Naimisi Tanzania ya miaka ya 70

Naimisi Tanzania ya miaka ya 70

Umenikumbusha mbali sana mzee mwenzangu, hongera kwa kutunza kumbu kumbu vzr...wengine tushaanza kupata magonjwa ya kusahau sahau

Sent from my GT-N8000 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu. Nilishaweka uzi hapa unaoitwa"cable za kibalozi". Umetokea wikileaks na unazungumzia misaada Nyerere anaomba Marekani. Waziri wake Malecela ndio aliyekuwa mpiga debe wake wa kuomba misaada. Hiyo ilikuwa mwaka 1974-76.

Sio tu habari za mawasiliano ya kibalozi yanaonyesha Nyerere anaomba msaada wa chakula bali pia msaada wa kujengewa barabara, zahanati na hata majenereta ya umeme na mafriji. Na Malecela aliomba sana waje wenyewe waone jinsi Tanzania inavyohitaji misaada. Na maofisa wa Marekani wakaja na kutoa misaada mingi tu.

Pia, muhimu zaidi, viongozi wa ulaya wakija Tanzania, hasa kutoka Skandinavia na Uholanzi, Nyerere sio tu anaomba msaada ili ailishe wananchi wenye njaa kali vijijini bali pia anawaombea msaada viongozi wa Msumbiji, Angola na nchi nyingine zilizokuwa zinagombania uhuru wao kwa wakoloni ili waweze kujikomboa na kulisha jumuia yao nje ya nchi zao.

Yote tulikuwa hatujui, tunalishwa propaganda na RTD.

Ila Nyerere apologists husema kuwa hali mbaya ya uchumi ilitokana na vita vya kagera. It's BS.








Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app

Hata sioni cha ajabu Nyerere hakuficha kuwa alichukua misaada. Ila kufanywa mpumbavu kwa sababu ya hiyo misaada ndio aligoma na ndio maana baadae walikuja msusia kama wanavyomfanyia Mugabe.
 
Dhamani hamukuwaga na Fesibuku nyoo

Sent from my SM-J100H using JamiiForums mobile app
 
Dhamani hamukuwaga na Fesibuku nyoo

Sent from my SM-J100H using JamiiForums mobile app

Tulikuwa na hii. Ukiita polisi ukiita ambulensi inakuja kama ulaya. We kimeo chako leo hebu ita polisi kama watakuelewa. Kwanza utawaelekezaje na nyumba za siku hizi hazina mitaa. Halafu tulikuwa na telegramu unatumiwa ujumbe au pesa ukiwa shule. Acha tigo pesa mara pesa zimeingia kwa mtu mwingine. Kuna demu alinitumia telegramu dingi akaintasepti weee ilikuwa ishu.

.
336769f3efb7cfebab159ba4e0d4038a.jpg
 
Mkuu. Nilishaweka uzi hapa unaoitwa"cable za kibalozi". Umetokea wikileaks na unazungumzia misaada Nyerere anaomba Marekani. Waziri wake Malecela ndio aliyekuwa mpiga debe wake wa kuomba misaada. Hiyo ilikuwa mwaka 1974-76.

Sio tu habari za mawasiliano ya kibalozi yanaonyesha Nyerere anaomba msaada wa chakula bali pia msaada wa kujengewa barabara, zahanati na hata majenereta ya umeme na mafriji. Na Malecela aliomba sana waje wenyewe waone jinsi Tanzania inavyohitaji misaada. Na maofisa wa Marekani wakaja na kutoa misaada mingi tu.

Pia, muhimu zaidi, viongozi wa ulaya wakija Tanzania, hasa kutoka Skandinavia na Uholanzi, Nyerere sio tu anaomba msaada ili ailishe wananchi wenye njaa kali vijijini bali pia anawaombea msaada viongozi wa Msumbiji, Angola na nchi nyingine zilizokuwa zinagombania uhuru wao kwa wakoloni ili waweze kujikomboa na kulisha jumuia yao nje ya nchi zao.

Yote tulikuwa hatujui, tunalishwa propaganda na RTD.

Ila Nyerere apologists husema kuwa hali mbaya ya uchumi ilitokana na vita vya kagera. It's BS.








Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app

Kumbuka ujamaa wa Nyerere ulikuwa ni wa "kutofungamana na upande wowote". Madaktari walisomea Urusi. TAZARA ilijengwa na wachina. Tuliendelea kuwa kwenye commonwealth ya muingereza. Na njaa ilipozidi kwenye ile miezi kumi na nane ya kufunga mkanda tuliletewa unga wa yanga. Watu walidai ni chakula cha farasi kumbe Marekani kuna mahindi meupe na ya manjano. Hata meusi kama mkaa nimeshayaona.
792b3116f22205186741aeb05c0a614e.jpg
 
Umezimiss Sukari guru za mia mia eh
 
Rudi utumwani.

Utumwa ni mfumo wa maisha wamebadilisha staili. Zamani walikamatwa wakafanyishwa kazi na mnyapara wakapewa chakula wale wasife.

