Najuta kuoa mwanamke mlokole

Najuta kuoa mwanamke mlokole

Kwa upande mmoja mkeo hana kosa kwani inaonekana wewe mlikuwa mnasali pamoja huko kanisani na huenda mkaoana mkiwa huko huko..hivyo yeye na wazazi wake walifahamu fika kuwa umekubali kumuoa huku ukiwa unajua taratibu zote za kanisani na ratiba ilivyo.. ( Correct me if i am wrong).. baada ya wewe kuona hapana ukachomoka huko, unamlazimisha na yeye kufuata uamuzi wako kwa ghafla..my friend mambo ya imani kwa wanawake sijui yakoje..wakizama wamezama..tofauti na sisi wanaume..sasa changing her way just like that is aprocess..not an instant coffee...Alafu kweli mwanamke hapigwi bwana..You could perhaps find a better way of handling the situation..ukiona unataka kumpiga ondoka nenda mtaani hasira zitaisha unarudi zako...Pia hata kama hutaki kumuona ujue wewe ni baba,una jukumu la kumtunza mwanao hata bible inatuambia he who doesnt take care of his own is as bad as an infidel.. umekosana na mkeo kweli miezi miwili humuangalii mwanao?
 
pole kaka kuna makanisa mengine yana majanga hayo na imani kubadilisha inahitaji sijui nn khaa mm kuna dogo hua anaondoka kilasiku saa sita anarufi saa moja au mbili usiku tumesemaaaaa tumechoka tumemuacha tuu sasa ila mm hata mia yangu hapati afe tuu na ujobless wake.
 
narudia tena mwanaume kamili na anayejiamini hpigi mke. mambo ya kupigana ni ya kinyama na hata wanyama hawapigi wanawake zao.huwezi kumrekebisha mtu kwakumpiga.unaonaje ukimpiga alafu ukamtia ulemavu.
kuna siku nilikuwa namwambia mtu pombe haifai.akasema hapana bwana inafaa ila usizidishe tu. nikamwambia tatizo la pombe ni pale ambapo unatakiwa kusema inatosha sasa.
mke sio mtu wa chini kiasi hicho. mbona wewe ukikosea hupigwi. huo ni mfumo kikurya ambao personally naudharau sana. wanaoongoza kwa mauza uza kwenye mahusiano mengi ni wanaume. wengi wanajisifia kufanya uzinzi ni uanaume na hata wanapofumania kuomba msamaha kwa mke wako unaona ni kujishusha. huo ni ujinga, upumbavu, ulimbukeni na ushenzi. mwanaume anayejitambua hawezi kuunda familia ya kupigana pigana. pia mambo ya kupigana sio ya kistaarabu wala kiungwana.
pia mke sio mtoto wa kuchapwa kiboko. mke ni patner. ana haki sawa kama wewe. watu wanaopenda kupiga ujue walikuwa abused wakati wa utoto wao.tabia ya kupiga ni tabia ya kinyama. ukishidwa kumrekebisha kwa vikao ujue umevamia ubavu wa mwenzakona sio wako huyo. sifa ya mchungaji mwema ni sauti yake kusikilizwa na kondoo wake. ukiona kondoo wako hasikilizi sauti yako ujue wewe sio mchungaji na hao au huyo sio kondoo wako
pia nakuona kama unahitaji msaada wakisaikolojia kwenye hili. am sure maafisa ustawi wa jamii wanaweza kusaidia na wanasaikolojia kama una hasira mbaya na tabia ya kupigamke. mtu anayemdharirisha mkewekwa kupiga ana chance kubwa pia kuwa huwa anabaka mkewe. hatuwezi kuunda taifa la wapigaji na wabakaji. lazima tabia hii ikome kabisa na ninasema ukweli nikikuta mtu anapiga mkewe barabarani lazima na yeye apigwe tu, maana hakuna namna nyingine na nasema apigwe tu apigaye mkewe
Utatigha ghontoka murisya, "mfumo wa kikurya" ighake!!! hivi nchi hii kuna wanaume romantic kama wakurya?!
 
Umefanya maamuzi sahihi. Pole sana rudi kwa Rachel kama bado yuko available. Waswahili walisema Usiache mbachao kwa msala upitao. Ungeamua kumuoa Rachel wala usingepata maudhi kama haya toka kwa ex mkeo, wazazi wake na wengineo.

