Naibu Waziri Mahiza na kejeli kwa walimu

Ng'azagala

JF-Expert Member
Jun 7, 2008
1,286
221
Nilimsikia Naibu Waziri wa Elimu Mh Mwantumu Mahiza akiongea na wanafunzi wa ualimu kule Songea (source TBC Taifa jana jioni).
Aliulizwa kuhusu mishahara midogo wanayolipwa walimu. Alijibu kuwa wale wanafunzi wasioridhika ni mishahara ya ualimu watafute kozi nyingine ili wapate hizo kazi zinazolipa zaidi. Na pia hata wale walimu wasioridhika na mishahara pia watafute kazi nyingine na sio kufanya migomo, kwani hata wao (mawaziri nafikiri) wakigoma itakuwaje?

Nilisikitika mno na kauli ile na nilijiulizi hivi
Serikali na wananchi tunalalamika sana kuhusu uhaba wa waalimu na pia mishahara midogo wanayolipwa hawa wachache ukiacha na haki nyingi wanazonyimwa. Je huyu Naibu Waziri anapata wapi kiburi cha kuwaambia walimu watafute kazi nyingine zitakazo walipa?
Alisema walimu wananzia kulipwa kama laki mbili hivi ambazo hazijakatwa kodi. Je huyu Naibu Waziri ameshafanya kautafiti kuona kuwa hiyo inawatosha kuwafanya wasilalamike?
Huyu ni Naibu Waziri wa ELIMU ambaye tunamtegemea asimamie vizuri Elimu yetu wa Tanzania iliyojaa matatizo. Badala ya kuwapa moyo walimu wanaoumia kwa kulitumikia Taifa kwa kujitolea, angalau kwa kuwaahidi kushughulikia matatizo ya Elimu, sasa anaongea kama mtu wa kijiweni.
Sijui CV ya huyu Naibu lakini nafikiri tunamatatizo makubwa na uwezo wa baadhi ya mawaziri wetu.

Hizi kauli MBOFU MBOFU kutoka kwa viongozi wetu zitakoma lini?
 
nimesikitishwa sana na kauli zake..huyu ni miongoni mwa mawaziri hovyo kabisa
 
Kifupi huyu mama hana shule...mtu ani-prove wrong...nasikia alikuwa mwalimu wa shule ya msingi moja hapa jijini na haijulikani ni lini alijiendeleza kielimu...???@#$%^
 
Huyu mama alikuwa mwalimu mkuu msaidizi shule aliyokuwa anafundisha mama Salma Kikwete,mara baada ya JK kuchukua utamu wa nchi,Salma alimwomba mumewe ampe fadhila Mwantumu kwavile alikuwa anamsaidia kumwandikia 'notes' za masomo ya kufundishia wakati yeye Salma akiwa safarini na mumewe.Hivyo kilichotumika hapo ni fadhila na si kigezo cha elimu kilichomfanya JK amteuwe Mwantumu kuwa mbunge na baadae naibu waziri.
 
Jamani hawa ndo mawaziri wa Muungwana eti,Huyu mama ni mtu wa mtaani sana kwani hamjui kuwa mume wake ni swahiba wa mwenye nchi??Hana lolote la kuwaambia wananchi kumbukeni kesi ya Mnally kuwalamba waalimu viboko alisemaje huyu?
Waalahi nawaambia wanafunzi waliomuuliza hilo swali ni bora zaidi sana kuliko yeye kwenye upstairs !!!Ni waziri kidole juu tu hamna zaidi.
 
Inasikitisha sana, unajua watu husaha kuwa kila tulichonacho kimetoka kwa mungu, na kila binadam anahitaji maisha bora na si ili mradi, nadhani huyu mama mungua atamuona na kumuadhibu kivyake, na ikishindikana basi kizazi chake kitakiona cha moto. Walimu ndo chanzo cha WWW.JAMIIFORUMS.COM, je bila hao walimu wa shule za msingi kuwa wavumilivu tungefika hapa.
 
