TheCrocodile
JF-Expert Member
- May 31, 2021
- 1,077
- 2,813
Wakuu salama?
Hivi karibuni, hasa kwa mwaka huu wa 2021 nimoepoteza watu wa karibu wengi sana tangu huu mwaka uanze; Nimepoteza wazee wangu-baba wakubwa wanne, pia nimepoteza marafiki zangu wale wa inner cycle watatu,akiwemo rafiki yangu mmoja wa karibu sana aliefariki kwa kansa ya utumbo, na jamaa zangu wengine kadhaa (ndugu wa mbali na marafiki).
Pia, kuna vifo viwili vya wana JF vya hivi karibuni ambavyo vimenigusa sana, cha ip_mob na warumi hawa watu nilikua nawakubali sana hapa JF japo sijawahi kukutana nao uso kwa uso.
Hivi vifo kwa huu mwaka vimenifanya nimekua mtu wa hofu sana juu ya kifo; Yaani sasa hivi nawaza sana juu ya kifo na nashikwa na uoga wa kutisha hadi natetemeka.
Mara nyingi usiku nakosa kabisa usingizi, nawaza juu ya kifo hadi machozi yananitoka. Saa zingine naogopa hata kulala usiku na kuufukuza usingizi, maana nawaza kuwa naweza nikalala nisiamke tena, nikapotelea usingizini na kuaga dunia.
Hii hali naona imeanza kuathiri shughuli za mihangaiko yangu, kwani mchana nakua nimechoka sana na pia inanikosesha amani kabisa naishi maisha ya wasiwasi sana.
Ndugu zangu, nimekuja humu kuwauliza je nyie wenzangu mnatumia mbinu gani kuondoa hofu juu ya kifo au kuwafanya msiwaze au kuogopa kifo?
Nimejaribu kuwa nasali sana na kwenda kanisani kila siku, nimeongea pia na mchungaji na amenifanyia maombi na kunipa nasaha, lakini bado imekua ngumu sana kwa mawazo na uoga huo kunitoka.
Naomba mnisaidie ndugu zangu nawezaje kupambana na hii hali?
Naomba mnisaidie wadau.
Ahsanteni.
Hivi karibuni, hasa kwa mwaka huu wa 2021 nimoepoteza watu wa karibu wengi sana tangu huu mwaka uanze; Nimepoteza wazee wangu-baba wakubwa wanne, pia nimepoteza marafiki zangu wale wa inner cycle watatu,akiwemo rafiki yangu mmoja wa karibu sana aliefariki kwa kansa ya utumbo, na jamaa zangu wengine kadhaa (ndugu wa mbali na marafiki).
Pia, kuna vifo viwili vya wana JF vya hivi karibuni ambavyo vimenigusa sana, cha ip_mob na warumi hawa watu nilikua nawakubali sana hapa JF japo sijawahi kukutana nao uso kwa uso.
Hivi vifo kwa huu mwaka vimenifanya nimekua mtu wa hofu sana juu ya kifo; Yaani sasa hivi nawaza sana juu ya kifo na nashikwa na uoga wa kutisha hadi natetemeka.
Mara nyingi usiku nakosa kabisa usingizi, nawaza juu ya kifo hadi machozi yananitoka. Saa zingine naogopa hata kulala usiku na kuufukuza usingizi, maana nawaza kuwa naweza nikalala nisiamke tena, nikapotelea usingizini na kuaga dunia.
Hii hali naona imeanza kuathiri shughuli za mihangaiko yangu, kwani mchana nakua nimechoka sana na pia inanikosesha amani kabisa naishi maisha ya wasiwasi sana.
Ndugu zangu, nimekuja humu kuwauliza je nyie wenzangu mnatumia mbinu gani kuondoa hofu juu ya kifo au kuwafanya msiwaze au kuogopa kifo?
Nimejaribu kuwa nasali sana na kwenda kanisani kila siku, nimeongea pia na mchungaji na amenifanyia maombi na kunipa nasaha, lakini bado imekua ngumu sana kwa mawazo na uoga huo kunitoka.
Naomba mnisaidie ndugu zangu nawezaje kupambana na hii hali?
Naomba mnisaidie wadau.
Ahsanteni.