Nahitaji Kujiunga na upadre

Nahitaji Kujiunga na upadre

Nina mengi ila naona utakata tamaa mapema. Elewa 8 kati ya 10 ya unaowaona mapadre sio mapadre. Pa kuanzia nenda kwa paroko wako akupe miongozo vizuri kwani kila shirika lina mtindo au karama tofauti.
Mkuu fafanua tu ali ajue vizuri usimfiche kitu kabla ya kuingia huko
 
Una degree ya kujisomesha mwenyewe halafu unataka kujiunga na upadre, unatania au!!! Wingi wamesomeshwa na mashirika eg Jesuits, utaona aibu mwenyewe kujitoa inabidi ujiunge. Ni uamuzi mzito kuishi maisha yote bila mahusiano na mwanamke. Tumia degree yako ujiendeleze ukitekeleza amri ya Muumba kuzaa na kuijaza dunia yake kwa kutumia mahesabu kulingana na kipato chako
 
Mkuu inaonekana una maarifa na hizi mambo embu toa experience mkuu, maana najua humu watu wa kila idara wapo
Nenda kwenye parokia yoyote umtafute padri atakupa maelekezo vizuri.

Humu ni vigumu kutambulika vizuri.
 
Kwanza inavyoelekea huna sakrament hata moja!
Kama unabisha jibu maswali yafuatayo!
1. Nitajie sakrament saba za kanisa katoliki
2. Daraja takatifu ni nini?
3. Taja alama za kanisa katoliki
4. Nini tofauti kati ya dhambi na dhamiri
5. Ushirika Wa watakatifu ni ushirika gan?
Ukinijibu maswali hayo! Ni PM namba yako kesho ukaanze malezi, ukishindwa nenda kanisani ukatubu uanze mafundisho ya ukatoliki.
Maswali mazuri Mkuu.
 
Mkuu hiyo ni propaganda!

Sijui kwanini watu hudanganya this much?

People need to be honest!

Ile ni kazi,hakuna mambo ya kipawa dunia hii!Hiyo ni utopia!
Mbona ueleweki kijana..???
Kila mahali wewe ni kupinga,hata ujulikani unasimamia kitu gani..!!!

Wewe uko kwenye lile kundi la kina Ngombale Mwiru..???

Hebu jielekeze kwenye msimamo wako ili tujue tunadili na mtu wa aina gani.
 
Mbona ueleweki kijana..???
Kila mahali wewe ni kupinga,hata ujulikani unasimamia kitu gani..!!!

Wewe uko kwenye lile kundi la kina Ngombale Mwiru..???

Hebu jielekeze kwenye msimamo wako ili tujue tunadili na mtu wa aina gani.


Jiwe la Majiwe

Ni wewe ndio hunielewi,usi generalize wanadamu wote.Kama ni kweli ukisemacho,ungekuta rebuttals kutoka kwa watu mbalimbali against me,ila that is not the case!

Acha kua personal namna hiyo!

Critique hoja yangu kua kazi ya ukasisi ni kazi kama kazi zingine!

Kwani Ngombale Mwiru sio mwanadamu?Au ni ng'ombe yule?Maana wewe ni mwanadamu sana zaidi ya wanadamu wengine kama Ngombale na mimi na etc?

Kwani siruhusiwi kupinga kitu?Ni haki yangu kupinga kama wewe unavyounga,sioni sababu ya wewe kua bitter namna hiyo!It is really hilarious!

Nipe critique iliyoshiba kwamba ukasisi ni kazi "special" sana zaidi ya kazi zingine?Mungu hajawahi tuma mtu,wanadamu wamejituma wenyewe kwa kujiewekea masomo ya kusoma kwa utashi wao wa kibinadamu then wakimaliza eti wameitwa na "Mungu" kumuhudumia!Ni kazi kama mimi niliyesomea udaktari nikapata cheti nikawa admitted to practice kuhudumia wanadamu wenzangu!

Huyo mungu aliewatuma aliongea na nyie lini?Barua za uteuzi ziko wapi?Huyo Mungu yupo wapi kwanza?Ni dini gani huyo Mungu wenu?

Wanafiki wakubwa!
 
Mrejesho? A serious man angekuwa ashachukua hatua mpk sasa!
 
Mkuu kama unataka kuwa Padre, una degree na bado mashirika yao umeshindwa kuyajua basi nakushauri usiende huko, huna wito. Yaani hata padre wako umeshindwa kuongea naye akaku-guide? Hata huko kanisani unaenda kweli?
Labda sio mkristo, anafananisha mavazi yao na baibui nyeupe!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama kweli una wito anza kwanza na kuwa "bruda" ni kipindi kizuri sana na upige falsafa ili ujue kama unaweza kusema "Bwana awe nanyi " Fanya maamuzi ya kina huku ukitafakari kuhusu wanafalsafa walisema nini .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni msaada mkuu, siunajua unakuwa unapitia mambo mengi mpaka unajitambua mkuu??
Ndiyo tatizo la vitoto vinajifunza kuposti humu JF, yaani humjui hata Mwenyekiti wa jumuia mtaani kwako,akupe mingozo achilia mbali kama humjui katekista,paloko au Padre,Mods futeni huu upuuzi haraka,maana jukwaa hili linataka kuwa kichwa cha mwendawazimu.
 
Ushahuri mzuri, ila ndo kuanza kujipendekeza wengine hatujazoea ila taratibu mambo yataeleweka. Ila nilitaka nipate connection ya moja kwa moja
Ninyi mnaotafuta connection kama hivi ni wa kuchunga sana, kuna jambo zaidi ya upadre. Si ajabu ukawa miongoni mwa wale wanaodhani kuwa kwenye upadre ndipo pa kufichia makasoro fulani fulani, ndio ninyi baadae mnaotukanisha wito wa upadre.
Natumaini hukufanikiwa kwenda huko. Nakuombea kila la heri kwenye maisha mengine, lakini siyo upadre. My instinct.
 
Ninyi mnaotafuta connection kama hivi ni wa kuchunga sana, kuna jambo zaidi ya upadre. Si ajabu ukawa miongoni mwa wale wanaodhani kuwa kwenye upadre ndipo pa kufichia makasoro fulani fulani, ndio ninyi baadae mnaotukanisha wito wa upadre.
Natumaini hukufanikiwa kwenda huko. Nakuombea kila la heri kwenye maisha mengine, lakini siyo upadre. My instinct.
Eti muda wote alikua wapi au ndo ameona bora akalishwe na waumini parokiani kitaa maisha magumu
 
Back
Top Bottom