Nahitaji msaada wa mawazo ya biashara/ujasiriamali

Mtoto wa kaka yangu alifeli kidato cha 4. Nataka nimfungulie ofisi. Je, kati ya saluni ya kiume na biashara ya mitumba ipi inalipa vizuri? Kiasi ninachotaka kumpa ni Tsh 3,000,000/. Na kama mtaona(wana-jf) kuwa labda hicho kiasi hakitoshi, naomba mnipe wazo mbadala ili tumuokoe kijana huyu. Maana amekosa uelekeo kabisa.

Biashara ni Elimu. Wengi wetu hunachukulia siku zote kufanikiwa kwenye biashara ni kama ngekewa hivi! Kumuingiza kijana kufanya biashara bila kuyajua vema mazingira ya biashara itarajiwayo lazima mwanzo apige mieleka mingi tu maana anakuwa anajifunza kwa makosa! Asipokuwa mvumilivu anabwaga manyanga.

Ushauri wangu mkishakubaliana nae juu ya aina ya biashara atakayoipenda yeye mwenyewe, mwombee akajishikize kwanza awe kama msaidizi kwenye hiyo kazi iwe ni saluni, mgahawa, kilimo au mitumba! Akajishikize kwanza miezi 3 hadi 6 hata kama ni kwa kujitolea au kwa yeye kulipia kitu kidogo! Huu ni mtazamo ambao wengi hawajauchangamkia. Atakapokuwa amejishikiza atajifunza mambo mengi sana kiasi kwamba utakapoamua sasa akasimame mwenyewe hiyo aina ya biashara uhakika wa yeye kusonga mbele utakuwa mkubwa. Ndiyo maana Mkuu Chasha alishadokezea kuwa, mtu mwenye taaluma fulani ni rahisi kufungua biashara kulingana na taaluma yake maana anajua mambo mengi yanayoendana na kitu hiyo.
 
Mi ninashauri Kama wapo moshi afuge sungura kwani wanalipa sana.na mbegu Nzuri inapatikana kenya
 
Mtu hufanikiwa zaidi akifanya kile ambacho anakipenda kutoka moyoni,muulize kile anachoweza kukifanya kisha kiangalie kama kina mantiki na kinaweza kumfikisha ktk hatua nyingine kimaisha.
 
wana jamii forum naomba ushauri mimi ni mwajiriwa ktk restaurant kama mpishi,sasa nataka kujiajiri ,kufungua mgahawa wenye uwezo wa wageni wa kukaa kama watu kumi na tano ,na natarajia kuuza bites na juices na soda bites ni kama cakes,samosas,pizzaz biscut home made,huo ni ufupi tu wa bidhaa zangu,je ni biz yenye mafanikio?ushauri p'se
 
wana jamii forum naomba ushauri mimi ni mwajiriwa ktk restaurant kama mpishi,sasa nataka kujiajiri ,kufungua mgahawa wenye uwezo wa wageni wa kukaa kama watu kumi na tano ,na natarajia kuuza bites na juices na soda bites ni kama cakes,samosas,pizzaz biscut home made,huo ni ufupi tu wa bidhaa zangu,je ni biz yenye mafanikio?ushauri p'se

mkuu ... hakika umelenga .... hii biashara ina high demand usirudi nyuma ... anza mara moja kwa kuanza kukusanya vifaa huku ukiwa unatafuta sehemu
 
wana jamii forum naomba ushauri mimi ni mwajiriwa ktk restaurant kama mpishi,sasa nataka kujiajiri ,kufungua mgahawa wenye uwezo wa wageni wa kukaa kama watu kumi na tano ,na natarajia kuuza bites na juices na soda bites ni kama cakes,samosas,pizzaz biscut home made,huo ni ufupi tu wa bidhaa zangu,je ni biz yenye mafanikio?ushauri p'se

Mkuu hiii Ndo the First and best method ya kupata wapata wazo la biashara, na mara nyingi watu wanao tumia ujuzi wao kujiajili wanakuwaga na % kubwa ya kufanikiwa, Uko nchi gani vile
 
Mtoto wa kaka yangu alifeli kidato cha 4. Nataka nimfungulie ofisi. Je, kati ya saluni ya kiume na biashara ya mitumba ipi inalipa vizuri? Kiasi ninachotaka kumpa ni Tsh 3,000,000/. Na kama mtaona(wana-jf) kuwa labda hicho kiasi hakitoshi, naomba mnipe wazo mbadala ili tumuokoe kijana huyu. Maana amekosa uelekeo kabisa.

Nachokushauri,kama hana mwelekeo makesure ana mwelekeo kwanza otherwise hata hiyo biashara unayotaka kumfungulia itakosa mwelekeo.Ni vizuri kum assess kama Chasanya alivyosema hapo juu.# team successful one
 
Back
Top Bottom