Naimisi Tanzania ya miaka ya 70

Naimisi Tanzania ya miaka ya 70

Unazungumzia mtu ambaye alijiuzulu akakaa pembeni na kuwaachia nyiye vijana muongoze. Mkaona short cut ni ubinafsishaji kama unavyotaka wewe na kuuwa viwanda kwa kuagizia bidhaa za nje. Unafikiri alishindwa kufanya kama Museveni au Mugabe. Ni ego zipi tena unazozingumzia?
Alijiuzulu BAADA ya miaka 21!!!!!!

Are you that ignorant/blind?
 
Yeah mtoa mada hii u make my day,nchi ina heshima na adabu,ukipelekwa jela ni kwa makosa sio visasi vinavyofanyika sasa,watu wanapambikiwa kesi ambazo sio za kwao,Babu Seya ile kesi naamini haukuamuliwa kihalali,DNA TEST ingesaidia kuamua ukweli kuhusu ile kesi,watu hata kwenye dunia ya kwanza wanapanga foleni ni kitu cha kawaida,kipindi hicho our no 1 naye alikuwa anapanga foleni,mmmm Zeni 2017 babu kubwa ukija kwenye muziki wa asili au dansi kila kitu kilikuwa natural sio sasa wanamziki wakiimba lazima wabane pua zao,sikiliza natural voice ya Bitchuka,DEDE(RIP),N.K ,KIPINDI CHA MICHEZO kiliboreshwa zaidi na Abdul Masudi (RIP),yes kipindi hicho tumeishi maisha bora.
 
Una maana viwanda vilikufa wakati wa Nyerere au vilikufa watu walipoanza kuvaa mitumba?

Zamni kuvaaa mitumba ilikuwa ni kitu cha aibu kabisa. Mitumba ilikuwa inaitwa kafa ulaya. Jiina mitumba lilianza kutumika miaka ya sabini mwishoni hasa hasa ikimaanisha magari yaliyotumika yaliyokuwa yanaingizwa na mabaharia. Mengi yao yalepelekwa pale uwanja wa taifa.

Mitumba ya nguo ilianza kuingia rasmi baada ya kuruhusiwa na Salim Ahmed Salim wakati huo akiwa Waziri Mkuu. Alikuwa kwenye ziara kule kusini, Mtwara na wananchi wengi hawakuvaa vizuri kabisa kisa ikiwa ni ukosefu wa nguo. Ndipo aliposema asingependa kuwa Waziri Mkuu wa watu wanaotembea uchi na kuruhusu mitumba kuingia.

Zamani, kabla ya Azimio la Arusha tulikuwa na viwanda vya nguo. Mashati kwa mfano yalikuwa yanatengenezwa na kiwanda cha Gossage cha Tanga. Karibu kila kijiji kilikuwa na mafundi wa kushona. Walishona mashati, suruali, chupi, sidiria, n.k. Kwenye miaka ya 70 katikati mafundi ushonaji, hasa wa mijini walilazimishwa kujiunga pamoja kwenye vikundi vya ushirika. Hilo suala lilisimamiwa na Kawawa - ufungaji wa maduka binafsi.
 
Wakati huo tulikuwa tukisikiliza Radio Soroti ya Uganda na zile za Kenya kulikuwa na mtangazaji akiitwa Lenard Mambo Mbotela,alikuwa ni balaa
 
Yeah mtoa mada hii u make my day,nchi ina heshima na adabu,ukipelekwa jela ni kwa makosa sio visasi vinavyofanyika sasa,watu wanapambikiwa kesi ambazo sio za kwao,Babu Seya ile kesi naamini haukuamuliwa kihalali,DNA TEST ingesaidia kuamua ukweli kuhusu ile kesi,watu hata kwenye dunia ya kwanza wanapanga foleni ni kitu cha kawaida,kipindi hicho our no 1 naye alikuwa anapanga foleni,mmmm Zeni 2017 babu kubwa ukija kwenye muziki wa asili au dansi kila kitu kilikuwa natural sio sasa wanamziki wakiimba lazima wabane pua zao,sikiliza natural voice ya Bitchuka,DEDE(RIP),N.K ,KIPINDI CHA MICHEZO kiliboreshwa zaidi na Abdul Masudi (RIP),yes kipindi hicho tumeishi maisha bora.
Achana na habari ya Babu Seya mbakaji,ongelea mambo mengine
 
Wakati huo tulikuwa tukisikiliza Radio Soroti ya Uganda na zile za Kenya kulikuwa na mtangazaji akiitwa Lenard Mambo Mbotela,alikuwa ni balaa

Kweli na aspro Job Isack Mwamto. Na kuna show za Marekani leo hii zinazofanana na kweli na aspro.
 
7558d6945394f104fd06fa86bafaf9a4.jpg


Mabrazameni walitumia viatu hivyo vilivyoitwa raizon.
 
Baba yako akisafiri kwenda nje ya nchi alikuletea raba mtoni utesee wanafunzi wengine shule. Nyerere hakuruhusu mtu auze raba mtoni ndani ya Tanzania. Ziliporuhusiwa kuuzwa baada ya Nyerere ndio viwanda vyetu vya viatu vikafa.
 
Sauti zilikuwa stereo nachurale hakuna kubana pua
 
Back
Top Bottom