Najuta kumfahamu huyu binti

Najuta kumfahamu huyu binti

unatamani kufa kwa sababu ya mtu? Khaa rest in pieces mkuu!

Ila jikeep busy hiyo hali itapita
 
Habari za majukumu wana jf,
kwa mara ya kwanza nimejikuta nikiingia katika jukwaa hili nikiwa
muhanga na majeruhi wa kufa leo au kesho kwa sababu ya mapenzi, ni miaka
2 sasa imepita toka nimfahamu huyu binti anayeninyanyasa(tukiwa shule
kipindi hicho) na katika kipindi cha mwaka mmoja tuliokuwa pamoja shule
tuliishi vizuri ila sii kama wapenz, nilitokea kumpenda sana ila
sikuthubutu kumwambia kutokana na kuhofia kuchanganya hali ya mambo japo
baadaye aligundua. Na katika kipindi cha mwaka mzima tulipoachana baada
ya kumaliza shule tuliendelea kuwasiliana japo kwa mara chache ila
ugonjwa wangu haukuwa umetibika bado kwan kila nilipoisikia sauti yake
mapigo ya moyo wangu yaliongeza kasi lakin pia sikumwambia kuwa
nampenda. Zahama ilianza baada ya kumwambia ukweli kuwa nampenda mwezi 1
uliopita, alinikubalia na akaniambia hilo alilitambua toka mwanzo, cha
ajabu kwangu imekuwa mateso kwan ninapoongea naye kwenye simu najisikia
burudani sana ila simu iki katika tu na aman nayo inatoweka kwangu na
hakuna ninachoweza kufanya kikawa sawa hata kula inakuwa shida, namuwaza
yeye tuu. Natamani kusitisha uhusiano ila nafsi yangu inanambia ni
afadhali mimi nife kuliko kusitisha uhusiano, nashindwa kuelewa kuwa
nampenda au namtaman. Wanajamvi plz, ushauri wenu ni muhimu sana kwangu
kwan najihisi kupungua uzito kwa kuwaza. Ahsanten

ukisia love is craze ndio hiyo, sasa suburia love is blind.
 
Umezama umezama kwenye bahari ya huba wewe kazana tu lkn angalia dont test the depth of river with both legs anza kwanza na mguu mmoja ili iwe rahisi kujikwamua usiondoke na mafuriko

ushauri mzuri. anaweza akaingia miguu yote miwili baadae akagundua na yeye ameongezwa kwenye list. hapo lolote baya linaweza kutokea!
 
Kwny simu unapata hizo stress je physicaly mkiongea inakueje?hatofaint kwel?



Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
sikushangai,yalishanikuta hayo.ni ugonjwa mbaya sana,maana mambo yakienda ndivyo sivyo,utapata maumivu makali sana
 
jamani mapenzi hayana umri au elimu.yakiingia yameingia,ingawa sio wote wako hivyo.kama mtu haujapenda mwenzako unamuona mjinga. kijana ji keep busy baadae utazoea
 
haya ndo matatizo ya kuingia kwa hii mambo ukiwa mtu mzima
ina maana wewe hata michozo ya baba na mama hukufanya wakati ukiw mtoto
angalia unaleta mambo ya kitoto huku we mwanaume ati? wacha mambo jambo things sifa ya mwanaume ni kuwa strong with life changes,,, utakua ***** usipoangalia,, kwanza unaonesha kiwango cha chini kuwa timid, lishindwa kumwambia hadi manzi anakugundua, hafu ndo unajamropokea sasa si unaona kwanza atachukulia advantage ya weakness yako? funguka macho usijelishwa limbwata mdogo angu,, haya mambo yanaenda kwa step,, be smart life goes
 
Back
Top Bottom