Kifupi huyu mama hana shule...mtu ani-prove wrong...1. nasikia alikuwa mwalimu wa shule ya msingi moja hapa jijini na haijulikani ni lini alijiendeleza kielimu...???@#$%^


1. nilidhani unaushahidi mkuu

2.ni kweli yawezakuwa hafai kulingana na maneno yako kama ufanisi wa mtu tunaupima kwa elimu peke yake lakini kiukweli nafikiri anauzoefu na wizara pamoja na nyanja yote ya ualimu na walimu ingawa ninaweza kukubali kwamba muda mwingine majibu anayotoa yanakuwa hayatoshelezi wapinzani.

unaweza kugonga kwenye link nitaiweka mwishoni kuona experience aliyonayo na kama unafikiri elimu ya kuwa na madegree pekee ndio kigezo basi kuanzia uhuru tungekuwa na raisi professor mpk sasa na kama La basi tukubali kwamba elimu pekee sio kigezo cha kumsiliba huyu mama. (Ni mawazo yangu tuu)

http://www.parliament.go.tz/bunge/mpcv.php?vpkey=321
 
Nilimsikia Naibu Waziri wa Elimu Mh Mwantumu Mahiza akiongea na wanafunzi wa ualimu kule Songea (source TBC Taifa jana jioni).
Aliulizwa kuhusu mishahara midogo wanayolipwa walimu. Alijibu kuwa wale wanafunzi wasioridhika ni mishahara ya ualimu watafute kozi nyingine ili wapate hizo kazi zinazolipa zaidi. Na pia hata wale walimu wasioridhika na mishahara pia watafute kazi nyingine na sio kufanya migomo, kwani hata wao (mawaziri nafikiri) wakigoma itakuwaje?

Nilisikitika mno na kauli ile na nilijiulizi hivi
Serikali na wananchi tunalalamika sana kuhusu uhaba wa waalimu na pia mishahara midogo wanayolipwa hawa wachache ukiacha na haki nyingi wanazonyimwa. Je huyu Naibu Waziri anapata wapi kiburi cha kuwaambia walimu watafute kazi nyingine zitakazo walipa?
Alisema walimu wananzia kulipwa kama laki mbili hivi ambazo hazijakatwa kodi. Je huyu Naibu Waziri ameshafanya kautafiti kuona kuwa hiyo inawatosha kuwafanya wasilalamike?
Huyu ni Naibu Waziri wa ELIMU ambaye tunamtegemea asimamie vizuri Elimu yetu wa Tanzania iliyojaa matatizo. Badala ya kuwapa moyo walimu wanaoumia kwa kulitumikia Taifa kwa kujitolea, angalau kwa kuwaahidi kushughulikia matatizo ya Elimu, sasa anaongea kama mtu wa kijiweni.
Sijui CV ya huyu Naibu lakini nafikiri tunamatatizo makubwa na uwezo wa baadhi ya mawaziri wetu.

Hizi kauli MBOFU MBOFU kutoka kwa viongozi wetu zitakoma lini?
nimeona taarifa hii,nilisikitika sana kuona mtu wa level yake anaweza kujibu kama mtu wa mtaani.....alikuwa na point kwa alichokuwa anakizungumza kwa maana ya kwamba nchi profession nyingi hazilipwi inavyostahili. lakini alivyojibu kwa kwa ukali ni kama vile anamjibu mwanae alikuwa anakaripia!!!!hii siyo sawa na haikubaliki hata kidogo. baadhi ya nukuu ni ''kwa mlio mwaka wa kwanza hamjachelewa ondokeni mkasomee kazi zingine na hata nyie wa mwaka wa pili badilisheni kazi mkafanye zinazolipa zaidi'' mawaziri kama hawa ni mzigo kwa serikali...
 
1. nilidhani unaushahidi mkuu

2.ni kweli yawezakuwa hafai kulingana na maneno yako kama ufanisi wa mtu tunaupima kwa elimu peke yake lakini kiukweli nafikiri anauzoefu na wizara pamoja na nyanja yote ya ualimu na walimu ingawa ninaweza kukubali kwamba muda mwingine majibu anayotoa yanakuwa hayatoshelezi wapinzani.

unaweza kugonga kwenye link nitaiweka mwishoni kuona experience aliyonayo na kama unafikiri elimu ya kuwa na madegree pekee ndio kigezo basi kuanzia uhuru tungekuwa na raisi professor mpk sasa na kama La basi tukubali kwamba elimu pekee sio kigezo cha kumsiliba huyu mama. (Ni mawazo yangu tuu)

http://www.parliament.go.tz/bunge/mpcv.php?vpkey=321

Nashukuru nimeiona hiyo link, elimu yake ni Diploma ya Chang'ombe, na kabla hajawa Waziri alikuwa headteacher wa Primary

Lakini kama alikuwa mwalimu, amepitia kwenye mazingira magumu sana na anajua hali ya huko, inakuwaje anakuwa waziri anatoa lugha mbovu hivyo? hapa TZ hakuna options za ajira nyingi namna hiyo naye anajua.

