Nahofia kumwambia nampenda sababu anatokea familia ya kitajiri

Benfamous

JF-Expert Member
Oct 10, 2016
484
374
Salam wakuu leo nimekuja kuomba ushauri.

Kuna dem nimempenda sana lakini kwao wana pesa sana nimeanza mazoea nae kupitia WhatsApp na tunachat vizuri tu ila bado hatujawai kuonana ana kwa ana nataka nimwambie kwamba nampenda but nahofia anaweza nikataa kwasababu mimi natokea maisha ya kawaida sana sina hela kivile so hapa najiuliza nimwambie ili tu hata kama akikataa niwe nimeshamwambia coz nampenda kiukweli au niachane nae kwa kuhofia kibuti cha mtoto wa maisha bora.

Ushauri plz wakuu
 
haujaonana nae ana kwa ana unampenda sana na kwao wana pesa sasa tukushauri vipi ss hapo wakat wewe tu domo zege
 
Ukikua vzr utawelewa mapenzi yakojo endelea hvo hvo hyo ni stage
 
Mnapotezaje mda kukashauri ako kavulana ka form one angalia uandishi wake tu unatia kinyaa "tyu" ndo nini?
 
Salam wakuu leo nimekuja kuombaa ushauri.kuna dem nimempendaa sana lakini kwao wana pesa sana nimeanza mazoea nae kupitia WhatsApp na tunachat vizurii tyu ila bado atujawai kuonana ana kw ana nataka nimwambie kwamba nampenda but nahofia anaweza nikataa kwasababu me natokea maisha ya kawaida sana af sina ela kivilee so hapa najiuliza nimwambie ili tu ata kama akikataa niwe nimeshamwambia coz nampenda kiukwel au niachane nae kw kuhofia kibutii cha mtoto wa maisha boraaa
Ushauri plz wakuu

Jitahidi kutumia maneno kamili, lugha zingine ziishie kwenye chats.
Kama umekosa hela jiongeze sehemu zingine.
Acha kumuita demu kama kweli unampenda. Unaonekana una umri mdogo na mdada nae atakua mdogo kiumri, swala la pesa usilifikirie sana, muoneshe upendo wa kweli na atakukubali tu.
 
Salam wakuu leo nimekuja kuombaa ushauri.kuna dem nimempendaa sana lakini kwao wana pesa sana nimeanza mazoea nae kupitia WhatsApp na tunachat vizurii tyu ila bado atujawai kuonana ana kw ana nataka nimwambie kwamba nampenda but nahofia anaweza nikataa kwasababu me natokea maisha ya kawaida sana af sina ela kivilee so hapa najiuliza nimwambie ili tu ata kama akikataa niwe nimeshamwambia coz nampenda kiukwel au niachane nae kw kuhofia kibutii cha mtoto wa maisha boraaa
Ushauri plz wakuu
andika vizuri sisi wengine ni baba zako hatuelewi hizo rejesta na misimu yenu
tyu...af...plz...hizi ni rejesta wapi??
coward
 
We umejuaje kama kweli kwao mboga saba, usiamini kila unalosikia.
Halafu huo mwandiko wako hauna viwango
 
Back
Top Bottom