Nahitaji maombezi

Tatizo linalokusibu ni nini? Je ni uchumi, elimu, ugonjwa? Imani yako ndio itakuponya. Kiukweli kupona ugonjwa kwa njia ya imani sio jambo jepesi inabidi uwe na imani haswaa

Mama Helen white anasema unapokua kwenye maombi au Mfungo ukiombea jambo Fulani ona ilo jambo limeshaisha, usifikirie kuhusu ukubwa wa tatizo fikiria ukubwa wa Mungu juu ya ilo tatizo, usisubiri upone completely ndio ujue umefunguka anza kupiga hatua na kua na furaha (tatizo hujasema shida ni nini yaweza kua ni personal).

Lakini inahitaji uwe na imani haswaa au nenda kwa Mwamposa maana kwenye imani tunasema ukiona jambo linakua gumu kwako na wewe unganisha nguvu za watu wengine.
 
Nachoweza kukushauri ni kuwa usichoke kuomba. Kila uombapo muombe roho mtakatifu akusaidie kukuombea kwa Mungu.

Muombe pia akusaidie upate macho ya rohoni ili uweze kujua tatizo ni nini, maana kuomba tu bila kujua tatizo ni sawa na kunywa dawa bila kujua unaumwa nini.

Kwa kuamzia, Mrudie Mungu, umkubali Yesu awe bwana na mwokozi wa maisha yako.
 
I feel you mkuu, hio hali sio pekee ako unapitia wengi tumepitia na tunapitia na hiki ulichokifanya ni hatua nzuri ya kuanza mabadiliko achana na wanaokukatisha tamaa pia hawa manabii na mitume sina hakika nao sana maana mimi nimexepirience hayo yote kama umeamua kumgeukia Mungu maombi ya kweli ni yale unayoomba mwenyewe unaweza usiwe unaona matunda unayotarajia lakini huenda usingeomba basi ungekuwa na hali mbaya kuliko uliyonayo sasa, kikubwa endelea kumwomba mungu kwa kadri ya unavoamini muda ukifika atatufungulia milango.

Amiin
 
Tatizo linalokusibu ni nini? Je ni uchumi, elimu, ugonjwa? Imani yako ndio itakuponya. Kiukweli kupona ugonjwa kwa njia ya imani sio jambo jepesi inabidi uwe na imani haswaa,
Mama Helen white anasema unapokua kwenye maombi au Mfungo ukiombea jambo Fulani ona ilo jambo limeshaisha, usifikirie kuhusu ukubwa wa tatizo fikiria ukubwa wa Mungu juu ya ilo tatizo, usisubiri upone completely ndio ujue umefunguka anza kupiga hatua na kua na furaha (tatizo hujasema shida ni nini yaweza kua ni personal).

Lakini inahitaji uwe na imani haswaa au nenda kwa Mwamposa maana kwenye imani tunasema ukiona jambo linakua gumu kwako na wewe unganisha nguvu za watu wengine.
Nakazia asome huu mstari. 1Yohana 4:4
 
Majaribu Ni mtaji wa kuongeza Imani..

Mungu hupanga kila kitu kwa wakati wake... Hapo inataka uvumilivu (kusubiri/ kutokata tamaa, kutochoka)

Sijui kilichokusibu lakini jua kwamba wapo walio pabaya hata zaidi yako.. .lkn kuvunjika moyo ukachoka ndio hatua kubwa Sana ya kumpa ushindi adui yeyote!

Watakuja kukuombea lakini Tiba ya kwanza kabisa inatokana na wewe mwenyewe kuamini kwamba utashinda na yatapita!

Pole sana

Sent from my TECNO CD6 using JamiiForums mobile app
 
Ungekuwa unaamini mizimu ningekuconect na babu yangu unajua tatizo ni nini onspot, unajua kabisa nini inaweza kuwa solution, ila tofauti na hapo basi we endelea kuomba tu kuwa na imani zaidi amini unachokiomba kinafanya kazi, amini maombi yako yanasikiwa, amka ukiwa na moyo wa ujasiri kuwa maombi yamefika yanapostahili.

Huenda tatizo linazidi kuwa tatizo japo unaomba sababu unaendelea kuliona ni tatizo haujaliangalia kama limeisha sababu ya maombi yako kujibiwa.

Hebu amini maombi yako yamefika panapostahili, kisha jipe siku moja ya kesho amka ukiamini kila jambo solved na fanya kwa kuamini kila jambo solved nadhani utapata mwangaza.
 
