Nahodha: Iko siku CCM itang'olewa

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
302
  • Akumbusha wajibu wa viongozi kwa wananchi
na Mwandishi Maalum, Mererani

Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha amewataka wana CCM kuacha kujidanganya kwamba chama chao kitaendelea kutawala milele.

Nahodha, mmoja wa viongozi wa juu wa CCM na serikali alitoa kauli hiyo jana wakati akiwahutubia wananchi wa Mererani wilayani Simanjiro mkoani Manyara.


“Ninatofautiana kimtazamo na watu wanaosema kwamba CCM itaendelea kutawala milele na milele, hapa kama hatutajipanga vizuri ipo siku chama chetu kitang’olewa madarakani…tusibweteke,” alisema Nahodha.


Akitoa mfano, Nahodha aliwataka wana CCM kujifunza kutoka katika nchi jirani ambako baadhi ya vyama vilivyopigania uhuru kama ilivyo CCM vimeng’olewa madarakani. Alikitaja chama cha Kenya African National Union (KANU) ambacho kilipigania uhuru wa Kenya kuwa mmoja wa vyama vilivyopata kung’olewa madarakani.


“Kumbukeni namna ambavyo KANU ilisambaratika kule Kenya… leo hii imesahaulika kabisa. Lakini si huko tu, kule Zambia (UNIP) na Malawi (MCP) vyama tawala vilibwagwa vibaya na sasa vimesahaulika masikioni mwa wananchi,” alionya Nahodha.


Akiendelea, alisema ni wazi ipo siku wananchi wanaweza kukichoka CCM na kukibwaga iwapo viongozi watashindwa kutimiza ndoto za wananchi za kuwaletea maendeleo.


My take:
Sasa ni ukweli uliowazi kwamba hata viongozi wakuu wameanza kusema ukweli tofauti na zamani ambapo ilikuwa ni nadra sana kusikia maneno kama haya ukimtoa Baba wa taifa aliyekuwa akiwaambia ukweli.
 
Penye ukweli uongo hujitenga, na lisemwalo lipo, kama halipo laja.

Mara nyingine umuhimu wa kuwa na viongozi vijana unaonekana, hawa viongozi vijana wanajua kuwa wataishi na maamuzi ya uongozi wao kwa miaka mingi ijayo, kuna baadhi ya wazee wetu wanajihesabia miaka yao michache tu hata hawajali.
 
Tatizo nadhani sio chama gani kipo madarakani, bali ni mfumo upi unaotawala ambao unaeza kuisaidia nchi kusonga mbele, ukweli ni kwamba with current system, kubadilisha chama ni sawa na kumtoa sultan mmoja na kumueka mwingine, as simple as that. Kama mnabisha angalieni yaliyotokea Zambia kwa Chiluba, na Kenya kwa NARC et al. IMO,Hakuna lolote la maana kwene hii thread.
 
Tatizo nadhani sio chama gani kipo madarakani, bali ni mfumo upi unaotawala ambao unaeza kuisaidia nchi kusonga mbele, ukweli ni kwamba with current system, kubadilisha chama ni sawa na kumtoa sultan mmoja na kumueka mwingine, as simple as that. Kama mnabisha angalieni yaliyotokea Zambia kwa Chiluba, na Kenya kwa NARC et al. IMO,Hakuna lolote la maana kwene hii thread.

Hiyo "hakuna chochote cha maana" imejumuisha na ulichoongea wewe? Au kwa yaliyoongewa kabla yako tu?
 
Penye ukweli uongo hujitenga, na lisemwalo lipo, kama halipo laja.

Mara nyingine umuhimu wa kuwa na viongozi vijana unaonekana, hawa viongozi vijana wanajua kuwa wataishi na maamuzi ya uongozi wao kwa miaka mingi ijayo, kuna baadhi ya wazee wetu wanajihesabia miaka yao michache tu hata hawajali.
Kiranga,
Ujana si panacea. Waangalie akina Ngeleja, akina Masha. Hawa kweli unaweza kusema kuwa ni viongozi wenye vision wanaoweza kuisukuma Tanzania kwenye neema?
I don't think so.
 
Hiyo "hakuna chochote cha maana" imejumuisha na ulichoongea wewe? Au kwa yaliyoongewa kabla yako tu?
I assume hujaelewa post. Sio kazi yangu kupost vitu mara mbili, ku-elaborate au kuexplain myself to anyone, unless nipo kwene mood.
 
