Naimisi Tanzania ya miaka ya 70

Naimisi Tanzania ya miaka ya 70

huko Marekani ulishaona watu wamekaa foleni kusubiri kununua sabuni mbuni, mafuata ya taa, dawa ya mbu, mkate wa Siha, n.k?

Unazungumzia miaka ya themanini baada ya vita. Hata Marekani baada ya vita vya Iraq uchumi ulikuwa zero watu wakakosa kazi wameokolewa na mikopo. Na deni la nchi limezidi mara tatu mpaka leo.

Nyerere alikosa wa kumsaidia tu na alipoona vimezidi na hakukubaliana na masharti ya wazungu akaacha na urais wenyewe.
 
Ni ya miaka ya 70 mwishoni wakati wa vita na baada ya vita, hujaelewa nimeandika nini?

Vita ilikuwa ni mwaka 78 baada ya hapo Nyerere akatangaza miezi 18 ya kufunga mikanda. Wazungu wakaendelea kumkwamisha kiuchumi kama wanavyomfanyia Mugabe.

Hata kama kulikuwa na umuhimu wa kubadilisha siasa hivi hakukuwa na sababu ya kuvunja misingi ya maadili iliyokuwepo. Ubinasishaji wa mali za uma, wizi na rushwa, udini, ukabila na kuuwa viwanda.
 
Na ndio maana namkubali sana Magufuli labda ataturudisha katika mstari.
 
  • Thanks
Reactions: KVM
Vita ilikuwa ni mwaka 78 baada ya hapo Nyerere akatangaza miezi 18 ya kufunga mikanda. Wazungu wakaendelea kumkwamisha kiuchumi kama wanavyomfanyia Mugabe.

Hata kama kulikuwa na umuhimu wa kubadilisha siasa hivi hakukuwa na sababu ya kuvunja misingi ya maadili iliyokuwepo. Ubinasishaji wa mali za uma, wizi na rushwa, udini, ukabila na kuuwa viwanda.


Kwa hiyo umeelewa enheee? Tulianza kupiga foleni mwaka 1978 mpaka 80.
 
Wangapi leo hii wako mijini wanategemea nyumba za mababu na mabibi zao na wao wenyewe hawawezi kununua nyumba?

Kulikuwa na mafuta ya kimbo, siagi za tanbond, maziwa ya kcc. Watu wanaokula mkate kwa siagi utasema wana shida ya chakula.

Familia ngapi leo hii zinakutana nyumbani kwa chai ya saa kumi? Ilikuwepo pale chuo kikuu mlimani sijui kama hawajaiondoa.

Elimu bure mpaka chuo kikuu hulipi hata senti tano.

Hospitali bure matibabu ya aina yeyote na huduma zilikuwa bora.

Barabara safi na usafiri wa uhakika.

Viwanda vya nguo vilikuwa vingi na mafundi cherahani kibao. Kuvaa kiraka ilikuwa ni uamuzi au hesabu za mtu. Ukiniuliza mimi bora kuvaa kiraka kuliko kuvaa mtumba wa mzungu. Wachafu sana hawa jamaa.

HAYA NI MAISHA YA ULAYA LEO. WATANZANIA WALIISHI HIVYO KWENYE MIAKA YA SABINI.
 
Enzi hizo nilikamatwa na polisi na kunishikiria kwa masaa kadhaa kisa nimenunua vitu vichache kama sabuni za lifeboy na colgate pale Tunduma mpakani na Zambia kwa matumizi yangu ya shule. Hivyo maisha hayakuwa mazuri kivile hasa kwenye kile kipindi cha miezi 18 ya kufunga mikanda baada ya vita na nduli Amini.
 
Enzi hizo nilikamatwa na polisi na kunishikiria kwa masaa kadhaa kisa nimenunua vitu vichache kama sabuni za lifeboy na colgate pale Tunduma mpakani na Zambia kwa matumizi yangu ya shule. Hivyo maisha hayakuwa mazuri kivile hasa kwenye kile kipindi cha miezi 18 ya kufunga mikanda baada ya vita na nduli Amini.

Tofautisha maisha ya mwanzoni mwa miaka ya themanini na maisha ya miaka ya 70.
 
Hata cereals zilikuwepo tulikuwa tunaziita vibato.
 
Televisheni ya Zanzibar TVZ ilifunguliwa mwaka 74 Na ndio televisheni ya kwanza ya picha za rangi kusini mwa Sahara katika Afrika.
 
Tena redio za zamani zilikuwa hazina masihara. Mradi upate betri mpya za eveready chapa ya nyau hata milimani vijijini zilikuwa zinafika.
 
Hata mimi najiuliza 'SIJUI TULIPOTEA WAPI'
Katika umri wangu nimebahatika kuyaona yote uliyoyasema. Na bado naendelea kuyaona mapya kama smartphone, voda,tigo,dala dala daraja la Kigamboni, stadium nk. Haya yote yangeliongezeka kwa yale uliyoyataja, tungelikuwa mbali na ningelikuwa nasubiria kwa hamu hiyo miaka 70. Lkn hali ilivyo kwa sasa na rushwa, ufisadi, majipu, mishahara hewa, deal deal nk. Sijui kama natamani kuiona Tz ya miaka 70.
 
Kulikuwa na Kajima na Mowlem walioijenga Dar bila ya kuwasahau MECCO.
 
Kwa hiyo umeelewa enheee? Tulianza kupiga foleni mwaka 1978 mpaka 80.
Mkuu. Nilishaweka uzi hapa unaoitwa"cable za kibalozi". Umetokea wikileaks na unazungumzia misaada Nyerere anaomba Marekani. Waziri wake Malecela ndio aliyekuwa mpiga debe wake wa kuomba misaada. Hiyo ilikuwa mwaka 1974-76.

Sio tu habari za mawasiliano ya kibalozi yanaonyesha Nyerere anaomba msaada wa chakula bali pia msaada wa kujengewa barabara, zahanati na hata majenereta ya umeme na mafriji. Na Malecela aliomba sana waje wenyewe waone jinsi Tanzania inavyohitaji misaada. Na maofisa wa Marekani wakaja na kutoa misaada mingi tu.

Pia, muhimu zaidi, viongozi wa ulaya wakija Tanzania, hasa kutoka Skandinavia na Uholanzi, Nyerere sio tu anaomba msaada ili ailishe wananchi wenye njaa kali vijijini bali pia anawaombea msaada viongozi wa Msumbiji, Angola na nchi nyingine zilizokuwa zinagombania uhuru wao kwa wakoloni ili waweze kujikomboa na kulisha jumuia yao nje ya nchi zao.

Yote tulikuwa hatujui, tunalishwa propaganda na RTD.

Ila Nyerere apologists husema kuwa hali mbaya ya uchumi ilitokana na vita vya kagera. It's BS.








Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app
 
Stadium! Tuliruka sana ukuta uwanja wa Karume. Kuna siku nilichupa nikadondokea katikati ya jopo la wanamgambo waliokuwa wanagawana majukumu ya kulinda uwanja. Ilibidi wenyewe wacheke.
 
Sawa mhenga

Sent from my TECNO-C8 using JamiiForums mobile app
 
Ninakumbuka dada mkubwa alipofaulu darasa la saba alipewa warranty ya train kwenda shule. Alituambia shule walipewa minara miwili ya mbuni na gardenia mbili kwa term.
 
Back
Top Bottom