Leo unatoka mwenyewe Mbeya unafanyishwa kazi na bosi unalipwa visenti ule ili usife.

Ngoma droo. Hasa kama umeenda Ulaya kubeba boksi.
 
Utumwa ni mfumo wa maisha wamebadilisha staili. Zamani walikamatwa wakafanyishwa kazi na mnyapara wakapewa chakula wale wasife.

Leo unatoka mwenyewe Mbeya unafanyishwa kazi na bosi unalipwa visenti ule ili usife.

Ngoma droo. Hasa kama umeenda Ulaya kubeba boksi.


Basi kataa utumwa!
Tafuta wa kukuoa akuweke kwenye bustani ya eden uwe unakula tu na kuchezacheza
 
huko Marekani ulishaona watu wamekaa foleni kusubiri kununua sabuni mbuni, mafuata ya taa, dawa ya mbu, mkate wa Siha, n.k?
Hivi baada ya vita vya Iraq uchumi wa Marekani ulikuwa kama wa kwetu baada ya vita ya Kagera? Kama sivyo ulitegemea ni Mmarekani yupi angepanga foleni kusubiria dawa ya meno ama sabuni? Ndio Marekani iliyumba kiuchumi lakini sio kwa kiwango hicho
 
Matusi ya nini kwenye hoja za watu? Hivi baada ya vita vya Iraq uchumi wa Marekani ulikuwa kama wa kwetu baada ya vita ya Kagera? Kama sivyo ulitegemea ni Mmarekani yupi angepanga foleni kusubiria dawa ya meno ama sabuni? Ndio Marekani iliyumba kiuchumi lakini sio kwa kiwango hicho

Mkuu uliyumba zaidi ya ulivyoyumba uchumi wa Tanzania. Ilikuwa benki zife. Watu wanaachishwa kazi kwa maelfu ndani ya siku moja. Kilichowaokoa ni kuwa walikuwa na solution ya haraka haraka Nyerere hakuwa nayo na hakuwa na wakumsaidia.

Wafadhili walimpa masharti ambayo aliyakataa akasema hatageuka nyuma awe jiwe. Mwinyi alipoyakubali masharti alitoa hotuba kuwa ni masharti makali kama mwiba lakini hatukuwa na budi.

Tatizo sio misaada wala masharti ya IMF tatizo ni mijizi inapoiba na kuhujumu pesa za misaada halafu haichukuliwi hatua yeyote. Jitu limeiba adhabu ya kubwa ni kujiuzulu au kuhama chama. What the hell....
 
Hata sioni cha ajabu Nyerere hakuficha kuwa alichukua misaada. Ila kufanywa mpumbavu kwa sababu ya hiyo misaada ndio aligoma na ndio maana baadae walikuja msusia kama wanavyomfanyia Mugabe.
Nyerere walimsusia kwa sababu hakutaka kutimiza sharti la kufungua uchumi wa nchi iwe huru na kuwapa wananchi sauti na kuwa na uhuru zaidi.

Lakini aliheshimika sana kwa mawazo yake na sauti aliyowapa wapiganaji wa uhuru wa nchi mbalimbali dhidi ya wakoloni. Alitembea nje sana kutafuta pesa za kuwasaidia Waafrika kujikomboa.

Hata hivyo, alipewa misaada sana, hasa na nchi za ulaya zilizo na mfumo wa kushoto (left wing parties) kama Sweden, Norway na Uholanzi. Uholanzi na nchi nyingine za ulaya pia iliwapa pesa wapiganaji wa uhuru wa Afrika lakini wakakataa kutoa msaada wa kijeshi. China na Urusi wakakubali ombi la Nyerere la msaada wa kijeshi kukomboa nchi za Afrika dhidi ya Ureno.

Mwaka wa 1973, mafuta yalipanda bei sana kutokana na mchafuko wa siasa na vita Magharibi ya Kati. Nyerere akajikuta amemaliza karibu fedha za kigeni zote benki kununua mafuta na kulisha wananchi waliokabiliwa na njaa kali vijijini. Lakini hakuwa tayari kufungua uchumi wa nchi.


Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu uliyumba zaidi ya ulivyoyumba uchumi wa Tanzania. Ilikuwa benki zife. Watu wanaachishwa kazi kwa maelfu ndani ya siku moja. Kilichowaokoa ni kuwa walikuwa na solution ya haraka haraka Nyerere hakuwa nayo na hakuwa na wakumsaidia.

Wafadhili walimpa masharti ambayo aliyakataa akasema hatageuka nyuma awe jiwe. Mwinyi alipoyakubali masharti alitoa hotuba kuwa ni masharti makali kama mwiba lakini hatukuwa na budi.

Tatizo sio misaada wala masharti ya IMF tatizo ni mijizi inapoiba na kuhujumu pesa za misaada halafu haichukuliwi hatua yeyote. Jitu limeiba adhabu ya kubwa ni kujiuzulu au kuhama chama. What the hell....
Hauwezi kufananisha uchumi wa nchi ya kitajiri na ya kimasikini.

