Nahitaji program ipi ntengeneze game kama fifa 14

Nahitaji program ipi ntengeneze game kama fifa 14

Kwanza kabisa hatuna capital ya namna hiyo, Fifa probably inacost around $100 milion kuitengeneza. Pili hakuna workforce yenye skills hizo hapa Tanzania na hakuna local market pia.

Tatu, industry ya gemu ni ngumu sana kupata mafanikio, hata ningekuwa ninayo hiyo 100 million nisingeingia humo, kwa kila hit video game unayoijua kuna 1000 of games ambazo hazikutengeneza hata centi.
Na hata waliotengeneza game ikiwa hit mara nyingi they don't make it financially kwa sababu ya costs kubwa.

Midway, watengenezaji wa Mortal Combat, NBA Jam
Zipper, watengenezaji wa SOCOM Navy seals
Barking Dog- Max Payne 3
THQ - UFC Undisputed

Wote hao wako bankrupt au washakufa kabisa.
nimekwelewa mkuu!!! lakini si lazima iwe fifa!! je ni gemu gani au softwares gani zimetengenezwa tz na zinatumika kama ilivyo kwa windows na nyinkginezo???
 
Siiyo kwamba kwa vile wameeleza jinsi ya kutengeneza hizo game ukafikiri ni kitu rahisi.
hata kama si kitu rahisi...je ni kitu gani kimetengenezwa ambacho sio complicated kama hizo games?? walau na sisi tuwetunangojea software au any application let say ya juakali itoke mwakani???!! au tunangojea vya nje!!!
 
hata kama si kitu rahisi...je ni kitu gani kimetengenezwa ambacho sio complicated kama hizo games?? walau na sisi tuwetunangojea software au any application let say ya juakali itoke mwakani???!! au tunangojea vya nje!!!

kijana listen, hii system ni a bit complicated. Ntaongelea myself as an example. Suala sio capital tu like what most people said, mimi kama umesoma my previous comment hapo juu i used to make games, nilikua natengeneza like level 1 au 2 tu ya hivi vigame vidogo vidogo tu i loved it sana, i was so determined nilikua najifunza mpaka kuandika script mwenyewe (mind you nilikua form two at dat time, zamani sana) ila baada ya kukosa both support and necessary education, well nikaachana nayo na kubaki na animate just for fun of it(maana its the closest thing, to that). Sikuhizi nikimaliza all my work i just sit around and make stuff like this
.
https://docs.google.com/file/d/0B4V7QyehEzrRV3hwUXlUc3BHSlU/edit?usp=sharing
.

Naamini kama 'ningepataga' like support and stuff i would have became greatest animator hapa ila ndo hivo, i just do it for my own entertainment. Nnachosema hapa ni kua System yetu haiko both supportive and conducive kwa hiyo industry.
 
hilo ndilo jibu mengine mbwembwe!!! naamini wataalam wa kompyuta wapo wengi sana humu nchini, lazima tukubali ukweli na tuache visingizio mara najua afu kuteneza sijui sasa mnajua nini??? maswala yakuwekea watu windows na kuformat pc i mambo yalishapitwa na hata mtoto wa la saba anaweza fanya iyo kazi, embu tuamke wakuu maana hili tatizo sio kwa wataalamu kompyuta tu na wengine pia wanahusika kila mmoja katika nafasi yake.

Bongo hakuna kitu hapa. Ukiona mtu anajifanya anaijua sana computer/simu na mambo yake ujue yeye ni mtaalam wa kuGoogle. Mtoto wa darasa la saba leo hii anaweza akaInstall Windows/Linux kwenye computer as long as anajua namna ya kuGoogle.

Umeomba uwekewe link ya game yeyote ya mtanzania ya angalau 2D kuna mtu aliyekuwekea?! Unataka uthibitisho gani tena?! Mimi mwenyewe ninajua mambo mengi sana kuhusu computer/simu na hakuna utakachoweza kunidanganya kwasababu ninajua kuGoogle.

Unapokuja kwenye reality kama hiyo ya kutengeneza game Google inakaa pembeni hapo ndiyo akili inapotakiwa ifanye kazi.

BTW, Watanzania tunajulikana kwa kuwa na maneno mengi bila ya vitendo.