Wananchi tunapaswa kubadilika, mtu akitoa lugha kama hiyo tusikubali kirahisi.
 
Nashukuru nimeiona hiyo link, elimu yake ni Diploma ya Chang'ombe, na kabla hajawa Waziri alikuwa headteacher wa Primary

Lakini kama alikuwa mwalimu, amepitia kwenye mazingira magumu sana na anajua hali ya huko, inakuwaje anakuwa waziri anatoa lugha mbovu hivyo? hapa TZ hakuna options za ajira nyingi namna hiyo naye anajua.

Wananchi tunapaswa kubadilika, mtu akitoa lugha kama hiyo tusikubali kirahisi.

Point of Correction......Diploma ya Chang'ombe ni mwaka 1987 mkuu na baada ya hapo zilikuwepo nyingine tena zenye exposure ndani yake.

pili hakuwa headteacher kabla ya uwaziri kama ulivyosema mkuu alikuwa MWENYEKITI WA UMOJA WA WALIMU WAKUU WA SHULE ZA MSINGI DAR ES SALAAM NA SASA NI AFRICA MASHARIKI KWA UJUMLA WAKE
 
The fallacy of this hubris is not only in it's content, but also, and some would say even more, in it's delivery.

The inviting dilemma, of whether to be mad because the junior minister lacked common courtesy and diplomatic language among many other things, or to be happy that this woman is such a nincompoop to have exposed herself openly like a person undressed -to the dismay of Tanzania watchers- is obvious.

What if, in theory at least, all the teachers were to decide that the profession is not rewarding enough materially? What alternative does the bravura of this modern day Mary Antoinette offer?

Many of these aspiring teachers have no option for other employment opportunities.Isn't this our very own case of "If you don't have bread eat cake"?

As the saying goes, it would be funny if it wasn't so tragic.
 
alikua sahihi kabisa kuwaambia ukweli, tatizo sisi watanzania tunapenda sana kudanganywa, na mtu anaposema ukweli hapo hapo anaonekana mbaya. Aliwaambia vile makusudi ili wafanyane kitu kingine mapema kabla hawajaingia kwenye huo ualimu. Hebu niambie ni mangapi serikali imeahidi lakini hayajatekelezwa? Kwa mtazamo wangu ni bora mtu anieleze ukweli kuliko kunidanganya, sasa hata hao watakao ingia kwenye huo ualimu, wajue kuwa hauna mshahara mkubwa na hivyo hana haja ya kugom. Hata hivyo hebu niambie serikali mtumishi mwenye degree analipwa sh. ngapi? kama sio 308,000 ni ngapi? sasa wewe mwl. mwenye cheti unataka alipwe 500,000? tusiwe tunazungumza ilimradi kuzungumza, pia tunatakaiwa kuangalia na sehemu nyingine. hata hivyo mtu hata akilpwa 10,000,000 bado ataklalamika hazitoshi......... ni mtazamo wangu tu
 
Kama amepitia huko angetafuta jinsi ya kuwajibu walimu kwa kuwapooza na kuwapa moral wa kazi ngumuuu sana wanaifanya.....ila jibu alilotoaa atakuja kulijutiaa sana akija kutoka hapo alipobebwa na kuwekwa....ni ulimbukeni tuu...hakuna kingine
 
alikua sahihi kabisa kuwaambia ukweli, tatizo sisi watanzania tunapenda sana kudanganywa, na mtu anaposema ukweli hapo hapo anaonekana mbaya. Aliwaambia vile makusudi ili wafanyane kitu kingine mapema kabla hawajaingia kwenye huo ualimu. Hebu niambie ni mangapi serikali imeahidi lakini hayajatekelezwa? Kwa mtazamo wangu ni bora mtu anieleze ukweli kuliko kunidanganya, sasa hata hao watakao ingia kwenye huo ualimu, wajue kuwa hauna mshahara mkubwa na hivyo hana haja ya kugom. Hata hivyo hebu niambie serikali mtumishi mwenye degree analipwa sh. ngapi? kama sio 308,000 ni ngapi? sasa wewe mwl. mwenye cheti unataka alipwe 500,000? tusiwe tunazungumza ilimradi kuzungumza, pia tunatakaiwa kuangalia na sehemu nyingine. hata hivyo mtu hata akilpwa 10,000,000 bado ataklalamika hazitoshi......... ni mtazamo wangu tu
usisahau tu huyo mwalimu ndiye aliyekupa jeuri ya kuongelea degree leo hapa Jamiii Forum, so at least unaona umuhimu wake...........
either hujui chochote kuhsu maisha ya waalimu tanzania or u r dumb
 
