Los técnicos
JF-Expert Member
- Sep 14, 2014
- 3,010
- 2,604
Huyu bwana kiufupi katoa connection, sijui kwa nini kuna baadhi mmemchukulia poa?Kama uko tanga ni uzembe wako kukosa ugali
1. Nenda kiwandani tanga fresh kange jeshini pale muulizie kessy jieleze muombe kazi ya kupakia maziwa ya kwemda dar kila siku jioni, hukosi 10k mpaka 15k. Kila siku gari mbili au tatu zinaondoka msuli wako tuu kupakia
2. Nenda kiwanda cha podoa, duga mwembeni kila siku wanaandikisha wafanyakazi 7000 kwa siku ukikomaa kupatana kama hujui kuonge 5000, mchawi barua ya mtendaji na kopi ya kitambulisho.
3. Nenda depo ya bia pale kwa minchi kama unaenda misitu, kuna kushusha na kupakia kreti za bia kila siku hukosi kazi.
4. Una lesen ya piki piki na wadhamin nenda pale pale kwa minchi kabla ya depo ya bia kuna wahind koko wanauza pik pik wanatoa za mikataba, ushindwe wew kuwa boda boda
5. Nenda amboni kwa liemba kiwanda cha chokaa, kazi zakutosha nunua mask na jipende kwa maziwa maana kuna vumbi la kutosha kila siku watu wanaacha kazi hakuhitaji connection
6. Kiwanda cha IPPTL kange jeshini kazi zipo kaongee na walinzi vizur mchawi barua na wadhamini
7. Nenda stand barabara ya 10, omba kazi za ukonda dei waka kuna costa za kwenda mlalo na korogwe vijana weng hawataki kazi za kulala kwenye costa mkifika mlalo, nenda wakujue jenga uaminifu kazi zipo
8. Nenda soko la mlango wa chuma kwa Mbilu ana fuso za kutosha omba kazi kaa kushoto hana uchoyo yule mzee kikubwa uaminifu tuu
9. Tanga wanawake wanapenda kulea vijana, nenda 15 au ya 8 maeneo ya maua pale, jipitishe vaa kisharobaro jioni wakikuona tuu umeula. Ila ujue kusimamia ukucha.
Tanga kulala njaa au kufa maskini ni kujitakia