Na mimi ninaomba niwekewe link ya game "yoyote" ya Mswahili mkazi wa hapa Tanzania.
 
kijana listen, hii system ni a bit complicated. Ntaongelea myself as an example. Suala sio capital tu like what most people said, mimi kama umesoma my previous comment hapo juu i used to make games, nilikua natengeneza like level 1 au 2 tu ya hivi vigame vidogo vidogo tu i loved it sana, i was so determined nilikua najifunza mpaka kuandika script mwenyewe (mind you nilikua form two at dat time, zamani sana) ila baada ya kukosa both support and necessary education, well nikaachana nayo na kubaki na animate just for fun of it(maana its the closest thing, to that). Sikuhizi nikimaliza all my work i just sit around and make stuff like this
.
https://docs.google.com/file/d/0B4V7QyehEzrRV3hwUXlUc3BHSlU/edit?usp=sharing
.
Naamini kama 'ningepataga' like support and stuff i would have became greatest animator hapa ila ndo hivo, i just do it for my own entertainment. Nnachosema hapa ni kua System yetu haiko both supportive and conducive kwa hiyo industry.

Mkuu mbona kwa ulichokifanya kwa bongo sio kitu kidogo, kama umeweza fika hapo ni mwanzo mzur na unaweza tafuta hadith ambayo itaeleweka mwanzo mwisho.

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
mkuu si kwamba hakuna games zilizotengenezwa na watanzania, zipo ni games ndogo na hazivutii kucheza
Mimi nimeanza ona games zilizotengenezsa na mbongo kitambo kidogo nakumbuka ilikuwa mwaka 2005 nadhani katika pitapita zangu
nilikutana na kiwebsite cha jamaa mmoja anaitwa George Buliki kilikuwa na magames na ndiyo mara ya kwanza naona kijana mdogo ametengeneza website nilishangaa sana.
Ninapoongelea suala la capital mkuu coding is not all that is needed kwamba ukae na computer yako nyumbani basi uanze ku code. Ili kuleta reality kuna mambo mengi yanahitajika.
Mfano Fifa ni game la mpira hivyo lazima watakuwa na team ya watu wanaojua vizuri sheria za mpira bila kubahatisha.
Kutakuwa kuna research zinafanyika kabla ya kutengeneza hilo game na zitakuwa zinawa cost millions of dollars zaidi hata ya kutengeneza movie.
Kuna watata wa programming pale utawakuta ni itakuwa ni team kubwa si mtu mmoja afanye Programming ya game lote haiwezekani.
Utakuta wataalamu wa graphics wengi tu nadhani unaweza kuona kuwa ni kazi kubwa kutengeneza avatars za watu wote wale na japo ni vi cartoon lakini vibehave na kufanana na watu halisi.
Mkuu si kwamba hapa Bongo hakuna watu wanaojua lakini vitendea kazi na support ni ndogo sana, na mtu anakuwa hayukpo sure kama ata invest ela yake itarudi maana kutengeneza game jambo moja je litauzika.
Wenzetu wako mbele zaidi yetu na wanajua marketing ndiyo maana unaona kitu kama whatsapp kimeanzishwa marekani lakini haikuchukua muda mpaka wewe leo unaitumia, where did vodacom tanzania's the grid go?
Did anybody in USA or India ever hear of it?
Ona Instagram imeanzishwa juzi tu na haina lolote la maana lakini on ailivyo famous.
Mkuu jaribu ku google upate video uone game zinavyotengenezwa utakubariana na mimi kuwa kibongo bongo ni vigumu sana ni sawa na studios zilizotengeneza movie ya avatar mkuu.
Ningekuwekea games ambazo wabongo walishatengeneza lakini bahati mbaya sina link, lakini making flash games wengi wanatengeneza tu for fun ndiyo maana utazikuta kwenye pc zao tu.

nimekubaliana na wewe 100%!!! kinachonishangaza hata kama ukisema ni capital, unatarajia utapewa 1bil kwa mkupuo?? je wewe kama wewe ushajaribu au ushatengeneza game gani afu ukakosa capital???

unaposema timu kubwa una maanisha nini mkuu?? kama ni watu, je ni wangapi wapo tokea Tanzania inapata uhuru mpaka leo na kipindi chote hicho hiyo timu haijatimia??

ni sawa, siwezi kataa!! na je hilo gemu lililotengenezwa na mtu mmoja liko wapi??? kama unaweza nipatia link walau nione itakua bora zaidi!!
sio kwamba nataka bishana na wewe/nyie, ila inasikitisha sana kuona wataalamu tunao(japo sio wa kompyuta tu) lakini mpaka leo hatugungua hata kaflash disk ka 1byte tunangojea tu wazungu watuletee na tukikesha kubisha mara huyu ni bora kushinda yule wakati hamna lolote!!!
 
nimekwelewa mkuu!!! lakini si lazima iwe fifa!! je ni gemu gani au softwares gani zimetengenezwa tz na zinatumika kama ilivyo kwa windows na nyinkginezo???

Calculator ya division kwa o level na a level ya nyasiro pamoja na kasuku media player ya stefano.