I assume hujaelewa post. Sio kazi yangu kupost vitu mara mbili, ku-elaborate au kuexplain myself to anyone, unless nipo kwene mood.

Namna hii huwezi kueleweka, na ukishindwa kueleweka unapoteza ushawishi. Kama wewe ni demigod kiaina hiyo then haina maana kuja hapa kwenye forum kuwasiliana na sisi mere mortals, tutashindwa kukuelewa iwe shida tu, kaa kimya tu.

Ama sivyo, tukikuuliza swali una wajibu wa kujieleza.

When u assume u make an ass of u and me

Swali dogo tu, unajikanyaga tayari.
 
Namna hii huwezi kueleweka, na ukishindwa kueleweka unapoteza ushawishi. Kama wewe ni demigod kiaina hiyo then haina maana kuja hapa kwenye forum kuwasiliana na sisi mere mortals, tutashindwa kukuelewa iwe shida tu, kaa kimya tu.

Ama sivyo, tukikuuliza swali una wajibu wa kujieleza.

When u assume u make an ass of u and me

Swali dogo tu, unajikanyaga tayari.

Like I said, hakuna social code ya kimjadala wala written rules kwamba nijieleze marambilimbili. Nipo kwa forum kwa ku-exploit uhuru,muda na nishati yangu, at my own pleasure and intent..Narejea tena siwajibiki kutoa ufafanuzi wowote kwa yeyote.
 
Kiranga,
Ujana si panacea. Waangalie akina Ngeleja, akina Masha. Hawa kweli unaweza kusema kuwa ni viongozi wenye vision wanaoweza kuisukuma Tanzania kwenye neema?
I don't think so.

Jasusi,

By no mean did I imply that they have a vision, the idea of a "vision" -I am so glad you mentioned it- is so foreign, hata waliokuja na visions zao inabidi wazibwage na ku "go with the flow"

Once in a million times they get it right, whether by design, happenstance, coincidence au Machiavellian machinations.

Naona kama ni rahisi kwa hawa vijana - with all their flaws, Rose Garden shenanigans and ATM fracas- kukubali ukweli kuliko wazee.

Kama haya maneno yako accurate, Nahodha amesema kitu unprecedented by CCM mortals , so far mtu pekee aliyewahi kusema kitu chenye akili za "country first CCM second" in this style ni Nyerere, sikumbuki mwingine, labda mnisaidie wakuu.

To be fair Mwinyi naye amenifurahisha juzi alipomlipua KIkwete kwenye hadhira pale Feza mbele ya watoto na wageni wa kimataifa. Naona anachukua gravita ya elder statesman na ku rise above party politics

Huyu jamaa kaongea essentially kwamba CCM is not infallible, ni kama mkatoliki kusema "Papa usijisahau" implyinmg that the Pope is not infallible contrary to Catholic doctrine, Nahodha anasema in fact CCM is prone to "kujisahau". Rather vague and non-specific, lakini katika nchi yenye kusujudia chama kama Communist China hii kauli ni kubwa kuliko ilivyokuwa reported.

Hususan ukizingatia kuwa wenyewe ndani ya CCM wanaweza wasiipende kwa kuona kama jamaa anawachulia.But "none a dem can fight the hands of time".

Somebody mentioned entropy earlier today, this is it at work. Any closed system will always move from amore ordered to a less ordered state. THat is an undisputable truism.Just as the arrow of time in this space-time continuum always move forward, and never backwards.

Ushawahi kulala usiku wa leo na kuamka asubuhi ya jana? Haiwezekani.
 
