Najuta kuharibu ndoa yangu

Najuta kuharibu ndoa yangu

Kuna Dada mmoja nimetokea kuzoeana nae maeneo tunakofanyia kazi hata yeye ni Mjasiriamali mzuri tu. Siku moja nilimkuta amekaa peke yake akionekana ni mtu mwenye mawazo mengi nikajaribu kumdadisi nielewe kinachomsumbua kichwa maana kama ni kipato anacho cha kumuendeshea maisha.

Aliamua kunipa stori yake ya maisha kuwa miaka saba iliopita alikua ameolewa. Anadai mume wake alimpenda sana kwani alimjali sana pamoja na kumheshimu. Ila yeye kama yeye hakuona thamani ya upendo kutoka kwa mume wake kwani alimdharau na kumfanyia makosa mengi lakini mume wake hakuonesha kukata tamaa kwani aliendelea kumpenda na mara nyingi alitumia muda mwingi kumshauri ili ajitambue na vile vile aitambue Dunia kua haina mwenyewe.

Anasema alianza kumsaliti mume wake ingawa mume wake hakuonyesha dalili za kusaliti ndoa yao. Anadai alikua anatoka na kijana mmoja ambae alimpenda zaidi ya mume wake siku moja mme wake alifumania sms kwenye simu yake ya mapenzi na ndipo alipomuambia amemkosea makosa mengi ila kwa lile hawezi kumsamehe siku hiyo hiyo alimuandikia talaka yake huku mwanaume akitokwa na machozi kwa uchungu pindi alipokua anaandika talaka.

Kutokana na alivyokua anajiamini kuwa mume wake anampenda sana alijipa moyo kua lazima atamsamehe tu, alijaribu kumuomba msamaha lakini mme wake alionekana mgumu akaamua kuondoka akijua baada ya wiki mbili hasira zitapungua na atamsamehe tu.

Aliendelea na uhusiano na yule kijana baada ya wiki mbili alimuomba wakutane ili wayamalize ila mwanaume alikataa. Baada ya mwezi mmoja alisikia kua ameoa mke mwingine na ndipo alipokata tamaa kuwa ameachika moja kwa moja. Ilibidi aongee na yule kijana aliekuwa anacheat nae ili amuoe, hakuamini maneno alioambiwa kuwa hawezi kumuoa kua kamwe katika maisha yake hawezi kumuamini.

Yule dada akamwambia alikuwa anasaliti ndoa yake kwa kua alikua anampenda sana, yule kijana alimuambia katika maisha hakuna kitu kama hicho huwezi kusaliti ndoa yako kisa ulienae humpendi na kama alikua hampendi kwanini alikubali kuolewa nae na akamwambia iwe mwisho wa mahusiano nae.

Aliniambia alijiona ni mjinga kati ya wajinga na baada ya miezi minne yule kijana na yeye alioa. Anasema amekutana na wanaume mbali mbali ili aingie kwenye ndoa mara ya pili lakini ameambulia kuchezewa tu mwisho wa siku anaachwa. Ilifikia wakati akaenda kwa waganga wa kienyeji ili wamuangalizie kama mume wake wa kwanza alimloga asiolewe lakini waganga wawili walimuambia hakuna kitu kama hicho na hata kama akienda kwa mganga akimwambia amelogwa huyo mganga ni tapeli.

Mpaka sasa mume wake walioachana amebahatika kupata watoto wawili na hata yule kijana aliekuwa anatoka nae na yeye ana watoto wawili, kwa hiyo anasema roho inamuuma sana kuharibu ndoa yake ni mwaka wa saba toka aachike.

Ushauri wangu siku zote ukiona umependwa jua thamani ya kupendwa hata kama wewe utakua umempenda kwa wastani vumilia hivyohivyo na heshimu mahusiano yenu. Hasahasa akina Dada nyie ndo mnakumbana na changamoto nyingi hasa linapofika swala la kuolewa ukiona mwanaume amekupenda na ukaamini kweli anakupenda muonyeshe upendo na umuheshimu kwani kuolewa kwenu kunatoka na maamuzi ya mtu mwengine ni tofauti na wanaume.