Hio ni mifano ya humu ndani, ukienda store za microsoft., google na apple unakuta pia software za wabongo
 
Hata uishi miaka 1000 hutaweza kuitengeneza! Game kama fifa ina lines of codes kama million 4 na ww huwez kuandika hata 10000 kwa mwaka mzima! Its team work and mostly improving from past versions(bug fixing) and mordezing(quality and reality)
 
Hata uishi miaka 1000 hutaweza kuitengeneza! Game kama fifa ina lines of codes kama million 4 na ww huwez kuandika hata 10000 kwa mwaka mzima! Its team work and mostly improving from past versions(bug fixing) and mordezing(quality and reality)

Kaka miaka kama 15 iliopita tulikua tuna 8 bit games kama super mario zilikua ngumu sana ila leo kuna tools unatengeneza game kama lile ndani ya siku.

Technology inavyokua miaka 20 ijayo fifa litatengenezwa ndani ya siku na fifa la mwaka huo maybe lina line milion 400 watu watadhan kama ni imposible kulitengeneza alone
 
Watu wanatengeneza softwares kwa ajili ya makampuni, nadhani umeshaona kampuni nyingi zinafunguliwa hapa kwa ajili ya software development.
Kuna mtu humu alipost trial version ya software yake yakupanga matokeo ya mashule.
Lakini tatizo ndiyo hilo marketing ni ndogo tofauti na wenzetu, pia hata serikali haitilii mkazo uvumbuzi wa hapa ndani. Mfano mdogo ni veta wanavumbua vitu vingi utaviona kwenye maonyesho lakini after that utaskia viko stoo.
Enzi za mkapa udsm waliwahi tengeneza mashine wakazipa jina la makufuri 1 na makufuri 2 ni mashine za kukandamiza barabara. Sikusikia zimeishia wapi serikali ina import vitu toka nje hata masofa tu itakuja kuwa software.
Mtu anaona bora atumie office ya microsoft si ya mbongo, sasa hii inawafanya programmers wasione umuhimu wa kutengeneza vitu ambavyo havitanunulia isipokuwa kwa order maalumu.
Watu tunapenda vya bure, wewe ni mara ngapi umenunua software au game? Almost softwares tunazotumia ni pirated.
Hii ina discourage programming. Humu kuna watu wanajua nadhani ulisikia project ya kasuku, na nyingine nyingi tu kama we mfuatiliaji we wadhani watu kwanini wana run ma linux kwenye pc zao.


hata kama si kitu rahisi...je ni kitu gani kimetengenezwa ambacho sio complicated kama hizo games?? walau na sisi tuwetunangojea software au any application let say ya juakali itoke mwakani???!! au tunangojea vya nje!!!
 
Calculator ya division kwa o level na a level ya nyasiro pamoja na kasuku media player ya stefano.

Hio ni mifano ya humu ndani, ukienda store za microsoft., google na apple unakuta pia software za wabongo
Kwani O-Level na H-Level calculator zao zina tofauti gani na hizi zilizopo online? UKitaka fanya biashara andika kitu unique otherwise kila siku tutazidi kupiga kelele software za wabongo hazina soko.
 
Tuache kutafuta wachawi tatizo kubwa ni elimu yetu, ubunifu ZERO kabisa, unapoiga kitu kilichogunduliwa na wengine utauza wapi hizo products zako?
 
Kwani O-Level na H-Level calculator zao zina tofauti gani na hizi zilizopo online? UKitaka fanya biashara andika kitu unique otherwise kila siku tutazidi kupiga kelele software za wabongo hazina soko.


Ni tofauti inajumilisha, inatafuta wastani halafu inaipa kila maksi grade kama ni a, b, c na kuendelea then mwisho ina analyze hizo grade na kutoa division ya mwanafunzi kwa one click

Kizuri zaidi inapanga matokeo kiasi unaweza kuyaprint grade za mwanafunz, marks na division vikaonekana.

Imetengenezwa full optimised kwa grade za kibongo
 
Ni tofauti inajumilisha, inatafuta wastani halafu inaipa kila maksi grade kama ni a, b, c na kuendelea then mwisho ina analyze hizo grade na kutoa division ya mwanafunzi kwa one click

Kizuri zaidi inapanga matokeo kiasi unaweza kuyaprint grade za mwanafunz, marks na division vikaonekana.

Imetengenezwa full optimised kwa grade za kibongo
Point yangu kubwa hapo ni utofauti lakini maelezo yako sijaona tofauti yoyote kwani almost software yoyote iliyoandikwa kwa matumizi ya mahesabu inaweza fanya kila kitu ulichoeleza hapo juu.
 
