Nahitaji kupata Majarida ya "Sani"

Nahitaji kupata Majarida ya "Sani"

Lubengera

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2019
Posts
1,073
Reaction score
1,708
Kichwa cha habari kinajieleza,

Mtakumbuka miaka ya nyuma kulikuwa na jarida la Sani, ambalo lilisheheni vituko vya kina, Madenge, Pro Ndumilakuwili, Lod Lofa, Pimbi,Ma Born Town na Ma Bush Stars, Betina na Mwenzake Zena, na mengine meengi.

Basi kwa mwenye archives ya magazeti haya, au kujua wapi naweza kuyapata kwa gharama nafuu, tafadhali naomba tuwasiliane.

Nataka nirudie tena kuyasoma, yalikuwa hayachoshi!
 
Mkuu nyumbani yapo maana mama alikuwa hapitwi nayo miaka ile ya 1995's yakitoka mara moja kwa mwezi mpaka miaka ya 2005's lilipoanza kutolewa kama gazeti. Akimaliza kusoma tu zamu ya watoto, nipo mkoa kikazi kama utakuwa hujayapata mpaka tar 15 nitakupatia. We upo mkoa gani?
 
Mkuu nyumbani yapo maana mama alikuwa hapitwi nayo miaka ile ya 1995's yakitoka mara moja kwa mwezi mpaka miaka ya 2005's lilipoanza kutolewa kama gazeti. Akimaliza kusoma tu zamu ya watoto, nipo mkoa kikazi kama utakuwa hujayapata mpaka tar 15 nitakupatia. We upo mkoa gani?
Na Wenye majarida ya Bongo na Tabasamu nao waonyeshe upendo kwa wajomba.
 
Mkuu nyumbani yapo maana mama alikuwa hapitwi nayo miaka ile ya 1995's yakitoka mara moja kwa mwezi mpaka miaka ya 2005's lilipoanza kutolewa kama gazeti. Akimaliza kusoma tu zamu ya watoto, nipo mkoa kikazi kama utakuwa hujayapata mpaka tar 15 nitakupatia. We upo mkoa gani?
Mkuu hata mimi nahitaji..nipo mwanza..lets arrange napataje.
 
Mkuu nyumbani yapo maana mama alikuwa hapitwi nayo miaka ile ya 1995's yakitoka mara moja kwa mwezi mpaka miaka ya 2005's lilipoanza kutolewa kama gazeti. Akimaliza kusoma tu zamu ya watoto, nipo mkoa kikazi kama utakuwa hujayapata mpaka tar 15 nitakupatia. We upo mkoa gani?
Mkuu nipo dodoma kwa sasa! lakini hakuna kinacho shindikana
 
Itakuwa vyema, haya majarida ya Sani huwa nikienda home huwa nayarudia na kurudia kuyasoma na kucheeka mwenyewe. It's one way of mind refreshment
Hahah sure mkuu,enzi ambazo mzazi anakupa gazeti ulisome akiwa hana wasiwasi No nudes,no lugha za matusi just entertainment tu

Maisha yalikua poa sana.
 
Hahah sure mkuu,enzi ambazo mzazi anakupa gazeti ulisome akiwa hana wasiwasi No nudes,no lugha za matusi just entertainment tu

Maisha yalikua poa sana.
Unajua ile mzazi anakuja nalo alafu hajamaliza kusoma siku hiyohiyo na asubuhi anaenda nalo kazini, tuliobaki nyumbani tunaomba akirudi awe amemaliza ili nasi tupate kuchungulia, nione madenge kamwingiaje mzee wake, pimbi kaopoa mshangingi wa aina gani alafu mission ikafeli, ndumilakuwili nae katika harakati zake za wizi bila kusahau maneno ya shombo ya mzee Lodilofa na kigari chake kile kwa wazee wenzake hapo bado hujamalizia tambo za Betina kwa Zena huku bi mkubwa wake Betina akila serveillence na ungo wake home kwa Zena kumnyong'onyesha siku ya pambano mwanae ashinde😂😂😂😂
 
Zama zangu nilikuta Ni gazeti la sani si jarida. Visa vya madenge, lodi lofa, bush stars, kifimbo cheza na wachafuzi wa lugha, Zena na Betina.

Ila jarida nimekumbuka lile la Bongo tulikuwa watoto story za kiutu uzima lakini hivo hivo tunazifutatilia kibishi .

Good old days indeed
 
Back
Top Bottom