Miezi miwili iliyopita nilipelekwa polisi na wazazi wa mke wangu, kwa kosa la kumpiga binti yao karibu nimuue, ndugu walikuja kunitoa

Iko hivi;
Huyu binti nilimuoa miaka miwili iliyopita na tuna mtoto mmoja, yeye na wazazi wake wote wameokoka, Hivi sasa naweza kusema kwamba mke wangu ameolewa na kanisa na si mimi.

Akitoka kazini saa kumi na moja jioni anakwenda kwenye maombi kanisani hadi saa tatu , na hii ratiba ni kila siku Monday to Friday, Jumamosi pia wanakwenda Jumapili ni kutwa nzima, wakati mwingine kuna mkesha katikati ya wiki, hali hii, imefanya ashindwe hata kupataa muda wa kumlea mtoto wetu wa mwaka alielazimika kumwachisha ziwa akiwa na miezi mitatu kutokana kubanwa na mambo ya kanisa.

Mtoto huyu ni kama amebadilishiwa mama, maana sasa analelewa na house girl wetu kwa hali na Mali
Ilifika pahala nikashindwa kuvumilia hali hii na nikamuita na kumueleza hali halisi na kumtaka abadilishe ratiba zake, akadai kwamba hana jinsi kwa kua ratiba ya kanisa kwake haina substitute , nikamwambia ni amri sio ombi

Akaendelea hivyo hivyo, kwa Mara ya kwanza nilimpa kipigo kwa kukaidi amri yangu, niliendelea kumpiga mara kwa Mara sababu ikiwa ni kanisa, kila tunapoitwa kusuluhishwa wazazi wake humtetea na kudai walikosea kunipa mm binti yao, ikawa tunagombana na wazazi wake vikaoni hadi nikaamua kuachana na vikao.

Mwanzoni mwa mwezi wa sita alidai kuna mkesha wa maombi siku hiyo na hivyo atalala huko, nikamwambia ukitoka huko utafute nyumba nyingine, baadae mama yake akanipigia kwamba kuna mkesha hivyo wote watalala church kwenye mkesha, nikamjibu haiwezekani wamruhusu wife arudi kwa kuwa ana mtoto mdogo, akakata simu

Kweli, wife hakurudi, ila kila saa alikua akinipigia simu karibu usiku kucha nami sikua napokea naiangalia tu hadi inakatika hadi saa kumi alfajiri, alikuja amesindikizwa na dada yake maana walijua nimekasirika sana

Walipofika tu niliwakamata wote wawili na kuwapa kipigo kizito sana hadi wife kuzirai, dada mtu aliniponyoka na kukimbilia main road huku nikiwa nimemtengua mbavu akapanda boda boda, saa moja wazazi wa wife wakaja nilikua nimemfungia stoo wakamchukua wakaenda nae.

Baadae wakanifuata kazini na polisi wakaniweka ndani kwa shambulio la kudhuru mwili, nilitoka kesho yake , kesi ikahamia Ustawi wa Jamii tuliitwa pale, mbele ya wazee wa pande zote, ikaamriwa kwamba binti arudi kwa wazazi wake hadi hapo baadae hali ikiwa nzuri, ila wazazi wake wakasema wanamchukua kimoja hawanihitaji tena, kwamba nisubiri taratibu za talaka, nikasema haina shida nipo tayari, tukaja nyumbani wakamchukua mtoto na hg na nguo zake wakarudi kwao

Nimeyasahau hayo naishi kwa auheni kiasi kwa sasa Ingawa bado nina msongo, surprisingly Friday wife akanifuata kazini hatukua tumeonana for two months, roho yangu iliingia kitu flani hata mtoto wangu sikutaka hata kuwa naenda kumuona ingawa pale ustawi wa jamii niliruhusiwa

Wife akaniomba tuongee, akasema anahitaji turudiane, akadai anaomba arudi home kwangu hata kesho yake ikiwezekana, kwamba ananipenda, kwamba tutarekebisha tu, nikamwambia haiwezekani simtaki tena

Wadau wana Jf, nimemwambia atafute Mme mwingine kanisani kwao ndo watawezana na sio Mimi, mke wa hivi hanifai, hata mshahara wote anapeleka huko, hilo kanisa Jumapili moja tu kuna sadaka kama 12 hivi tangu asubuhi hadi jioni, unaweza kwenda na laki mbili usirudi hata na shilingi jioni, bado katikati ya wiki, halafu wachungaji wanaishi kifajari.