HIZI NI FACTS, Nina imani amesoma alama za nyakati na kuanza kutoa unabii. KWA KAULI HII NAM HALI INAVYOENDELEA WANAPASWA CCM WAJIANDAE KUONDOLEWA MADARAKANI, WASIWAKAHAMAKI NA KUWA CHANZO CHA VURUGU KWA KUNYANG'ANYWA MKATE KINYWANI.
 
kuondoka kwa C C M ni swala ambalo lipo mikononi kwa watanzania, ikafika sehemu watanzania hawataki tena kuongozwa na viongozi wahuni wanao wakejeli na kuwasemea vibaya wafanyakazi, mafisadi, waizi na watu wanaojijali wenyewe tutafikia lengo la kuing!oa C C M,

KEEP IN MIND SIO KAZI RAISI SAAAANA, C C M INA BASE TOKEA KIPINDI CHA UHURU NYERERE WAS VERY BRAVE, HE GAVE EACH AND EVERY THING TO THEM KIPINDI VYAMA VINGI VINAANZISHWA, SO THEIR RICH,
 
Nadhani wanaweza kukubaliana na mie kuwa sasa dalili ya mvua ni mawingu na dalili ya CCM kupasuka tunaanza kuiona vema umelisema nahodha maana najua unalijua hilo
 
Saaaaaaaafi Vuai, viongozi wenzako wanajidanganya kuwa CCM watatawala milele, hizo ni ndoto na mwaka huu ndio mwisho wao.
 
kuondoka kwa C C M ni swala ambalo lipo mikononi kwa watanzania, ikafika sehemu watanzania hawataki tena kuongozwa na viongozi wahuni wanao wakejeli na kuwasemea vibaya wafanyakazi, mafisadi, waizi na watu wanaojijali wenyewe tutafikia lengo la kuing!oa C C M,

KEEP IN MIND SIO KAZI RAISI SAAAANA, C C M INA BASE TOKEA KIPINDI CHA UHURU NYERERE WAS VERY BRAVE, HE GAVE EACH AND EVERY THING TO THEM KIPINDI VYAMA VINGI VINAANZISHWA, SO THEIR RICH,
Lipo jambo moja ambalo ni uhakika nalo juu anguko lao, nalo ni kwamba laana ya uasi wa mafundisho na miongozo makini ya JKN et al iko juu yao. Bahati mbaya zaidi kwao ni kwamba hata hajutii matendo yao wala hawana mpango wa kufanya toba ya kweli.
 
Nakumbuka enzi zile za mwalimu tukikiua unapofanya kosa mbele ya wakubwa hata kama si wazazi wako unaadhibiwa na hauna fursa ya kusema home, lakini mpige mtoto wa siku hizi kama hakukupeleka polisi.

Sasa ssiemu tatizo linaanzia kwa mwenyekiti wake, hapendi uikosoe,umkosoe na wapinzani anawaona maadui wakubwa, na iwapo utaonekana unamuonekano wa kiupinzani utakula jeuri yako na hiyo sio sasa ila toka yupo waziri wa nje, kuna profesa maarufu alikua muhadhiri wa chuo cha diplomasia alimfukuza kazi ati kisa alikwenda ukonga kumsalimia mwenyekiti wa chama kimoja wapo cha siasa ambae ni mwanzuoni mwenzake.

Hivyo kwa kauli hii ya nahodha nina wasiwasi kama hataitwa dodoma kujieleza kwani mwenye mtoto wake hataki mwanae asemwe vibaya, lakini tuombe mungu ipo siku maneno yatatimia
 
siku hiyo iko karibu na itakuja kama surprise. hata hawatakuja waamini kama ilivyokuwa KANU kenya tu. lets get together kuking'oa chama hiki.
 
siku hiyo inakuja kama mwivi ajavyo, hawataamini macho yao, itakuwa surprise kubwaaa bila hata kutegemea.
 
Tatizo nadhani sio chama gani kipo madarakani, bali ni mfumo upi unaotawala ambao unaeza kuisaidia nchi kusonga mbele, ukweli ni kwamba with current system, kubadilisha chama ni sawa na kumtoa sultan mmoja na kumueka mwingine, as simple as that. Kama mnabisha angalieni yaliyotokea Zambia kwa Chiluba, na Kenya kwa NARC et al. IMO,Hakuna lolote la maana kwene hii thread.

Umenena Abdul: sasa hivi mfumo wa utawala uingereza unapigiwa kelele na unataka kubadilishwa, hasa ktk namna ya kuendesha uchaguzi. hata hivyo Brown jana katangaza kuwa siyo tu atastep down as party leader (kutokana na chama chake Labour kushindwa uchaguzi) bali pia hata-support candidate yeyote atakayewania nafasi yake. Ingekuwa nchi zetu hizi za Kiafrika huyo huyo angeng'ang'ania tu hadi inazuka civil war.
 
Back
Top Bottom