yupo na kazi. Ila kwa bahati mbaya mimi karibu mwaka sasa sina kazi ila pesa za kula hazinikosi.
Huyu binti wakati naenda kumtambulisha kwetu alinifanya nikosane na ndugu zangu wote. Lakin kwa kua nampenda nilisimamia show mpaka wakanielewa. Maisha yetu mimi na yeye yamekua ya magomvi sana kwa takriban miaka 7 sasa. Hakuna tulichofanya cha mafanikio mpaka muda huu.
Magomvi yetu mengi yamekua ni tabia za unafki,uzinzi,uongo,dharau,majibu mabaya ya kutia hasira na kutojali wala kumthamini mtu. Ni mzuri sana wa kuomba msamaha ambapo baada ya kuomba msamaha hurudia kitu kile kile alichofanya baada ya muda mfupi.
Sasa maisha yamebadilika sana....baada ya yeye kua na kibiashara ambacho kinamuingizia pesa licha ya anazopata kwenye mshahara. Unachomweleza hakusikii hata kidogo. Anajifanya yeye ndio yeye...misheni town...kugawa namba ovyo kwa wanamme...kua na namba tofautitofauti ambazo hata mimi sizijui ambazo huzitumia kuwasiliana na wanamme zake wa nje.
Kiukweli mpaka time hii....nimewahi kumfuma akicheat zaidi ya mara 7. Akiwasiliana na wanamme wapya au ma X zake. Ni mtu wa iringa. Anakiburi sana na dharau ya hali ya juu. Hajali kama tunawatoto au la.
Hutoa majibu ambayo hunifanya nipate hasira sana na ikafikia mahala nikampiga kama mara 3 ivi. Na jana ilikua mara ya nne. So nimefikiria sana na nimeona ngoja nikimbie mji nimwachie kila kitu niende ninakokujua.
Kwa hasira nilizokua nazo jana....nimemwambia...hata akisikia nimekufa...asije kuniona...wala mimi sitakuja kumuona. Koz kama ni kunipotezea muda kanipotezea muda mwingi sana na gharama nyingi sana. Lakin zaidi ya yote ni kuhusu watoto wangu ambao sikutaka kabisa waishi ktk malezi mabovu kwasababu yake.
Nawashauri wanawake wenye tabia hizi waache. Malipo ni hapa hapa. Mtu akikutoa ujinga usimdharau.