Huyo mchungaji wa hilo kanisa ameshawateka akili, mimi binafsi nilikua huko nikahama kutokana na hiyo biashara ya kutakiwa kushinda huko 24/7 na pia kutumia sehemu kubwa ya mapato yangu kanisani badala ya kujenga familia, kanisa gani wanaomba hadi salary slip? Na usipowapa watakusema sana kwamba umepotea njia na kadhalika
Kanisa gani halijali ndoa za watu?

Sio kwamba sipendi mke wangu aende kanisani, aende kwa kiasi na ratiba akizingatia kuwa yeye ni mama wa familia, inapaswa kwenda kanisani unashiriki na wenzako mchana au jioni unarudi home, jumatano unakwenda kwa maombi masaa mawili, six jioni unarudi kwako, there will be nothing wrong, lakini huwezi kwenda kushinda huko 24/7. Seven days a week, inakuja kweli hiyo?

Hata dada wa mke wangu niliempiga, mumewe pia alikuja kwangu na malalamiko kama haya ya kwangu, nimeamua simtaki tena, kwanza akili yangu imeshachanganyikiwa,
Nonsense

Ni bora nirudi kwa Rachel, alinivumilia tangu chuo hadi mtaani nikamtendea vibaya nikaoa mlokole nisiemjua, kwa kweli najuta sikujua nachofanya.
 
mwanaume kamili hapigi mke wala kulalamika. kama mtu anazingua unachukua njia yako. sioni hata haja ya kuwasema mabinti wa kilokole kwa sababu hukulazimishwa kuwa naye. kama na ameona mchungaji wake ni wa maana kuliko wewe chukua maamuzi magumu au mlowase. pia kuna ulokole na ugonjwa. ulokole hausemi mtu aharibu ndoa yake. hizo ni Imani za watu wasiojua wanachofanya. pia kisheria ukimuachisha mtoto maziwa kabla ya miezi sita unaharibu ubongo na kinga yake.
pia ungeenda kuongea na mchungaji wake. sio ustaarabu kupiga mke ambaye hulingani naye nguvu. pia hata wewe unaoneka una wenge jingi maana umempiga mke wako na kuja kumangaza hapa jf wakati yeye hawezi kujitetea. unapomsema mtu hakikisha naye yupo na anaweza kujitetea kama wewe. pia kwangu sioni tija ya ulichofanya hapa. mahusiano sio jela. mtu akizingua unajiachia kivyakooo
Usi mm judge kaka, ndio mwanaume kamili hapigi mkeo wala mwanamke, ila kumbuka huyu ni binadamu haja kamilika ana mapungufu yake,ndoa nishida sio kitu kidogo hakula zimishwa kuoa wala kua nae wamekutana wamependana ila mama hapo kazidisha kosa kubwa saana kuto kumsikiliza mumeo na hapo hakuna ulokole yani hio ni dhambi tosha tuh so kanisani huyo ana sindikiza bure tuh mume ndo kila kitu msikilize na umtii, huyo mwanamke anapata support kwao kashikwa ndo maana alikua ana jeuri hio, asaivi karudi kwao kaona shida zile za nyumbani anataka kurudi kwenye nyumba yake. haja mtangaza hapa tupo kushauriana ku share moja mbili tatu za matatizo sio mbaya kushauriana kama kutangaza ange andika jina la mkeo na familia, ndo kazi ya forum kuelezea hivi ni dawa tosha unaya toa yote ya moyoni usi mkatishe tamaa, ndoa ngumu jamani una kuta mtu hana tabia zakupigana au kulewa ila tangu haoe ndo unakuta mtu anakua mlevi wanawake stress nyinyiiiiiii
 