Hakika ujumbe umenigusa sawia, naomba nami Mungu anisaidie huu mwaka usiishe
niwe nimempata wangu.
"Amen"
 
Kwakweli hawajui hili wasome na wabadilike kwsni hawajui thamani ya mwanamme anapokuwa anawapenda na pia husahau kuna wanawake wazuri zaidi yao na mwanaume anahitaji kupendwa na wako tayari kukuachia chochote na kwenda tafutamwanamke atakayempa FURAHA
 
Na ipo siku au mahali mwanamke huyo anakaa nakuponda kabisa kuwa hakuna mwanaume mwenye mapenzi ya kweli,au anaponda ndoa za watu wakati yeye ni shahidi ya kuwa mtu usipokuwa muaminifu ni lazima uachwe tu hata kama una mimba,na watu wa namna hii tunao sana katika jamii hii,sijawahi kuona wala kusikia mwanamke ambaye hajaolewa au kupata mchumba atayekuwa mumewe ikiwa mwanamke huyo alikuwa anajiheshimu nakuheshimu mahusiano yao,wote walioachika au kutoolewa walishaumiza mtu hapo nyuma(kutokuwa waaminifu),kwa hiyo hiyo ni laana anaishi nayo kama wengine wanavyoish na laana za namna hii,maana machozi ya moyoni ni mabaya afadhali upigwe ujue nimepigwa..
 
malipo hapa hapa dunia,na mkataa pema pabaya panauita,ogopeni sana watu wenye reaction ndogo unapokosea
 
mamafacebook, jino limepona! najua umelala kumbe uko bise na haya majuto ya uy aliebomoa ndoa yake wa mikono yake mwenyewe achana nae, uyu tunamwita mwanake mpumbavu. Wajanja tunabembeleza mpaka umauti ututenganishe

Yaani hapo ilikua sijaling'oa bado nipo nasubir zamu yangu ila nimelitoa sasa hiv namalizq nyimbo zote hapa kwa maumivu sasa hivi naimba gospel
 
Hii story inafanana na moja iliyotokea miezi miwili iliyopita hapa Mza....

Dah..... Sina la kusema zaidi ya kumpa pole mlengwa.

Nimepata kitu hapa....
 
Nimeipenda reaction ya jamaa,kuoa baada ya mwezi ili kuziba gape.Iyo laana ya usaliti itamtafuna uyo mwanamke mpaka kufa.
 
Mshauri huyo dada amtafte jamaa aombe msamaha hata kama wasiporudiana. Atubu, na kujutia makosa yake. Atakuwa freee na atapata mume mwingine.
 
Na ipo siku au mahali mwanamke huyo anakaa nakuponda kabisa kuwa hakuna mwanaume mwenye mapenzi ya kweli,au anaponda ndoa za watu wakati yeye ni shahidi ya kuwa mtu usipokuwa muaminifu ni lazima uachwe tu hata kama una mimba,na watu wa namna hii tunao sana katika jamii hii,sijawahi kuona wala kusikia mwanamke ambaye hajaolewa au kupata mchumba atayekuwa mumewe ikiwa mwanamke huyo alikuwa anajiheshimu nakuheshimu mahusiano yao,wote walioachika au kutoolewa walishaumiza mtu hapo nyuma(kutokuwa waaminifu),kwa hiyo hiyo ni laana anaishi nayo kama wengine wanavyoish na laana za namna hii,maana machozi ya moyoni ni mabaya afadhali upigwe ujue nimepigwa..

Aisee big up sana! mchango wako maridadi kabisa.yaani ni kweli tupu.
 
sometimes ni muhimu kutikisa kiberiti, nishawah kumwambia mtu naomba tutengane kwa muda coz alikua ananichukulia poa, kuna msemo kuwa huwezi kipenda kitu ambacho huwez kukipoteza so mpenz wako ukimuonesha kuwa ndo yeye tu tegemea vituko
 
mkasa huu utawafunza kiasi...ila wanawake na wanaume wote wameubwa kusahau..... watasoma hapa baada ya siku kadhaa wanasahau
 
Watu huwa hatujui thamani ya kile tulicho nacho hadi siku tukianza kitafuta pale kitowekapo mikononi mwetu.
 
Mmmh! Hii stor tu.
Kweli baaa ya mwez mwanaume aoe?!
Lakn hadithi yako ina mafunzo mazur.
 
aisee kuna mtu wangu wa karibu sana yamemkuta km hayo
majuto mjukuu
 
Back
Top Bottom