Chotara wanapagaisha wengiMkuu , rangi ya chotara ilikuchanganya....pole sana , uvumilivu wako na kutofanya maamuzi magumu mapema vimekuponza
Waheshimiwa habari za mida,
Mimi ni IT specialist kwenye shirika moja lisilo la kiserikali mshahara wangu ni wa kati si mkubwa sana wala si mdogo sana. Lakini pia mimi ni lecturer part time nafundisha jioni wafanyakazi katika chuo kimoja hapa DSM, Nimeoa na nina watoto wawili, huyu mke wangu ni chotara wa Kiarabu.
Wakati tumeanza kudate hakuniambia kama ana mtoto na kwa kweli alivyo mzuri sikutilia shaka kama ana mtoto maana hata nyonyo zake zilikua zimesimama kama mtoto anaebalehe.Baadae mapenzi yaliponoga ndipo akaniambia kuwa ana mtoto alie darasa la kwanza yupo kwa mama mzazi yaani bibi wa mtoto.
Kwa kuwa nilikua tayari nimezama kwenye mahaba mazito ikabidi nikubali tu maana by that time nilishatangaza ndoa ilikua ni point of no return. Ila mchumba alinihakikishia kuwa mtoto wake hatakua kikwazo kwenye ndoa yetu na kwamba huduma zote za malezi ikiwa ni pamoja na shule, malazi, maradhi na mengineyo yatakua chini ya baba wa mtoto.
Huo ndio ukawa mkataba wetu na kwamba mtoto ataishi kwa bibi na baadae atahamia kwa baba mzazi ambae ni Mwarabu mwenzie. Akabadli dini kuja ukristo tukafunga ndoa haikua shida maana mama ake pia ni mkristo baba ndio muislam na aliwatelekeza siku nyingi.
Miezi sita baada ya ndoa akamleta mtoto kwetu kuishi permanent kinyume na mkataba wetu, anyway nikawa na roho ya utu nikasema haina shida kuepusha shari. Mtoto wake alipofika darasa la nne wakampeleka boarding sisi hapo tuna watoto wawili mapacha wa miaka minne kasoro nadhani mimi ndie nililipa ada ya boarding.
Siku moja katikati ya wiki nilibeba mahitaji kadhaa nikampelekea yule mtoto shuleni, niliomba wakaniruhusu kuingia pale Surprisingly Matron akaniambia huyo mtoto mbona ana vitu vya kutosha. Mama yake na baba yake walikua hapa juzi siku tano hivi zimepita. Akaniuliza kwani wewe ni nani wa mtoto nikamweleza, akashangaa akaniambia mbona walikua wamekaa na mtoto kama ni familia inayoishi pamoja.
Akanipa kama umbea flani hivi nilishangaa kwa kuwa mke wangu hakuniambia kama alienda kwa mtoto na mzazi mwenzie alikuwepo. Visiting day moja nikaenda na watoto wangu kumuona mwenzao, mke wangu aliondoka mapema akatangulia tulipofika pale tukakuta jamaa nae yupo wamekaa na mtoto na wife.
Mshikaji akaaga bila kunisalimia akaondoka zake nilishindwa kumwelewa, nikazuga tukaendelea na mengine hatimae yule mtoto akamaliza la saba. Mama yake akamtafutia shule nzuri sana yenye matokeo mazuri kila mwaka kimbembe kikaja kwenye ada, mimi nikamwambia mwisho wangu ilikua ni la saba.
Sasa walipe wenyewe maana watoto wangu pia wameanza shule ya Mapadre Lieberman ada wote wawili ni million sita kwa mwaka bado nina mdogo wangu wa kike anasoma chuo nalipa mimi ingawa ana mkopo asilimia ishirini. Bado gharama za uendeshaji familia za kila siku, hivyo nikamwambia sitaweza kulipa, ni vema babaake ajipange kulipa.
Wakuu kwa kauli yangu hiyo ulizuka mgogoro mkubwa, Huduma zote muhimu nilisitishiwa pamoja na za chumbani akaondoka akarudi kwao kwa mwezi mzima baada ya kusuluhishwa akarudi mimi nikashikilia msimamo kuwa silipi ada.
Hivi karibuni wakati hayupo nimeingia kwenye mapenzi na mdada jirani yangu amepanga upande anaishi na ndugu, wife amerudi sina hamu nae tena. Huyu mdada jirani nimekua nikimpa lift asubuhi kwa muda mrefu sasa na ndipo tukaelewana na anajua matatizo yetu, alikua akitusaidia sana nyumbani wakati wife ameondoka.
Nimedhamiria kumuacha wife mazima nimeshachoka, juzi baba amekuja akaniambia nilikushangaa ulipojifanya mjuaji kuoa mwanamke mwenye mtoto tukakuzuia ukalazimisha sasa umeyaona.
Wakuu nipo njia panda, ushauri tafadhali
Pole mkuu.ilikuaje??Bro nimejifunza kuwa ktk mahusiano na mwanamke mwenye mtoto. Yaneshanikuta hapa sina hamu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Pia kasema kusaidiwa hapa nyumbani, hajataka matumiziMkuu yeye ndiye anayempa lift huyo mrembo.
Mkuu mwanamke mjane ni Yule aliye pewa talaka na mumewe au nasema uongo ndugu zanguniUSHAURI WA BURE NA WA KWELI: Usioe single mother, isopokuwa awe amefiwa na x - mume wake, la sivyo utakuja kufa bure.
Narudia tena OA MWANAMKE AMBAYE SIO SINGLE MOTHER, isipokuwa awe mjane.
Sent using Jamii Forums mobile app
baba amekuja akaniambia nilikushangaa ulipojifanya mjuaji kuoa mwanamke mwenye mtoto tukakuzuia ukalazimisha sasa umeyaona.
Wakuu nipo njia panda, ushauri tafadhali
Kwa kweli kwa jeuri hio ya baba mzaziPole sana mkuu kwa majanga,
Hapo obviously ni kuwa jamaa mwenye mtoto anakugongea wife wako..maana kama wana uwezo wa kwenda pamoja shule kwa mtoto ina maana wanakwenda na sehemu nyingine pasi na wewe kujua..mtoto kwao ndo kiunganishi
Halafu mkuu, ujue hizi races nyingine tunaishi nao lakini ubaguzi wao haujaisha 100%...hawa waarabu na wadosi wakikutana wao kwa wao something is apt to happen..so kama we ni mdengereko pure na umeoa half-caste wa kiarabu na amezaa na muarabu mwenzake basi ndugu andika maumivu
Halafu cheki walivyo na dharau..yaani aliondoka bila kukusalimia pale skuli wakati we ndo unamsomeshea mtoto..unajua alikuwa anakupa ujumbe gani?..."you just spoilt my romantic reunion with mzazi mwenzangu, you silly SOB!!!" ndicho alichokisema moyoni
Umeshauri utumbo mkuu,,,,sorryKaeni kikao na wazazi wenzako wote watatu (pamoja na baba wa mtoto) mjaribu kupata solution
Hasa wakikutana na Wasukuma! Hata huyu Jamaa anaonekana ni Msukuma ndiyo maana Chotara kamchezesha anavyotaka!!Chotara wanapagaisha wengi
Wasukuma na Vitu white ni Kama Mbwa na chatu! Mbwa lazima awe mpole na ajipeleke mwenyewe kwa Chatu japo kua anajua kabisa anaenda kuliwa!!mkuu achana na huyo mwanamke jamaake bado anamtomba kwa mgongo wako , yan we ulipe gharama jamaa ale bure ? sio kweli mkuu...YAN KIMBIA