Mkuu i feel your pain pole saana ndo maisha hayo hakuna a perfect wife wala husband, ndoa zote zina ups and downs.
Kua mpole tuh kama kweli amekuja amekuomba msamaha sahau msamehe tuh mfikirie mwanao sio nzuri kwa mtoto anakulia kwa mama au baba leo aende kwa mama kesho kwa baba au awe na baba wa kambo au mama wa kambo inakua ina distract. hakirudi akikisha unasimama kwenye msimamo wako biashara ya church utaki na iwe final warning kwake na kweli ajue kosa lake na hajutie. ila mfikirie mwanao kwanza
 
pole mkuu....nimependa sehem yakutoa dozi
 
Miezi miwili iliyopita nilipelekwa polisi na wazazi wa mke wangu, kwa kosa la kumpiga binti yao karibu nimuue, ndugu walikuja kunitoa

Iko hivi;
Huyu binti nilimuoa miaka miwili iliyopita na tuna mtoto mmoja, yeye na wazazi wake wote wameokoka, Hivi sasa naweza kusema kwamba mke wangu ameolewa na kanisa na si mimi.

Akitoka kazini saa kumi na moja jioni anakwenda kwenye maombi kanisani hadi saa tatu , na hii ratiba ni kila siku Monday to Friday, Jumamosi pia wanakwenda Jumapili ni kutwa nzima, wakati mwingine kuna mkesha katikati ya wiki, hali hii, imefanya ashindwe hata kupataa muda wa kumlea mtoto wetu wa mwaka alielazimika kumwachisha ziwa akiwa na miezi mitatu kutokana kubanwa na mambo ya kanisa.

Mtoto huyu ni kama amebadilishiwa mama, maana sasa analelewa na house girl wetu kwa hali na Mali
Ilifika pahala nikashindwa kuvumilia hali hii na nikamuita na kumueleza hali halisi na kumtaka abadilishe ratiba zake, akadai kwamba hana jinsi kwa kua ratiba ya kanisa kwake haina substitute , nikamwambia ni amri sio ombi

Akaendelea hivyo hivyo, kwa Mara ya kwanza nilimpa kipigo kwa kukaidi amri yangu, niliendelea kumpiga mara kwa Mara sababu ikiwa ni kanisa, kila tunapoitwa kusuluhishwa wazazi wake humtetea na kudai walikosea kunipa mm binti yao, ikawa tunagombana na wazazi wake vikaoni hadi nikaamua kuachana na vikao.

Mwanzoni mwa mwezi wa sita alidai kuna mkesha wa maombi siku hiyo na hivyo atalala huko, nikamwambia ukitoka huko utafute nyumba nyingine, baadae mama yake akanipigia kwamba kuna mkesha hivyo wote watalala church kwenye mkesha, nikamjibu haiwezekani wamruhusu wife arudi kwa kuwa ana mtoto mdogo, akakata simu

Kweli, wife hakurudi, ila kila saa alikua akinipigia simu karibu usiku kucha nami sikua napokea naiangalia tu hadi inakatika hadi saa kumi alfajiri, alikuja amesindikizwa na dada yake maana walijua nimekasirika sana

Walipofika tu niliwakamata wote wawili na kuwapa kipigo kizito sana hadi wife kuzirai, dada mtu aliniponyoka na kukimbilia main road huku nikiwa nimemtengua mbavu akapanda boda boda, saa moja wazazi wa wife wakaja nilikua nimemfungia stoo wakamchukua wakaenda nae.

Baadae wakanifuata kazini na polisi wakaniweka ndani kwa shambulio la kudhuru mwili, nilitoka kesho yake , kesi ikahamia Ustawi wa Jamii tuliitwa pale, mbele ya wazee wa pande zote, ikaamriwa kwamba binti arudi kwa wazazi wake hadi hapo baadae hali ikiwa nzuri, ila wazazi wake wakasema wanamchukua kimoja hawanihitaji tena, kwamba nisubiri taratibu za talaka, nikasema haina shida nipo tayari, tukaja nyumbani wakamchukua mtoto na hg na nguo zake wakarudi kwao

Nimeyasahau hayo naishi kwa auheni kiasi kwa sasa Ingawa bado nina msongo, surprisingly Friday wife akanifuata kazini hatukua tumeonana for two months, roho yangu iliingia kitu flani hata mtoto wangu sikutaka hata kuwa naenda kumuona ingawa pale ustawi wa jamii niliruhusiwa

Wife akaniomba tuongee, akasema anahitaji turudiane, akadai anaomba arudi home kwangu hata kesho yake ikiwezekana, kwamba ananipenda, kwamba tutarekebisha tu, nikamwambia haiwezekani simtaki tena

Wadau wana Jf, nimemwambia atafute Mme mwingine kanisani kwao ndo watawezana na sio Mimi, mke wa hivi hanifai, hata mshahara wote anapeleka huko, hilo kanisa Jumapili moja tu kuna sadaka kama 12 hivi tangu asubuhi hadi jioni, unaweza kwenda na laki mbili usirudi hata na shilingi jioni, bado katikati ya wiki, halafu wachungaji wanaishi kifajari.