alikua sahihi kabisa kuwaambia ukweli, tatizo sisi watanzania tunapenda sana kudanganywa, na mtu anaposema ukweli hapo hapo anaonekana mbaya. Aliwaambia vile makusudi ili wafanyane kitu kingine mapema kabla hawajaingia kwenye huo ualimu. Hebu niambie ni mangapi serikali imeahidi lakini hayajatekelezwa? Kwa mtazamo wangu ni bora mtu anieleze ukweli kuliko kunidanganya, sasa hata hao watakao ingia kwenye huo ualimu, wajue kuwa hauna mshahara mkubwa na hivyo hana haja ya kugom. Hata hivyo hebu niambie serikali mtumishi mwenye degree analipwa sh. ngapi? kama sio 308,000 ni ngapi? sasa wewe mwl. mwenye cheti unataka alipwe 500,000? tusiwe tunazungumza ilimradi kuzungumza, pia tunatakaiwa kuangalia na sehemu nyingine. hata hivyo mtu hata akilpwa 10,000,000 bado ataklalamika hazitoshi......... ni mtazamo wangu tu
Kwahiyo? Suggest, what should be done?
 
1. nilidhani unaushahidi mkuu

2.ni kweli yawezakuwa hafai kulingana na maneno yako kama ufanisi wa mtu tunaupima kwa elimu peke yake lakini kiukweli nafikiri anauzoefu na wizara pamoja na nyanja yote ya ualimu na walimu ingawa ninaweza kukubali kwamba muda mwingine majibu anayotoa yanakuwa hayatoshelezi wapinzani.

unaweza kugonga kwenye link nitaiweka mwishoni kuona experience aliyonayo na kama unafikiri elimu ya kuwa na madegree pekee ndio kigezo basi kuanzia uhuru tungekuwa na raisi professor mpk sasa na kama La basi tukubali kwamba elimu pekee sio kigezo cha kumsiliba huyu mama. (Ni mawazo yangu tuu)

http://www.parliament.go.tz/bunge/mpcv.php?vpkey=321

Hapa mkuu hakuna kitu, kutoka headteacher wa primary school to deputy minister!! aaaaah....

Mzee hapa lazima kuna jambo tu!!!!! Lakini ukweli unabaki pale pale kuwa ni klaza tu!!!
 
alikua sahihi kabisa kuwaambia ukweli, tatizo sisi watanzania tunapenda sana kudanganywa, na mtu anaposema ukweli hapo hapo anaonekana mbaya. Aliwaambia vile makusudi ili wafanyane kitu kingine mapema kabla hawajaingia kwenye huo ualimu. Hebu niambie ni mangapi serikali imeahidi lakini hayajatekelezwa? Kwa mtazamo wangu ni bora mtu anieleze ukweli kuliko kunidanganya, sasa hata hao watakao ingia kwenye huo ualimu, wajue kuwa hauna mshahara mkubwa na hivyo hana haja ya kugom. Hata hivyo hebu niambie serikali mtumishi mwenye degree analipwa sh. ngapi? kama sio 308,000 ni ngapi? sasa wewe mwl. mwenye cheti unataka alipwe 500,000? tusiwe tunazungumza ilimradi kuzungumza, pia tunatakaiwa kuangalia na sehemu nyingine. hata hivyo mtu hata akilpwa 10,000,000 bado ataklalamika hazitoshi......... ni mtazamo wangu tu

wewe ni pumbafu kabisa, huna tofauti na chiligati
 
Kama amepitia huko angetafuta jinsi ya kuwajibu walimu kwa kuwapooza na kuwapa moral wa kazi ngumuuu sana wanaifanya.....ila jibu alilotoaa atakuja kulijutiaa sana akija kutoka hapo alipobebwa na kuwekwa....ni ulimbukeni tuu...hakuna kingine

Mkuu heshima mbele, sijakupata sawa hapo kwenye bold..kwa maana angewadanganya au angewapiga siasa na kukwepesha ukweli ama...?
 
Back
Top Bottom