Ungekuwa ni jinsia ya KE ningekupa ramani ili uje huku niliko. Hakika ningekufanyia maombi maalum ya watu wawili tu na kupona kabisa hilo tatizo lako.
 
Sikia ebu relax muda wakuwaza tofauti acha uo muda wakufikiria ujinga acha wewe sikiliza hii radio itakuunganisha na kristo Tzgospel
 
Mshukuru Mungu tu. Hawa jamaa wa Mungu Kwanza Online Radio wanakua na maombi Kila baada ya one hour, nawasikiliza sana. Jaribu kuwasikiliza na wewe. Wana maombi na Gospel NZURI sana za kufariji.
 
Muamini MUNGU ACHANA na jokes za humu

15233021647728.png
15164598683587.png
 
Habari za muda huu?

Nahitaji msaada wa maombi ili Mungu anisaidie, napitia kipindi ambacho sielewi nifanye nini.
Nimeomba nimefunga lakini sioni badiliko lolote nahitaji msaada sana katika hili maana sina option nyingine kabisa.

Nikipata msaada wa mtu mwenyewe moja kwa moja ntashukuru sana awe mchungaji, mtume, nabii au muumini wa kawaida tu maana naamini Mungu anaweza kumtumia yeyote. Anaewiwa kunisaidia mzigo huu karibu.

Tafadhali msinielekeze namna ya kusali ama vipi maana nimeomba usiku na mchana inawezekana sijaomba vizuri kiasi cha kufikia kiwango cha kupata msaada nnaohitaji lakini nilipofikia nimechoka sasa siwezi tena mwenyewe nahisi/naamini nahitaji msaada wa watu wengine ili kuinuka hapa.

Asantee natanguliza shukurani.

Endelea kuomba yeye hachelewi wala hawai
 
Maombi yenye nguvu ni kutoa sadaka/misaada kwa jamii (Yatima, Wagonjwa, wenye shida/uhitaji mbalimbali).

Jitahidi urudishe tabasamu kwa jamii wenye uhitaji na Mungu atakurudishia tabasamu maradufu.
 
Pole.
Inawezekana Mungu aliishajibu maombi yako, tatizo lako hukuisikia sauti ya Mungu.

Pengine uliambiwa wasiliana na fulani au fanya kitu fulani ila ukashindwa uanzie wapi.

Omba maombi ya kufunguliwa, kama uko dar nenda hapo kimara korogwe wapo waombaji.
 
Mwenyezi Mungu akutangulie.Japo hatuna maneno mazuri na ya kuvutia tusisite kuomba.
 
Habari za muda huu?

Nahitaji msaada wa maombi ili Mungu anisaidie, napitia kipindi ambacho sielewi nifanye nini.
Nimeomba nimefunga lakini sioni badiliko lolote nahitaji msaada sana katika hili maana sina option nyingine kabisa.

Nikipata msaada wa mtu mwenyewe moja kwa moja ntashukuru sana awe mchungaji, mtume, nabii au muumini wa kawaida tu maana naamini Mungu anaweza kumtumia yeyote. Anaewiwa kunisaidia mzigo huu karibu.

Tafadhali msinielekeze namna ya kusali ama vipi maana nimeomba usiku na mchana inawezekana sijaomba vizuri kiasi cha kufikia kiwango cha kupata msaada nnaohitaji lakini nilipofikia nimechoka sasa siwezi tena mwenyewe nahisi/naamini nahitaji msaada wa watu wengine ili kuinuka hapa.

Asantee natanguliza shukurani.
Unakosea unaposema umeomba lakini huoni badiliko lolote. Ukisema hivyo maana yake ni kuwa unampangia Mungu kutoa majibu! Ukiomba, subiri, Mungu anajua muda wa kukujibu. Lakini pia yawezekana ameshakujibu, ila wewe hujaona kwa macho ya kibinadamu.

Kuna mambo mengine yanaonekana kiroho lakini kibinadamu hayaonekani. Majibu yanaweza yakawa: ili tatizo lako liishe fanya kwanza jambo hili; hapa unaweza kuambiwa na mtu yeyote au ukaona kwenye ndoto.

Mambo mengine hayana majibu ya moja kwa moja, isipokuwa mpaka upitie intermediate stages. Yawezekana jambo linalokusumbua suluhisho lake ni rahisi na linaweza kutatuliwa katika mazingira unayoishi. Unaweza kutumia nguvu nyingi kumuomba Mungu, kumbe tayari alikwisha kukupa majibu siku nyingi.
 
Back
Top Bottom