Huyo mchungaji wa hilo kanisa ameshawateka akili, mimi binafsi nilikua huko nikahama kutokana na hiyo biashara ya kutakiwa kushinda huko 24/7 na pia kutumia sehemu kubwa ya mapato yangu kanisani badala ya kujenga familia, kanisa gani wanaomba hadi salary slip? Na usipowapa watakusema sana kwamba umepotea njia na kadhalika
Kanisa gani halijali ndoa za watu?

Sio kwamba sipendi mke wangu aende kanisani, aende kwa kiasi na ratiba akizingatia kuwa yeye ni mama wa familia, inapaswa kwenda kanisani unashiriki na wenzako mchana au jioni unarudi home, jumatano unakwenda kwa maombi masaa mawili, six jioni unarudi kwako, there will be nothing wrong, lakini huwezi kwenda kushinda huko 24/7. Seven days a week, inakuja kweli hiyo?

Hata dada wa mke wangu niliempiga, mumewe pia alikuja kwangu na malalamiko kama haya ya kwangu, nimeamua simtaki tena, kwanza akili yangu imeshachanganyikiwa,
Nonsense

Ni bora nirudi kwa Rachel, alinivumilia tangu chuo hadi mtaani nikamtendea vibaya nikaoa mlokole nisiemjua, kwa kweli najuta sikujua nachofanya.
Pole sana ,kama ndivyo kweli hajui anacho kitafuta ,wote tunao sali na kuswali lengo ni mbingu.ila kwa HV hapana anamtumikia mtu. Kuna kioja kingine cha hv Yule baba alikuw anaudumiwa na beki tatu na watoto pia ilifika kipindi yule baba akajenga nyumba nyingine akaoa yule beki 3 watoto wote wakakataa kubaki na mama yao wakaenda kwa bek3 mama ndio anstuka analeta na mchungaji aliambuli manyoya amebaki na nyumba tu
 
Chapa kabisa, kanisa gani hilo Hadi unasahau Mtoto, by the way walokole wengi huwa hawako sawa upstairs
 
Mkuu pole sana,nimecheka sana "eti walipofika niliwakamata wote wawili na kuwapa kipigo kizito"

Ushauri wangu kwako Msamehe,alafu mwambie aache tabia ya kusikiliza wazazi wake anatakiwa atambue kwamba ninyi wawili mumeungana mmekuwa sio wawili tena bali wamoja Mwanzo 2:18-24 na pia atambue wewe kichwa cha familia unatakiwa kusilizwa kwanza barua ya kwanza kwa Petro 3;1-7 anapochukua jukumu la kuwasikilizaa wazazi wake zaidi anapinga maandiko hata kama anaenda kukesha kanisani.
 
We jamaa umenichekesha kidogo,ulipomvunja mbavu shemejio! Anyway maisha ni mafupi,hamna sababu za kuishi na stress Fanya maamuzi magumu tu hamna namna!
 
Siku hizi mama wakwe zetu ndo wanawapa vichwa mabinti zao. Usitegemee uwashirikishe wazazi wa mkeo disappointment za binti yao wakakuelewa. Huwa wanamtetea binti yao na happier ndio mwanzo wa kuharibika kimoja
 
Nitarudi ukitaja kanisa analosali mkeo vinginevyo naona ni fasihi simulizi tu.
 
Swali langu kwa mtoa uzi huu.. huyo mwanamke kabla hujamuoa umekaa naye muda gani kwny uchumba,? Na je hizo tabia hukuziona kipindi cha uchumba au wataka sema kazianza mkiwa tayari kwenye ndoa? Ama ulijibebea tu ukaweka ndani?
 
Back
Top Bottom