- Thread starter
- #61
Upo sahihi kabisa.
Mimi nilikuwepo. Maisha ya vijijini hata mwaka 1974 na kuendelea ilikuwa magumu sana. Ndio maana Nyerere alinunua ngano nje ili kukabili njaa. Pesa za kigeni ilivyokauka, akaomba msaada Marekani na nchi nyingine kulisha wananchi.
Mwska 78 na kuendelea, nakumbuka kununua chokoleti ya magendo kutoka Kenya (cadbury) ambayo napenda kula mpaka leo. Pia, kushonewa Kaunda suti, kukaa foleni na kitabu changu cha ration ya kilo ya sukari na unga wa Yanga. Wengi pia walitumia unga wa mhogo. Sabuni za msaada kutoka Urusi na mafuta ya kupikia ya msaada lakini wajanja walikuwa wanauza mitaani. Nadhani walikuwa wanaitwa walanguzi.
Tumetoka mbali sana kwa kweli.
Toka lini ngano ikanunuliwa kukabili njaa Afrika?
