Najuta kutupa pesa yangu VETA

Najuta kutupa pesa yangu VETA

Ni upotezaji mkubwa sana wa muda kwenda veta.

huwa wanatoka weupe. yaani hakuna wanachokijua. zaidi utaambiwa tu hiki kinaitwa hivi hiki kinaitwa vile.
Elimu ya tz ni ya kutafta chet tu maaa gata waajiri wa serikal wanatafta watu wenye vyet na sio ujuzi... Mtu ana cpa unamkuta kwenye mapokezi TRA
 
Sijaona upungufu wa VETA mpaka sasa... kwamba wanafundisha theory? Yes wanafundisha theory, ila ambacho ungetakiwa kufanya ni kuingia kitaa kupata uzoefu sambamba na elimu ya theory... na ndivo elimu ya bongo inatakiwa iwe..

Theory plus practical, kama practical hawatoi VETA kwa mapungufu yao, wewe inatakiwa ujiongeze ukaitafute practical kitaani
Kwahyo manake ukilipa ada percent flan unaibiwa
 
Udsm wanatoa digrii ya muziki.. ila hao wahitimu. Hawajui kuimba na wala hawajui hata kupiga chombo chochote cha muziki.

Walimu wao nao hivyo hivyo
Unaenda kukah chuo miak mitatu unasomea mziki na hujui mziki kuimba

Juz nilisafiri kwa Kaz zangu za udr kwenda kiteto Kuna bint Yuko home pale alimaliza udsm Sasa koz alichosoma Ni ujinga mtupu sijui literature

Bab ake akasema huyu mtot hakushaurikia kwani aliona Ni Bora kuacha kusoma Ila ilimradi tu akosome udsm degree yoyote

Leo Yuko anajifunza ufund cherehani

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Unaenda kukah chuo miak mitatu unasomea mziki na hujui mziki kuimba

Juz nilisafiri kwa Kaz zangu za udr kwenda kiteto Kuna bint Yuko home pale alimaliza udsm Sasa koz alichosoma Ni ujinga mtupu sijui literature

Bab ake akasema huyu mtot hakushaurikia kwani aliona Ni Bora kuacha kusoma Ila ilimradi tu akosome udsm degree yoyote

Leo Yuko anajifunza ufund cherehani

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Literature?
Angejua hata nusu ya jinsi ya kuongea kama Peter Drury angepiga hela
 
Kabla sijaenda niliomba ushauri kwanza wengine wakaniambia niende maana mafundi wa mtaani wengi ni wachoyo kukupa siri zote za kazi, na wengine wakaniambia nisiende maana hiyo pesa ya ada robo tu unapata fundi anakufundisha vizuri tu.

Llakini nikaona ni bora tu niende veta ila nilichokikuta huko ndugu yangu sikushauri na wewe uende.

Nilienda kusomea ufundi simu hardwire na softwire lakini mpaka namaliza sijui hata kutoa port ya kuchajishia simu, nimekuja kujifunzia huku mtaani na nimejua.

Kule ni kwenda tu kujua majina ya component na matatizo ya simu
Ni veta za serikali lakini.
Jilaumu mwenyewe kwa kuwa kilaza, usiwasingizie Veta...
 
Watu mnavokomment humu kama sio nyie vile. Eti kajifunze mtaani,,,, tukiwafata huuko mtaan mnatuzarau sana/mnatupandishia vioo sana sie tunaoomba kujifunza. Watanzania wanafiki sana.

Utaskia ooooh msimu huu hakuna wateja subir mwakan,, mara oooh mimi hapa sipokei wanafunzi na sababu lukuki.

Unakuja kwa madereva sasa hawa ndio balaa. Nishaongeaga na madereva wa malori,,, kila unaeongea nae anakwambia ntakuunganisha na jamaa fulan mara hapokei smu zako mara nn yaan sababu lukuki.

Penye uzia penyeza rupia

#MaendeleoHayanaChama
 
Hard
Kabla sijaenda niliomba ushauri kwanza wengine wakaniambia niende maana mafundi wa mtaani wengi ni wachoyo kukupa siri zote za kazi, na wengine wakaniambia nisiende maana hiyo pesa ya ada robo tu unapata fundi anakufundisha vizuri tu.

Llakini nikaona ni bora tu niende veta ila nilichokikuta huko ndugu yangu sikushauri na wewe uende.

Nilienda kusomea ufundi simu hardwire na softwire lakini mpaka namaliza sijui hata kutoa port ya kuchajishia simu, nimekuja kujifunzia huku mtaani na nimejua.

Kule ni kwenda tu kujua majina ya component na matatizo ya simu
Ni veta za serikali lakini.
Hardwire = Hardware, Softwire = Software. Pia upite kwa Ras Simba au British Council... inaonekana Roho yako i radhi ila hicho kiingereza ndo dhaifu.
 
Inawezekana maselemala wengi waliojaa mitaani na kazi zao ni mbovu wametokea huko pia
 
Nadhani lengo la mtoa mada ni kutaka kuichafua VETA.

Mimi nimesoma kozi hiyo na nimetoka vizuri.

Wakati tunaanza tuliambiwa tuwe na mazoea ya kwenda kwa mafundi simu ili kupata uzoefu. Pia huwa wanasisitiza wanafunzi kwenda na simu mbovu kutoka mitaani ili kuzitengeneza na kupata uzoefu.



Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Hujapoteza muda..

huyo anayebadilisha transitor ukimuuliza kazi ya transitor ni nini au transformer nini anaweza asijue, ni vizuri kujua theory na basic ya kitu chochote kwenye ufundi.

Shule ya ufundi haikufundisha kufanya kazi au kuwa competent kwenye kazi bali inakupa uelewa na practical utakwenda kuikuta mtaani..

Mafundi wengi mtaani wa magari ni wazuri sana wa kufungua funga aka fixing na kusolve matatizo waliyoyakalili lakini wengi wao hawana technical knowhow..

Ndio maana ukiwa na European car inashida ya kutumia akili utapata shida sana kupata fundi Tanzania maana wengi wamekariri gari za kijapan...lakini fundi mwenye good technical knowhow na practical skills anaweza kutengeneza gari yeyote duniani kwa kusoma mfumo..
 
Back
Top Bottom