Karot
JF-Expert Member
- Mar 6, 2017
- 1,159
- 1,309
Habari za majukumu wakubwa na wadogo.
Kichwa cha habari chahusika.
Ilikua siku ya Jumamosi mnamo saa 11 za jioni nimetoka na familia yangu nyumbani kuelekea kwenye sikukuu adhim.
Kwa bahati nzuri mbele ya safari folen ikasimamishwa ya magari kupisha watoto wanaovushwa barabara. Wakati tunasubiri watoto wale wamalizike kivuka ghafla nilisikia mshindo wa kugongwa na gari aina ya Alphard ikanisukumiza mbele ambako kulikua na gari nyingine aina ya land cruser. Gari yangu ni I.S.T.
Kwa bahati mbaya gari yangu iliumia nyuma na mbele ambako mbele kulisababishwa na ule msukumo uliotokea baada ya kugongwa. Sasa alinigonga akaniomba tusishirikishe polisi twende kwa fundi wake tukamalizane mimi na yeye. Mimi nilikubaliana na ile hali, lakini cha kushangaza jana usiku majira ya saa nne nilipigiwa sim ya kwamba kuna barua yangu ya kunitaka niripoti kituo cha polisi.
Sasa nikawa najiuliza inamaana huyu mtu kaenda kutengeneza mazingira ya kwamba asinitengenezee tena gari yangu? Nilijaribu kumpigia sim alijibu ya kwamba yeye aliongea na bosi wake kwamba asikubali kosa la kutengeneza gari mbele wakati kosa lake kaigonga nyuma.
Sasa na mimi nikajiuliza inamaana mbele niliigonga mimi au yeye ndo kaja kunisababishia kuigonga gari yangu? Hapa nilichowaza ni kwamba keshaenda kutengeneza mazingira na polisi ili nikose haki zangu. Ndo nikaamua kuja jukwaa hili naamini nitapata msaada wa kisheria ili nijue pakuanzia.
Nakaribisha maswali, maoni pia kama una mawazo yoyote ya kujenga nambie kipi nifanye ili nishinde kesi hii...
NB: Shahidi niliekwenda kugonga gari yake baada ya mimi kugongwa namba zake ninazo.
Kichwa cha habari chahusika.
Ilikua siku ya Jumamosi mnamo saa 11 za jioni nimetoka na familia yangu nyumbani kuelekea kwenye sikukuu adhim.
Kwa bahati nzuri mbele ya safari folen ikasimamishwa ya magari kupisha watoto wanaovushwa barabara. Wakati tunasubiri watoto wale wamalizike kivuka ghafla nilisikia mshindo wa kugongwa na gari aina ya Alphard ikanisukumiza mbele ambako kulikua na gari nyingine aina ya land cruser. Gari yangu ni I.S.T.
Kwa bahati mbaya gari yangu iliumia nyuma na mbele ambako mbele kulisababishwa na ule msukumo uliotokea baada ya kugongwa. Sasa alinigonga akaniomba tusishirikishe polisi twende kwa fundi wake tukamalizane mimi na yeye. Mimi nilikubaliana na ile hali, lakini cha kushangaza jana usiku majira ya saa nne nilipigiwa sim ya kwamba kuna barua yangu ya kunitaka niripoti kituo cha polisi.
Sasa nikawa najiuliza inamaana huyu mtu kaenda kutengeneza mazingira ya kwamba asinitengenezee tena gari yangu? Nilijaribu kumpigia sim alijibu ya kwamba yeye aliongea na bosi wake kwamba asikubali kosa la kutengeneza gari mbele wakati kosa lake kaigonga nyuma.
Sasa na mimi nikajiuliza inamaana mbele niliigonga mimi au yeye ndo kaja kunisababishia kuigonga gari yangu? Hapa nilichowaza ni kwamba keshaenda kutengeneza mazingira na polisi ili nikose haki zangu. Ndo nikaamua kuja jukwaa hili naamini nitapata msaada wa kisheria ili nijue pakuanzia.
Nakaribisha maswali, maoni pia kama una mawazo yoyote ya kujenga nambie kipi nifanye ili nishinde kesi hii...
NB: Shahidi niliekwenda kugonga gari yake baada ya mimi kugongwa namba zake ninazo.