KipimaPembe
JF-Expert Member
- Aug 5, 2007
- 1,285
- 699
Wadau nawaelewa sana. Ujue mpaka sasa akili imestack....sijui pa kwenda....sijui cha kufanya. Na roho ya mauti inaniwinda sana....bora nife...nyingine nenda hata Lindi ukaanze upya. Mara. ..we vumilia tu kidogo umuone ujinga wake.....kila jaribu lina mlango wake....kwamba soon nitapata ahuheni nitaondoka kuendelea na mambo yangu upya. Kama ni watoto ipo siku wakitaka kumjua baba yao watanitafuta.
Maskini watoto wanguuuuuu........Mungu waupushe na mabaya yote. Sikua na nia mbaya na huyu mwanamke. Kwa wema wote niliotenda mpaka kumtafutia kazi leo naonekana mburula.....ananidharau na kunijibu kunya??..NSSF nilimpa zaidi ya 80% ili afungulie biashara zake. Leo sina kazi ananiona mjinga kweli.........nipeni bastola wadau....nipeni tafadhali. Pls
Inahitaji ujasiri wa hali ya juu kuyashinda haya. Inaonekana wewe ni jasiri sababu ulioa bila kusikiliza ushauri wa ndugu. Mie nilifanya hivyo hivyo na yalinikuta kama yalivyokukuta wewe. Ila sasa hivi nimeshinda, simuhitaji tena kwa lolote. Ila siri ni lazima mtengane nyumba au vyumba. Mie sababu ya watoto nilitengana naye vyumba tunaendela kuchangia nyumba. Sasa hivi hata nimuone live na mwanaume mwingine sijisikii chochote, yaani sina emotion tena. Yeye ndo baadhi ya siku hunichokoza kwa visa vya kijinga jinga, ila namkacha tu kiaina. Hata watoto hawajastukia sana ila wanajua tunaishi vyumba tofauti. Ila mie vile vile naamini kuhama nyumba ni bora. Ila kwa changamoto za kiuchumi ulizo nazo kuhama nyumba inaweza kuwa ngumu kwako. Ila kama una mahala pengine pa kwenda, kuhama nyumba ni bora kuliko hayo unayoyafikiria. Kwa wanawake wanaume tunapoteza vingi. Hiyo mikwanja na misaada uliyompa we sahau. songa mbele!