Watu wengi waliachishwawa kazi Marekani na viwanda vingi vimehama Asia kupunguza gharama.

Lakini huwezi kufananisha njaa iliyotukumba Tanzania chini ya siasa ya Ujamaa na njaa ya wananchi wao ilivyoshuka uchumi wao.

Tofauti ya masikini wao na wetu ni kama usiku na mchana.

Tuna "social network" ipi inayomsaidia mlala hoi wa Bongo vijijini?


Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu. Nilishaweka uzi hapa unaoitwa"cable za kibalozi". Umetokea wikileaks na unazungumzia misaada Nyerere anaomba Marekani. Waziri wake Malecela ndio aliyekuwa mpiga debe wake wa kuomba misaada. Hiyo ilikuwa mwaka 1974-76.

Sio tu habari za mawasiliano ya kibalozi yanaonyesha Nyerere anaomba msaada wa chakula bali pia msaada wa kujengewa barabara, zahanati na hata majenereta ya umeme na mafriji. Na Malecela aliomba sana waje wenyewe waone jinsi Tanzania inavyohitaji misaada. Na maofisa wa Marekani wakaja na kutoa misaada mingi tu.

Pia, muhimu zaidi, viongozi wa ulaya wakija Tanzania, hasa kutoka Skandinavia na Uholanzi, Nyerere sio tu anaomba msaada ili ailishe wananchi wenye njaa kali vijijini bali pia anawaombea msaada viongozi wa Msumbiji, Angola na nchi nyingine zilizokuwa zinagombania uhuru wao kwa wakoloni ili waweze kujikomboa na kulisha jumuia yao nje ya nchi zao.

Yote tulikuwa hatujui, tunalishwa propaganda na RTD.

Ila Nyerere apologists husema kuwa hali mbaya ya uchumi ilitokana na vita vya kagera. It's BS.








Sent from my SM-G610F using JamiiForums mobile app


Hii ni kweli ila kumbuka....kwa sisi tuliokulia hapa Dar huo mwaka 1976 hatukuwahi kupiga foleni kununua sabuni mbuni, au sukari guru.....hizi za foleni zilikuja mwaka 1978 na uanzilishi wa maduka ya jumuiya/ujamaa/ushirika (unakumbuka hii) yalianza hapa.
 
Matusi ya nini kwenye hoja za watu? Hivi baada ya vita vya Iraq uchumi wa Marekani ulikuwa kama wa kwetu baada ya vita ya Kagera? Kama sivyo ulitegemea ni Mmarekani yupi angepanga foleni kusubiria dawa ya meno ama sabuni? Ndio Marekani iliyumba kiuchumi lakini sio kwa kiwango hicho


Sasa hap unabisha nini wakati ulishajuwa ukweli, kuna vitu vya kufananisha il si kama hivi.
 
Yalikuwa maendeleo ya furshs kwa wakati ule. Kwa Sasa hali imebadilika maendeleo ya Sasa ni ya wachache

Sent from my TECNO W1 using JamiiForums mobile app
 
Hii ni kweli ila kumbuka....kwa sisi tuliokulia hapa Dar huo mwaka 1976 hatukuwahi kupiga foleni kununua sabuni mbuni, au sukari guru.....hizi za foleni zilikuja mwaka 1978 na uanzilishi wa maduka ya jumuiya/ujamaa/ushirika (unakumbuka hii) yalianza hapa.
Upo sahihi kabisa.

Mimi nilikuwepo. Maisha ya vijijini hata mwaka 1974 na kuendelea ilikuwa magumu sana. Ndio maana Nyerere alinunua ngano nje ili kukabili njaa. Pesa za kigeni ilivyokauka, akaomba msaada Marekani na nchi nyingine kulisha wananchi.

Mwska 78 na kuendelea, nakumbuka kununua chokoleti ya magendo kutoka Kenya (cadbury) ambayo napenda kula mpaka leo. Pia, kushonewa Kaunda suti, kukaa foleni na kitabu changu cha ration ya kilo ya sukari na unga wa Yanga. Wengi pia walitumia unga wa mhogo. Sabuni za msaada kutoka Urusi na mafuta ya kupikia ya msaada lakini wajanja walikuwa wanauza mitaani. Nadhani walikuwa wanaitwa walanguzi.

Tumetoka mbali sana kwa kweli.
 
Zama zimebadilika mkuu hiyo ilikuwa yako yetu hii mbona bado iko poa
Kuna barabara za kufika tuendako
Mawasiliano ya sim
Shule huru(binafsi)
Sawa viwanda vimepungua ila bidhaa zipo angalau kutokana na soko huria
Nk

Sent from my SM-N9005 using JamiiForums mobile app

Viwanda vimeongezeka sana. Wakati wa Nyerere viwanda ilikuwa vichache na vyote vya serikali
 
Back
Top Bottom