Mkuu hiyo calculator si calculator ya kawaida, ni software ya kufanyia calculation ya matokeo ikiwa na maana kwamba mtu anafanya kujaza marks za kila somo la mwanafunzi yenyewe itajumulisha marks, itoe average, grades, mpaka division ya kila mwanafunzi. Mwalimu anakuwa hana haja ya ku calculate hayo yeye ni kuingiza marks tu

Point yangu kubwa hapo ni utofauti lakini maelezo yako sijaona tofauti yoyote kwani almost software yoyote iliyoandikwa kwa matumizi ya mahesabu inaweza fanya kila kitu ulichoeleza hapo juu.
 
Waheshimiwa Good Guy, Kang na wengine kama middlebopper...maelezo yenu ni mazuri sana kiasi kwamba hata mimi nnaejua kidogo kuhusu kompyuta nimeelewa ni kwa namna gan hizi games zinatengenezwa!!! Kinachonichanganya ni kwamba inakuaje mnajua yote haya na sijawahi sikia(wenda vipo) kuna gemu au kitu kingine kimetengenezwa hapa kwetu?? Na sisi tiwe tunangojea mtoe fifa 16 au 14!! Mnaojua na tusiojua wote tunangoja wamarekani na wazungu watengeneze na sisi wote ndo tutumie!! Sasa hapa kuna tofauti gani nyie mnaojua na sie tisio jua?? Au mnangoja siri-kali iwawezeshe!??

mkuu issue kubwa inayotusumbua watanzania ni kutaka kufanya vitu tulivyovizoea mfano umesomea comptr science lakn ukigraduate unataka ukafanye kazi voda,tigo etc, watu hawapendi kuwaza nje ya boksi ukicheki watu wasio na jobs ni wengi ni kujiorganize na kufanya kaoffice ka kizushi, kenya wanatoa funds kwa watu wanaojishughulisha na games kwny smartphones, mf. Mwaka jana walitoa kwa jamaa wa Uganda tatizo nimesahau websites za hizo fundings ni kua na interest tu hakika uwezo wa kutengeneza upo..capital ni elimu na knowledge ya wapi ukaombe funds over
 
Last edited by a moderator:
Pamoja na kuwa LORDVILLE anaweza asiwe sahihi sana specifically kwa suala la kutengeneza game lakini hoja na dukuduku lake bado ni la msingi sana.

Leo ntawasema watu wa kada hizi...

Animators:

Vijana wa kitanzania wengi wetu tunapenda sana "masifa" ya kukimbilia mitandaoni bila kuweka bidii stahiki katika kujifunza masuala. Kuna mambo hayahitaji fund ili kuyafanya vizuri... hata fund pia hupatikana penye ishara ya ubora. Animation nzuri kwa level ya Shrek inatengenezeka Tanzania angalau kwa urefu wa dakika tano (mtengenezaji mmoja).... lakini je ni wangapi hapa Tanzania ambao badala ya kuwekeza katika ubora na kutengeneza kitu kizuri kifupi (ndipo wasaidiwe) wao wanakimbilia kutengeneza kazi ndeeefu amabayo ni chini ya kiwango?? Halafu haooo mbio mitandaoni kujisifia. Ukiwakosoa unaitwa hater au huna uzalendo. Uzalendo katika mambo ya kitaalmu??

Web designers (wengi mpo humu):
Wadau wengi humu wanaojitangaza kutengeneza websites au social networks wanaappear kuwa technicians... designs zao ni mbaya sana interms of visual appeal.. hazivutii kabisa....hii haihitaji fund.

Wapo mabingwa humu akina Kang, chief-mkwawa na wenzao.. we demand more from you guys.. siyo kila siku mnalalamika oooh Wakenya oooh Wahindi...

Yapo mambo ambayo ni ndani ya uwezo wetu... Wazee tukaibe kazi Kenya, Burundi, China, Morocco, Marekani, Chile... popote. Tuwanyang'aye kazi Wakenya, Wazungu, Wahindi.......

Kwanini sisi kila kitu hatuwezi??? Fund, fund, fund......!! What the....!!

Haya sasa, wenye interest na gaming sasa angalau waanzie na UNITY 3D aliyopendekeza Kang.. japo kwa taabu lakini atakayefanya bidii ataweza kutengeneza game nzuri kuliko zote zilizowahi kutengenezwa Tanzania hadi leo dakika hii naweka nukta hapa.

Asante LORDVILLE, unaweza usiwe sahihi kwa kila kitu lakini ni kweli wengi wetu sisi ni wapiga porojo na walalamikaji... well tunaye wa kumsingizia: SERIKALI.

Kama kwa knowledges walizonazo Kang na chief-mkwawa hawajafanya lolote (la maana (sitaki hoja za "maana ni relative")) hadi sasa kinachofuata ni kuwavua uraia tu (Operesheni Kimbunga).
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom