Naishindaje hofu ya kifo inayoniandama?

amini kwamba piga ua ipo siku utakufa, then endelea na shughuli zako. Acha kuogopa kitu ambacho ni PIE kwako
 
Ahsante mkuu.... Ulichokisema ni sawa kabisa.
Sasa mimi inanitokea tu mawazo ya hofu ya kifo yanatawala akili yangu, japo nafahamu yote uliyoandika hapo.... Sasa nitumie mbinu ipi kuyafukuza hayo mawazo au kuzuia yasije?
Puuzia !! Usiwe serious sana na maisha yenyewe, enjoy kila unapopata nafasi ya kufanya hivyo
Kufa ni lazima mkuu , i hate the idea ya kwanini tunazaliwa na kuja kufanya struggles zote hizi huku kifo kinatusubiri muda wote.
 
Hakuna asiyeogopa kifo wote tunapenda uhai.


Lakini elewa kifo ni kama chafya ikifika siku huwezi zuia. Ukiwa na afya pamoja nguvu basi fanya yatakayoufurahisha moyo wako ilimradi usikwaze watu, Mungu wala Jamhuri.
 
Kufa ni lazima, ukishajua hivyo hutakiwi kuwaza tena juu ya kifo, jua tu kwamba kuna siku utakufa, utazikwa na watu wàtakuacha peke yako kaburini. Kitakachotokea huko ndani hakuna anayejua.

Relax and enjoy life, life is for the living...
 
Pole sana jitahidi kujichanganya na watu mbalimbali, kifo kipo hakiepukiki cha muhimu ni maombi kwa sana na kumshukuru Mungu kila iitwapo leo.
 
Usijali Mkuu uwaze au usiwaze punishment iko palepale. Muhimu cha kukushauri kaa katika Imani yako ya Kiroho Uliyonayo kwa Udhabiti. Ili siku ya siku ikifika Imani Yako ikitetee..
 
Wakuu salama?

Hivi karibuni, hasa kwa mwaka huu wa 2021 nimoepoteza watu wa karibu wengi sana tangu huu mwaka uanze; Nimepoteza wazee wangu-baba wakubwa wanne, pia nimepoteza marafiki zangu wale wa inner cycle watatu,akiwemo rafiki yangu mmoja wa karibu sana aliefariki kwa kansa ya utumbo, na jamaa zangu wengine kadhaa (ndugu wa mbali na marafiki).

Pia, kuna vifo viwili vya wana JF vya hivi karibuni ambavyo vimenigusa sana, cha ip_mob na warumi hawa watu nilikua nawakubali sana hapa JF japo sijawahi kukutana nao uso kwa uso.

Hivi vifo kwa huu mwaka vimenifanya nimekua mtu wa hofu sana juu ya kifo; Yaani sasa hivi nawaza sana juu ya kifo na nashikwa na uoga wa kutisha hadi natetemeka.

Mara nyingi usiku nakosa kabisa usingizi, nawaza juu ya kifo hadi machozi yananitoka. Saa zingine naogopa hata kulala usiku na kuufukuza usingizi, maana nawaza kuwa naweza nikalala nisiamke tena, nikapotelea usingizini na kuaga dunia.

Hii hali naona imeanza kuathiri shughuli za mihangaiko yangu, kwani mchana nakua nimechoka sana na pia inanikosesha amani kabisa naishi maisha ya wasiwasi sana.

Ndugu zangu, nimekuja humu kuwauliza je nyie wenzangu mnatumia mbinu gani kuondoa hofu juu ya kifo au kuwafanya msiwaze au kuogopa kifo?

Nimejaribu kuwa nasali sana na kwenda kanisani kila siku, nimeongea pia na mchungaji na amenifanyia maombi na kunipa nasaha, lakini bado imekua ngumu sana kwa mawazo na uoga huo kunitoka.

Naomba mnisaidie ndugu zangu nawezaje kupambana na hii hali?

Naomba mnisaidie wadau.
Ahsanteni.
Mkuu wewe unasumbuliwa na hofu kubwa..ni ugonjwa huo wa akili...ukiweza tafuta mwanasaikolojia akushauri..la tumia mbinu zifuatazo: jiepushe kukaa bure na pekeyako..jitahidi kujichanganya na marafiki wanaongea mambo tofauti na kifo, fanya mazoezi utokapo kazini maana mwili utachoka na hvo ukilala utalala fofofo.
Usichukulie poa hali hii...usipokuwa makini utajikuta ushapata uchizi kabisaa
 
Huo uoga unaitwa Thanatophobia kwa kizungu. Unaweza ukagoogle uone wanasaikolojia wanavyoshauri jinsi ya kuuepuka huo uoga.

Lakini mkuu kuna vitu ni bora kuvikubali tu kwenye maisha. Kifo ni experience ambayo ni lazima kuipitia.

Binafsi kwenye kufa kama kufa huwa siogopi. Ila ambacho huwa kinaniogopesha ni maumivu nitakayoyapitia kabla ya kufa. Imagine ufe kifo cha kuungua na moto, I always feel it to be painful as a human being.
 
Hali hii ilinifika pia ,nilichofanya nikakubali kwamba kifo ni haki yetu! Yan nitakufa tu! Nikaanza kufuatilia documentaries mbalimbali kuhusu kifo !! Jinsi mortuary palivyo ! Watu wanavoandaliwa mpaka kwenda kuzikwa ! Kuna hadi watu wanafanya hadi make up kwenye miili iliyojeruhi vibaya ili iweze kuagwa! Ooh mpaka nikawa addicted kabisa. Hofu inaisha ,lakini uchungu wa kuondokewa na mpendwa wako ni kawaida.
 
Kwanza pole sana ,pili nikuambie tuu kuwa hii hali inatokea sana kadili unapokuwa mtu mzima kwa maana kuongezeka umri , sababu ni majukumu tulionayo na matamanio ya ndoto zetu ,sasa isikupe shida chakufanya iambie nafsi yako kwamba juzi nliogopa kufa na sikufa hali kadhalika jana pia sikufa na leo sifiii apo tuu , nasema hivi kwasabu mimi mwenyewe imenitokea hii kitu na ndio mbinu nlio tumia ,lakin jitaid kusali binafsi usitegemee sana kuombewa omba mwenyewe ivoo tuu mkuu.
 
Kuna siku usiku nilipigwa na kichomi kwenye moyo wakati nimelala, aiseeeh nilishtuka na kupiga kelele mpaka wife akashangaa, mapigo ya moto yalienda mbio balaa.

Kuanzai hapo nikawa ni mtu wa kuwazia kifo tu(kama wewe hivyo kabsa) nikawa Sitaki usiku uingie na ukiingia nikiwa kitandani nawaza labda moyo utalipuka upasuke nife,kwahiyo sikuwa kabisa na amani for almost two weeks na baadae mpaka hivi ninavyoandika suogipi chochote pamoja na kwamba bado nakumbuka like pigo la moyo.Nina uhakika 100% kama wewe ni mtu wa kukuchamganya hilo litapita faster tu.

Nakuongezea na hii, Tulikua na rafiki yetu mmoja (wa kufa na kuzikana) tulikuwa tunafanya nae kazi pale GGM, jamaa alikuwa na pesa chafu (alikuwa na kaurafiki JPM), huyu jamaa alianza kusumbuliwa na kisukari miaka ya hivi karibuni alipambana sana lakini siku moja usiku akazidiwa na akafariki.....aiseeh kuna jamaa yangu nae alikuwa na kisukari aliingiwa na hofu ya kifo kiasi kwamba kila mikikaa anawaza kufa tu, anakuuliza kama Benjamin amekufa pamoja na hela zake zile sisi hizi hela tunazotafuta ni za nini Sasa?...Kilichofata sukari yake haikuwa inashuka for almost a week licha ya kwamba anatumia dawa..sukari yake ulikuja kukubali kuwa regulated alipoacha kuogopa kifo.

Maana yangu ni kwamba, chunga sana hofu isizidi kiwango maana kupitia jamaa yangu nimejifunza kwamba hofu ni ugonjwa mwingine unaloweza kukuua.

Hupaswi kujitwika mawazo ambayo daima hautaoata suluhisho lake, utajipa msongo wa mawazo tu. Kifo hakifikiriki kabisa, no matter what tutakufa tu kwahiyo kukiwaza ni kujitia mzigo tu.
Ahsante sana kwa ushauri.
Hofu ni mbaya sana aisee.
 
Soma Zaburi 34:4 na Mathayo 11:28

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
Zaburi 34:4
"Nilimwomba Mwenyezi-Mungu naye akanijibu, na kuniondoa katika hofu zangu zote."
Mathayo 11:28
"Njoni kwangu nyinyi nyote msumbukao na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha."
Shukrani sana mkuu kwa mstari hii, imenipa faraja. Nimeiandika kwenye notebook yangu, nitakua naipitia mara kwa mara.
 
Ha ha ha imenibidi nikoment kufa tumeumbiwa binadamu na mungu alivyo wa ajabu anatusahulisha kabisa kama kuna kifo mpaka usikie Fulani kafa na we ndo unashtuka kumbe kuna kifo acha kuwaza siku ikifika utakufa tu ulale,usilale,usimame,ukae utakufa tuuu.
Ukweli mchungu.
 
Hali hii ilinifika pia ,nilichofanya nikakubali kwamba kifo ni haki yetu! Yan nitakufa tu! Nikaanza kufuatilia documentaries mbalimbali kuhusu kifo !! Jinsi mortuary palivyo ! Watu wanavoandaliwa mpaka kwenda kuzikwa ! Kuna hadi watu wanafanya hadi make up kwenye miili iliyojeruhi vibaya ili iweze kuagwa! Ooh mpaka nikawa addicted kabisa. Hofu inaisha ,lakini uchungu wa kuondokewa na mpendwa wako ni kawaida.
Natumaini na mimi hiyo hali itaisha pia.
 
Back
Top Bottom