Nakaribia kudhulumiwa, naombeni ushauri

Taratibu za kumtoa mpangaji ni zilezile wala hazina tofauti shirikisha uongozi wa mtaa mpe notisi ahame ndani ya miezi mitatu ikiisha miez mitatu toa vitu vyake nje.

Kama una nia ya kuendelea kudai hela yako kamfungulie kesi ya madai mahakamani, mahakama itatoa summons ataenda na utapata haki yako.
 
Hakuna lolote, hajayatimba, hao jamaa umiwashitaki kikosini wanakatwa pesa kwa nguvu.
 
Umeanza vizuri halafu ukapuyanga mwishoni [emoji2].

Mkuu, sisi wengine huwa hatupendi kutumia vyeo vyetu, kwasababu kama nikiamua kutumia mamlaka niliyonayo naweza kuathiri hata kibarua cha huyu bwana mdogo.

Na ndio maana hata nikienda kambini kwake siwezi kujitambulisha mimi na nani, nitaenda kama mwenye nyumba wa kawaida tu tena mkulima wa nyanya kule Lushoto [emoji1].

Mimi nimelelewa vizuri na namwamini Mungu. Ndio maana niko tayari hata kumsamehe kwasababu pesa inatafutwa, kama niliweza kujenga kwa jasho langu; hiyo milioni moja pointi kdg haiwezi kuniathiri kwa chochote.
 
Ni typing error tu, lengo ni jina /madai.
Kwa mwajiri wake ni rahisi zaidi kupata msaada. Wanasikiliza malalamiko ya raia dhidi ya askari wao.

Polisi ni kisheria zaidi, lakini itawalazimu kuomba ushirikianao wa mwajiri wake.
Its your choice mkuu.
Ooh nimeelewa mkuu. Pole kwa kuteleza.

Nitafanya kama ulivyoshauri.

Kwasababu sina uhakika na kambi yake basi nitaanzia Lugalo nione kama wanaweza kunisaidia.
 
Dah mkuu ASANTE sana. Umenifungua pakubwa.

Kesho mapema tu ntakuwa pale na ntaleta mrejesho humu.
 
Nashukuru sana mkuu.
 
Migogoro ya ardhi likiwemo hilo la kodi hayapokelewi polisi kwa sababu hiyo sio jinai bali ni shauri la madai hivyo apeleke shauri lake baraza la ardhi na nyumba la wilaya.
 
Yes.
Kweli Maisha magumu, kama umempangisha nyumba mzima anaweza kutengeneza documents akampiga hiyo nyumba
 
Hawa watu wanaitwa askari si watu wa kufanya nao ukaribu hata kidogo, kama ni urafiki uwe wa kupeana tu salamu barabarani ila kuwaingiza kwenye maisha yako binafsi hasa ya kifedha utaishia kulia
 
Nenda hapo Upanga kama ulivyoshauriwa ukiwa na kopi ya nyaraka zote muhimu zitakazokusaidia ktk mdai yako, muhimu majina yake matatu,hao wanaokushauri umsubiri arudi vp kama anajiandaa kwenda zake nje ya nchi kwamwaka mzima.
Pia naomba kuuliza je haishi nafamilia ambayo ingekusaidia kujua kambi yake
 
Acha kutisha watu wewe kayatimba yap sheria zipo Na haki itapatikana muhimu yeye kujua cha kufanya akiwa na ushahidi,

Watu kama wewe ndio manaochangia usumbufu kama huu kisa vyeo vyenu
 
Kama hutaki mambo mengi sijui mahakamani ,sijui polisi n.k ...

fanya hivi...

Nenda kwa mjumbe mwambie humtaki huyo mpangaji kwako na sababu ni hii.

hapo atapewa mwezi mmoja au siku kadhaa kama week 2 hivi za kuhama na atahama na

Ikibidi kabisa mtishie huyo mpangaji kwamba utaenda kazini kwake kushitaki kama atagoma kuhama. yaani asipohama huyo labda sijui..
 
Mkuu watu kama hao uwa wanajiandaa kusumbuana usikute ni mhaya au mnyaki wewe ukienda kwa mjumbe yeye anaenda baraza la ardhi na nyumba na mauongo kibao na hakuna sehemu yenye urasimu kama huko jambo dogo tu ambalo lingeweza kuisha kwa wiki au wiki mbili linachukua miaka mitano na hata ukija kushinda aambiwe akulipe fidia hana chochote cha kukulipa labda ungesema dawa ya wajinga kama hao ni kuwaroga tu kama kweli huo uchawi upo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…